Jopo litakalotwikwa jukumu la kuchunguza sakata inayozingira utendakazi wa jamaa anayedaiwa ni polisi bandia Joshua Waiganjo linatarajiwa kuanza kazi yake na kuwasilisha ripoti yake siku 10 baadaye kama ilivyoagizwa na Rais Mwai Kibaki. Haya yanajiri huku mkuu wa polisi mkoani kati Francis Munyambu akiwa bado hajajitokeza kuzungumzia anachokifahamu kuhusiana na sakata hiyo iliyochipuza katika eneo alikowahi hudumu kama mkuu wa polisi mkoani Rift Valley.
5 янв 2013