Asante sana pastor, nilianza kula mara mbili kwa siku, asubuhi na mapema jioni. Uzito umepungua, uchungu magotini ukaisha, kiungulia kikaisha kabisa, nafurahi
Mama mzazi alikuwa na shida ya miguu kuuma sana kwa miaka mingi. Ikawa kutembea, kusimama na kukunja miguu ni shida. Pia kulala ilikuwa taabu. Akatembelea hospitali nyingi na kufanyiwa vipimo vingi ambavyo matokeo yalikuwa mengi na tofauti. Mwisho tukaamua kufunga na kufanya maombi pamoja na yeye (wore tulikuwa sehemu tofauti) kwa ratiba ya pamoja. Baada ya muda mfupi mama alipona mpaka sasa hivi. Yeye Ana umri wa zaidi ya 70yrs lakini hivi sasa Ana mazoea ya kufunga siku 3 kavu bila shida yoyote na anafanya mazoezi Kila siku. Mwili wake umerudi ujana kiasi kwamba watu waliomuona akiwa mgonjwa na sasa hivi hawamtambui.
Kiroho 1.Saidia kuwa mnyenyekevu, mpole, 2.kusikia sauti ya Mungu 3.inasaidia kutanguliza wengine 4.kuweza kujua nini cha kufanya kabla ya kufanya maamuzi fulani kama ndoa. Kiafya I. Ongeza hormone ya kukua. 2.inazuia uwezekano wa kupata type 2 diabetes. (kisugari) 3.inasaidia mwili kujikinga na tumors zinazoleta cancer. 4.inaongeza uwezo wa ufahamu na kupunguza obesity(uzito uliopitiliza) . 5.inasaidia mcharuko wa mwili. 6.inasaidia kupunguza pressure. 7.inaondoa seli zilizokufa.
pastor kwa hili leo nakubaliana na wewe! mimi ni binti nafanya kazi ya nyumba hapa warabuni qatar, miezi 2iliyopita nipata kazi kwenye nyumba moja hapa ambapo nafanya kazi, kwa hii nyumba mambo na mlo ni tofauti kabisa na nyumba zingine apo awali! mlo ni mara moja kwa siku, na mimi naona kama ni mbaya kwa sababu kwetu nyumbani ni mlotatu kwa siku,💪 mjungaji nakwambia juzi nikipima weights nimejipata nimepunguza uzito from 64kg to 54kg in 2months 😏😏 najisikia vibaya kwa vile mimi naona kama ni kukonda na konda, lakini vile nimesikia hii clip yako nitendelea na huu mfumo kwa ajili ya afya yangu asante.
Ubarikiwe sana pastor, maana mafundisho yako mawili kuhusu kufunga nimeyasikiliza kwa makini, na nimeanza kuyafanyia kazi. Nimefunga mara mbili kwa wiki tatu na matokeo ni kuwa, nilikuwa navimba miguu, sasa naona miguu nimeanza kusinyaa. Nitaendelea mpaka kieleweke. Bwana Mungu azidi kukubariki pamoja na uzao wako.
Pastor mbaga nikianzisha ratiba ya kupata mlo wangu asubuhi, halafu kwa Yale masaa ya mchana badala ya kupata lunch niwe natumia kunywa maji tuu mpaka mida ya dinner, vp ntakuwa nipo sahihi katika mfungo?
Nikweli kufunga kula na kunywa kunafaida kiafya,Mimi si mnene ila nilikua na kitumbo kama nanyemelewa na kitambi ivi ila sikuelewa ilikua ni nini,Nilianza kufunga lakini sio kwa jambo hilo ni kwa jambo tofauti, baada ya muda kama mwezi na nusu ivi icho kitumbo kikapungua sasa nikapata faida ya ziada kwa mfungo wa jambo tofauti,Nina mshukuru MUNGU kwa kuningoza kufunga.
Kufuga kwa kwel kuna faida!! Me binafsi sasa nmechukua muda wgu na fuga bt me hua nafunga ivi nikila kama sa tatu ucku ndo sili tena mpk sakumi na mbili jioni cku nyigine, na pia nmeona faida kwa mwili wgu. Ila naomba kuuliza kufunga mfungo huu ni saw au laah??