Itoshe kusema tuna kikosi bora saaana msimu huu,,,Allah atufanyie wepesi tuweze kutetea mataji yetu na kufika mbali kwenye mashindano ya CAF. Kila la kheri wanajeshi wetu pamoja na benchi la ufundi, Ukawe msimu bora saanana wenye mafanikio
Pia kocha afanyie kazi makosa yaliyojitokeza kwenye goli la kwanza Aziz andambwile alishindwa kuruka na ikawa rahisi kwa mfungaji kupiga kichwa pila shida
Acha zako unazifahamu sheria za mpira wewe, mchezaji ukiwa nje ya pitch na madaktari wamefika hutakiwi kuingia uwanjani mpka akuruhusu refa ndo maana hata madaktari hawaruhusiwi kuingia uwanjani kabla hawajaitwa na refa wakiingia wanapewaga kadi nao, we husikii watangazaji wanasema hii kadi kajitakia, ilitakiwa aombe ruksa aingie ndo akae sasa yeye kaingia wakati refa karuhusu mpira
Hujui mpira, huyo mchezaji alipewa njano mara ya kwanza baada yakupata hasira na kuudundisha mpira kwa nguvu, pili aliumia akiwa nje ya kiwanja, kwa kujifanya refa haoni akabingirika uli atibiwe uwanjani kitu ambacho siyo sahihi hivyo kadi ya pili na kilichofuata ni red card. Sasa wewe unayejifanya shabiki wa yanga unapinga nini? AU WEWE KOLO?.