Mungu Ibariki Simba mwaka huu Kwa jina la Yesu Naiombea timu . ya Simba Tunaanza na Mungu tutamaliza na Mungu Viongozi, Wachezaji. na Mashabiki tuwe kitu kimoja ushindi wetu Simba nguvu mojaaaaaa ❤❤❤❤
Ifike mahali tuonyeshe ukubwa wa kweli wa Simba yetu ni miaka inaenda siku zinakimbia tutachezea viwanja vya watu mpka lini ifike mahali tuseme basi tupate wetu sasa nas tutambe zaidi
Magori mengi Kwa timu yangu msitufanyie Yale ya costal fungeni Kila mchezaji awe na kiu ya kupachika magori msimu huu ubingwa naona ukiamuliwa na idadi ya magori
Semaji habari? Kwanza kabisa maua kwa Ahmed Ali kwa kueka matumaini hai kwa wanasimba wengi ambao tulisusa hata kuja kwenye mitandao ya kijamii. Pongezi pia viongozi wetu wakuu wa timu hasa Raisi wa heshimu wa simba MO kwa kusisikliza maoni yetu na kuunda timu ambayo ni ya mapambano kusema ukweli. Sasa huu ubaya ubwela usiishie kwenye midomo tu iwe noma hasa nje ndani ya uwanja. Bingwa wa ligi Lazima awe mmoja tu lakini simba tulibweteka na tukajikuta tumepotea. Mambo matatu ya kuzangatia simba tukiyadhibiti basi tutarudi mapema anga zetu. (1) Wachezaji wetu na benchi la ufundi waambiwe mapema tu kwamba kila mechi ya ligi ya simba timu pinzani inakuja kucheza na simba kama fainali kwa sababu tatu kuu (a) Wachezaji wengi kucheza na simba ni nafasi ya kutafuta ajira ndani ya simba na kujitangaza pia kwa timu nyengine kwani mechi za simba zinafuatiliwa ndani na nje ya nchi. (b) Vile vile vilabu kadhaa vinapokea motisha kadhaa zikiwemo pesa taslimu kutoka kwa wapinzani wetu wakuu wa ligi ili wapambane kufa kuhakikisha tunadondosha points. (C) Wachezaji wetu wanapaswa kupewa elimu maalum ili kutokuja kutoka mchezoni kutokana na vitimbi vya Marefaree wetu ambao mara nyingi Yanga amekuwa bingwa kutokana na points kadhaa za wizi kupitia Marefaree licha ya kwamba yanga wana timu bora sasa hakuna ubishi juu ya hilo. (2)Siri ya Yanga ya Gamondi ni Mazoezi ya nguvu muda wote na jiitihada binafsi za mchezaji mmoja mmoja. Yanga kama wanakutana na timu inayocheza teamwork asilimia mia moja basi ni timu 🎉ya kawaida sana. (3)Angalizo ni kwa Wachezaji wa simba kujitunza nje na ndani ya mazingira ya kazi. Ligi ni kukusanya points luxury inakuja baadae. Ukiangalia mechi na coastal union backline yetu iliruhusu goalkeeper wetu kufikiwa kirahisi na hata mechi Yanga backline yetu ilichemsha hii inatupa kumbukumbu za machungu kutoka simba iliyopita. Nadhani kusiwe na kigugumizi sasa cha kumueka benchi beki ambae ni muendelezo wa matatizo kunako backline yetu. Lioneli Ateba mtu wa kweli kocha ana mawinga na midfielders wa kutosha sasa itakuwa busara kwake kumsimika Ateba kuwa namba tisa halisi wa kukaa pale kwenye box kuna mpira au hakuna mpira ili ashibe confidence kwani simba tunahitaji hiyo aina ya mshambuliaji.
Kwanini uwanja wetu wa Mo Arena haukamiliki?kila siku sisi ni watumwa wa Viwanja! Ninaomba fanyieni kazi uwanja wetu,kuna kipindi tulichanga fedha za kujenga ukuta wa uwanja imefikia wapi?
Ahmed Ally tunawaomba sana mjihadhari sana na huyo Manula kiwango chake limeporomoka vibaya sana sisi wanachama mashabiki na wapenzi Tunasema hatumtaki asipangwe kabisa ktk mchezo wowote wa ligi ya mwaka huu,
Kama uwanja ni mdogo hamuoni Kama hamtutendei haki wapenzi due limited number ya wate watezamaji?please angalieni the I'll conceived idea ;why tusitumie uwanja WA shamba la Bibi? economically mmechemka mno ;watazamaji 70000?huo ni utoto!