Mwenyezi Mungu atujalie na kutulinda Daima hii ni nyakati ngumu saana ila kwa Uwezo wa Mwenyezi Mungu atatuongoa na kutujalia kuishinda kaumu ya Makafiri ila Afrika sisi ndie wateule wa Mwenyezi Mungu tusimamie na kukomesha maasi Maana Mwenyezi Mungu atatuokoa tuangalie Dunia ilipo kutokana na uasi Mwenyezi Mungu ataleta Adhabu kuu, huu ni wakati tusimame pamoja hakuna Uongo tena hakuna Vitisho tena maana saa ya Ukombozi ndie sasa tusimamie kweli ya Mungu mkuu
Nachokiona kibaya ni kuwa Uchumi unapoelekea ni mbaya zaidi ya miaka ya 80, Idadi ya wasio na ajiri inazidi kuwa kubwa, Uchumi unakuwa polepole sana tena kwa wawekezaji wachache ambao wengi ni wageni, Wimbi la mwaka 80 tulilivuka salama wakati Jamii ya Watanzania hawakuwa na taarifa za kutosha (Habari zilikuwa zinadhibitiwa ,Hakuna magazeti, Redio ni Moja tu RTD na hakuna Upinzani wa kusema ), Mikopo ya ( Ujenzi wa Reli ya SGR, Bwawa la Rufiji, Ununuzi wa Ndege za ATC,Daraja la Busisi na Tanzanite, Barabara za Mwendokasi ,na Ujenzi wa Mji wa Dodoma na Uhamaji wa Wafanyakazi ) hatuwezi toka salama kwenye Marejesho ya Madeni.
Remember Mw. Nyerere once told MPs who wanted him to imprison Dar University students who were involved a strike/ demonstration. He asked them to read the placard and discuss the message. Instead, he advised them that : “ ideas are never crushed by rungus but by superior ideas!
Nigumu sana kwa CCM kukubali upinzani kuwepo, kwani tokea Zamani kikiwa TANU zama za Nyerere 1965 hawakupenda kuishi maisha ya Ushindani wa hoja bali walitaka watawale wenyewe hata wa kikosea wajitatue, Mwaka 1992 tulilazimika kuingia kwenye Mfumo wa Vyama vingi na ( Uhuru wa Habari,Kumiliki Biashara au Mitaji n.k) ilikuwa ni mkwamo tu wa uchumi wanatafuta pa kutokea bila kujua walipo kosea.
Inaumiza sana. Lakini kwani wakati wa kesi ya ugaidi aliyozushiwa Mbowe waliofanya ile kazi siyo huyu igp wa sasa na dci wa sasa? Hivi si inaweza kuwa kwamba aliyewateua alitumia kigezo cha uzoefu wao katika mambo ya namna hii?
Uvunjwaji wa katiba na sheria za nchi umekua tishio kwa wananchi,kila mtu anakimbia wala hajui anakoelekea kwa kuogopa adhabu ya kesi za uhaini ambapo adhabu yake ni kifo! Je,watakaokamatwa na kuuawa ni wangapi?! Watoa amri wakinyamaza, wasiojulikana wanapotea, Watoa amri wakiongea wasiojulikana wanaibuka upya! Mheshimiwa Rais tuliyekupa dhamana,una uhakika na tamko la IGP kwamba MDUDE, MWABUKUSI,SLAA,NA MADELEKA,na NSHALA sio wanaharakati bali ni Wahaini wenye vitendea kazi,silaha,na majeshi hivyo wanatosha kuwa WAHAINI wakae ndani na kisha wamyongwe?!!
Hao polisi hawana uhuru wa kukataa wakiagizwa na CCM ni kutii tu sio kukataa wakiagizwa na kutekelezwa sasa sisi wananchi tunawalaumu polisi buree3eee tatizo juu na huo ndio udikteta
Ngurumo una pwenti kubwa hapa. Kimsingi, wanakamata mbuzi mwisho wa siku watajikamata. kumbuka mchezo wa kuigiza wa vitimbi wa nchi jirani. Mzee mmoja alipenda kufukuza wafanyakazi wake. Siku moja alifukuza wote. Alishangaa kujikuta yuko peke yake, alimua kujifukuza mwenyewe akisema "na mimi nitoke' akajifukuza.
Mtumishi unachokisema ni Sawa kabisa CCM itafika sehemu itamkusanya mwananchi Kwa garama sana, na itatumia nguvu ya pesa ambayo ni kodi ya wananchi wake pasipo mafanikio bali hasara tupu
ASANTE KWA KUWAWEKA WAZI.INAWEZEKANA WATIMIZE WAJIBU WAO KWA UMMA MZIMA WAWATANZANIA.WAWAACHIE HURU,KWANI TANZANIA NI YETU SOTE NAKUILINDA NI JUKUMU LETU SITE KWA MANUFAA YETU NA VIZAZI VYOTE VIJAVYO.
Je Zanzibar ilifanya mapinduzi je? Mbona hapakuepo na kesi ya uhaini kwa wahusika mbona walisifiwa kwa matendo yao yakaitwa mapinduzi matakatifu nini maana yake
Kama kupindua serikali ni neno la kisiasa jee unaposema vituo vya polisi vitiwe moto na office za ccm zichomwe moto pia maneno hayo ni kisiasa??? What the hell are you talking
Wanatumwa. That's my point. Polisi huwa hawajitumi. Wanaishi kwa amri. Lakini wakati mwingine wakubwa wa polisi wanajiongeza kwa kujiongezea majukumu. Mwenye amri asipowazuia, maana yake amewaruhusu; wanaendelea.
Kwa akili yako unaamini Dr Slaa kama angelikuwa bado ni balozi wetu huko ng'ambo ananeemeka kwa mishahara, posho na "heshima" ya ukuu hayo mambo ya bandari angeyesema au kuyakosoa???
