Chakra ni nini?
Katika video hii utajifunza juu ya elimu ya chakra kama moja kati ya vituo muhimu sana vya safari ya meditation,
Ambapo kila chakra utaijua maana yake na faida yake pale utakapo ifungua mafanikio ni kwa kila mtu ambaye ni mwenye elimu za kiroho.
Wengi waliopo gizani kwenye elimu hizi basi utaona kwao mitihani na mambo mazito mazito hayaishi kwao.
Na kila panapokucha unakuta ni mtu mwenye mtihani mpya na mambo ya kusikitisha ambayo hupelekea wengine kufikia hatua ya kuamua kukufuru kisa tu kukosa maarifa.
Hivyo katika video hii nitakufundisha moja kati ya maarifa makuu kabisa yenye msaada mkubwa kwa maisha ya kila mtu na yenye muongozo mzuri katika maisha ya mwanadamu.
Vile vile usisite katika kufuatilia mafunzo haya kwani elimu ni bahari na ila manufaa kwa kila mazingira mtu aliyopo na jinsi unavyozidi kuiendea dunia na umri unavyozidi kwenda basi utatamani kama ungejua maarifa mengi sana kwa maana bila maarifa hakuna kitu kinaweza kuongozeka wala kwenda.
Hivyo siri ya kwanza kabisa ya mafanikio kwa mtu yeyote yule ipo kwenye maarifa kama huna maarifa wewe ni sawa na boksi na ili kuonyesha maarifa yako basi ni vema na ni bora zaidi yakawa na manufaa kwa watu wengi.
Kwa wageni basi channel na website zetu zinahusiana na maarifa salama ya juu sana kiroho na yenye faida kwa wengi na hasara kwa wachache ambao hata katika kutizama tu hawakuweza kuelewa kinahusu nini.
Kaa vema tuliza roho yako kuna mengi roho yako inataka kukwambia ambayo mwili na ubongo wako hazifahamu laiti ungeanza mapema kusikiliza roho yako basi ungependa uwe ni mwenye kuitaka shauri kwa kila hatua unayopiga katika maisha yako.
Kuna njia nyingi sana katika kuwasiliana na roho yako lakini most effective way ni kuongea na roho yako na kuweza kutulia na kuzikiliza roho yako.
Ifikie sehemu rafiki wa kweli baada ya Mungu wako basi iwe ni roho yako ukitambua maarifa mengi yaliyopo ndani ya roho yako basi utaweza kubadiri mengi katika maisha yako
Jina langu ninalotumia zaidi ni Rakims yaani Rakimz kwa wale ambao hamnifahamu vile vile kwa wale ambao ni wenye kuomba sana namba na mawasiliano yangu niwakumbushe tu ikiwa nimekupa au umechukua namba basi tumia sana mawasiliano ya ujumbe kupitia whatsApp ama voice note kwa maana ni bora zaidi kujibu kwa ufasaha kuliko kupiga simu wakati ambao sio sahihi kupiga simu. hivyo kuwepo na hekima ya mawasiliano hasa katika kupiga simu na vile vile ni vema zaidi kama mtu akitumia ujumbe mfupi kuliko kupiga simu
Kwa mawasiliano;
Email: Rakimsspiritual@gmail.com
WhatsApp: +255 783 930 601
Rakims
8 окт 2024