Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itafanya mapitio ya sheria na kanuni zinazohusiana adhabu dhidi ya makosa ya unyanyasaji wa kijinsia, lengo likiwa ni kukomesha vitendo hivyo nchini.
Majaliwa ameyasema hayo leo Aprili 18, 2024 wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Malapo.
Tunza amesema matukio ya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto, wanawake na makundi mengine yamekithiri.
13 окт 2024