Wee bwana hatutaki siasa kwenye bandari zetu please!.. Wewe ni mnafiki na kwa kutumiwa na WAHUNI na hii maelezo yako kuna kundi huwa unalitumikia.. Kwani chanzo cha hizi kesi si ni mkataba? Kwanini husemi wafute mkataba?!! Mpaka unafika hatua unawaita ‘mbuzi’ na hivyo kuna ‘swala’ na ‘tembo’ yaani ionically unawadogosha!
Tatizo ni DOGO SANA akili ndogo inapo iongoza akili kubwa mwenye akili ndogo atatumia nguvu ccm wameishiwa mbinu kwakifupi zambi inawatesa mateso maisha magumu ya watanzania ni matunda ya chama Chao hicho tutajuana huko tuendako
Una maneno mengi sana mzee, lakini huna action, huna hatua yenye matunda ZAIDI ya propaganda za hapa kwenye channel yako. Pole sana mzee, nameombea mpambanaji wa kweli (Bony Mwabukusi) huyo namwombea kwa mungu maana hana chuki na mtu Bali ana mawazo chanya na watanzania.
@@AnsbertNgurumoUnapandikiza mbegu za mfarakano tu. Mambo yakiharibika hapa kwa sumu unayopandiliza, hutakuwepo. Njoo uyaongelee huku kama alivyo Lisu, Slaa, Lema na mimi.
@@johannesishengoma1232 😂😂😂😂😂😂Wewe Ishengoma 😂😂😂😂😂 Ishengoma huna level hizo za mtu kama Dr .Slaa , Lema , Hon. Lissu na Ndg Ansbert Ngurumo Mwanahabari Nguli
@@AnsbertNgurumoansbert tunakusikiliza sana na unatusaidia pia kusamaraiz mengi ya kiwiki kimiezi kuwa habari fupi yenye kuweza kuelewa sisi wananchi ambao muda wote kuwa ktk mitandao on line au kusech habari nishida bando ni ghali sana tunakushukuru watu wakawaida na wananchi wa kawaida.kaza buti twende mzee wetu
Mzee habari yako? Mimi mzalendo, mwanaharakati, naona wanaharakati wenzangu wamekamatwa sasa wewe unayemchukia JPM badala ya wahalifu mbona sijakuona ukitoka mstari wa mbele kutetea au kushawishi watu waingie mtaani? Au na wewe ni lioga pia? 😂😂
@@saheedali7467 MWENYE CHANNEL. ANAOGOPA KUITWA MHAINI🤣🤣🤣. HUYU JAMAA NI SAWA NA KUSEMA (MBAYA LAKINI MZURI). ANAYOLILIA NDIO MAMBO AMBAYO JPM ALIYAPIGA VITA... SIO WATU ALIPIGA VITA WIZI WA MALI ZA WATANZANIA, ALITETEA MTANZANIA WA CHINI KUFAIDIKA NA MALI ZA NCHI... AKAWAPIGA VITA WABAYA WOOTE WA WATANZANIA KUANZIA NDANI YA TANZANIA HADI NJE... LAKINI HILI JITU HAPA LINAMTUKANAGA KILA SIKU... MANENO YAKE UTASIKIA CHATO CHATO... RISASI RISASI... SASA HUA NASEMA JE BORA CHATO AU BORA KUPELEKA UARABUNI AU BANK ZA ULAYA AU WABEBE WAKAFUNGUE BIASHARA KENYA AU RWANDA? CHATO NI TANZANIA... HILI JAMAA LINA WIVU MBAYA NDIO HUO UNATUFIKISHA HAPA, WANAANZA KULIA TUMEUZWA, TUNAIBIWA... LAKINI TUNAUZWA NA KUIBIWA SIO SABABU YA HAWA WANAOWALAUMU YANATUPATA YOOTE HAYO SABABU YA WATU KAMA HAWA... HUA WANAMISLEAD WATU, YAKIGUNDUA YALIKOSEA HAYAOMBI RADHI... HAWA WASINGEMTUKANA JPM CHUKULIA MANENO YAO YA UKWELI LABDA ALIUA KWELI, JE ANGEWAUA KAMA WANGEKUBARI KUFANYA NAYE KAZI MOJA YA KUJENGA NCHI HII? WALIKUA WANAPINGA KILA KITU, SASA TUNATEMBELEA MOTO YANALIA TENA, BADALA YA KUOMBA RADHI WATANZANIA KWANZA WANABAKI KUPIGA KELELE NA KUENDELEZA MATUSI, CHUKI, WIVU, NA KUKOSA MAONO YA NCHI. KAMA MIMI NAWEZA KUJUA CHATO NI TANZANIA NA HAINA SHIDA IKIENDELEA NA MIMI MAKAZI YANGU SI CHATO... HILI LINASHINDWA NINI KUELEWA KAMA NI LIZALENDO?.MPINZANI LABDA TUSEME, KUWA MPINZANI SIO KUPINGA KILA KITU, MIMI SINA CHAMA NINI CHAGUA WATU BILA ITIKADI YA CHAMA CHOCHOTE, NAENDESHWA NA MAAMUZI YANGU SIO ITIKADI.. NINATAZAMA MTAZAMO WA KITAIFA SIO WA KIKANDA AU WA WIZI WIZI... MZEE KWANZA WAOMBENI RADHI WATANZANIA KWA KUTUTUKANIA JPM WETU, MMEMTUKANA SANA NA MIMI BADO NAUMIA SANA NIKISIKIA MNAMTUKANA KWA KOSA LA KARANGA NA FAIDA YA BILLION HUIONI UNAONA HASARA YA KARANGA. KUKOSA AKILI HUKO