Kufuatia mgomo wa Madereva wa Mtandaoni Tanzania (TADO) unaoendelea kwa siku mbili sasa dhidi ya kampuni ya Uber, zaidi ya madereva 50 wamenyang'anywa magari na mmiliki wa magari hayo akidai kushindwa kuvumilia hasara kubwa anayopata.
Mkurugenzi wa kampuni ya Smart Rental Car, Fredy Emmanuel ambaye ndiye mmiliki wa magari hayo amechukua uamuzi huo kufuatia mgomo wa madereva wakidai kuendelea kukandamizwa na Uber kila iitwapo leo kwa kufanya kazi ambayo haina faida.
--
Dar24 ni chanzo namba moja cha habari kwa watanzania mahali popote walipo duniani. Kwa habari za uhakika kutoka nyanja mbali mbali tembelea www.dar24.com
#Dar24 #Dar24Media
18 сен 2024