Hivi hamna watanzania wengine wasomi zaidi ya hizi sura kila siku ndo hizi??Mbn watanzania tena wasomi wazuri ni wengi tu?Huu mzunguko tumeuchoka tunahitaji badiliko ya dhati na kweli ili kuleta maendeleo kwani wote hawa walikuwepo tangu awamu ya 4 kwa mzee wa Msoga na walifeli kwa sbb hawakuleta matokeo mapya yyte,tupo wasomi wengi huku nje angalieni tena na tunaweza kuiletea maendeleo Tanzania tukiaminiwa.
hizo ni siasa ndugu yangu, lazima ateue watu anao waamini, hawezi kuteua tu watu, siasa zina hujuma na fitna lazima awe na timu anayoijua, yenye uzoefu na anayoiamini
Kuna watu walitolewa tangu mwanzo Mama anaingia, wengine hatukuelewa kwa nini awatoe? Kama Kabudi na Lukuvi. Sasa kawarudisha! Rai yangu muda wote huu ambao hawakuwepo wangekuwa wamemsaidia sana, hivyo hakukuwa na haja ya kuwatoa. Kuendesha nchi ni kazi ngumu, Rais inabidi awe tayari kutembea na wachapakazi. Asiwe anawatoa kwenye nafasi watu wa namna hii wasaidie nchi kwenda mbele. Haisaidii kiongozi unapotaka kubaki na watu laini laini tu, nchi inakuwa haiendi. Bora lawama lakini nchi isonge mbele!!!
@@KulthumSalum-d6pAnaumwa huyu mama anatapa tapa alitoa watu wakaz kaweka watu wez wameiba sasa wanamgeuka wampindue ndio anashtuka Atakoma nabado tutashuhudia meng kat yahaya
Tanzania ina historia na baadhi ya watu wanaofanya vizuri wawapo kwenye utumishi wa serikali. Kama profesa kabudi hakustahili kuwa nje ya utumishi wa serikali, toka awamu hii ya sita inaanza. Maana ndio waliosimamia mazungumzo ya ukwepaji kodi uliokua unafanywa kwenye makinikia. Alisimamia vizuri sana. Hadi boss wa kampuni ile alikuja hapa nchini, akakubaliana kuilipa serikali ya Tanzania. Lakini kazi kubwa ilifanywa na kabudi na timu yake.
Hongera sana Mhe. Prof. Paramagamba Kabudi Ukweli ulivyo Wewe ni Jembe. Mhe. Rais wetu hakika amekuona Rais wetu nimwema sana. Ccm Oyeeeeeeeeeeeeeee ee.
Mabadiliko ya kila uchao hayasaidii.Tupate mabadiliko ya uchumi.Kila unaowapanga hawana msaada.Kwa Feleshi sawa kabisa kabisa tulikuwa hatuna Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Mama anaanza kurudisha vyuma vya Magufuli baada ya mwamba kuoza. Ila it is never too late, simlaumu mama maana transition ya kijinsia ina joto lake, kilichobaki Makonda ajitokeze kama yuko hai, ili kazi iendelee.
Unateuwaa watu walewale kila cku utapata utofauti gani hapo sawasawa kuchukua ela ufuko hu na kuweke mfuko mwngine kuna nini!? Hapo fukuza weka watu wapya tanzania ina watu milion 60 wewe unaangaika na ao ao kila cku jamanii da! Hi nchi kichwa cha mwenda waziximu
hali ngumu kimaisha kwa nani??? mbona wezako tunaishi vyema, na hali ngumu yako kimaisha kuifanya iwe rahisi jukumu la nani??? babako mzazi tu huwezi kumlaumu hai ngumu ya maisha kwanini umlaumu Rais ambaye hata hajui kuna wewe unaishi mahala, kaza matako, Mungu tu jasema mtakula kwa jasho, we unataka nini upewe vya bure?
@@filamupictures9349Endelea kufanya kazi vyema na muombe Mungu aendelee kukubariki hapo ulipo na uende mbali zaid, sio kila mtu ana nafas kma ulio nayo wewe au amebahatika kufika apo ulipofika wewe. Maisha ya mtanzania mmoja mmoja ni magumu licha ya kua kuna wachache wanamaisha mazuri. Mungu atubariki sote na aendelee kutulinda katika harakat zetu za kila siku🙏
Mheshimiwa Rais Mama Samia SULUHU HASSAN hongera sana kuwakumbuka wazee na waheshimiwa Lukuvi na parakabudi huo ndo msimamo thabiti usiyumbishwe KWA vile Wana maacount yao Kwenye mabenki!
WATANZANIA WENZANGU TUOMBE UZIMA HAYOA MAMBO YA MENGINE HUPNGWA NA MUNGU MWENYE NAFASI YA KUKA MWACHENI ALE PAMBANA KIVYAKO IKA KWAKWELI UPANDE WA WAZIRI WA FEDHA HATA MIMI SIJUI MAMA SAMIA ANAMPENDEA NINI YAANI MTAAN HATA MIRADI HAIENDI MFANO EMEME WAKANDARASI HAWALIPWI PESA ZAKO MIRADI IMESIMAMA
Hadi Mrundi atumbuliwe ndipo nione kafanya la maana. Huyu mhuni ndiyo sababu ya madeni, malipo ya fidia, kuporomoka kwa sarafu yetu na ugumu wa maisha ya Mtanzania wa kawaida.