Yesu Kristo ni Mungu wakati amekaa katika kiti cha enzi,ni mwokozi wa ulimwengu alipokuwa katika mwili na akafa msalabani,anakuwa roho mtakatifu aliporudi akiwa katika roho,wote ni mungu moja,jinsi mwanadamu alivyo na mwili,roho na nafsi,flesh,soul and spirit.
Very nice! Ipo hivi, ili uwe mtu au binadamu lazma uwe na mwili na roho, na hii ni kutokana na sheria za Mungu mwenyewe, so kimoja kikikosekana maana yake sio binadamu tena. Ni hivyo hivyo kwa Mungu, yeye alie Mungu yu katika Baba na pia yu na Mwana ndani yake, maana ni Neno lake na maana lilikuwepoa na Baba toka mwanzo na Roho wake maana yu ndani ya Mungu mwenyewe. Hivyo huyo Neno alikuwa mwili ili aje awaokoe wanadamu ili arithi na wanadamu pamoja nae.
KWA NINI YESU [NENO] AITWE MWANA WA MUNGU ANGALI NA YEYE NI MUNGU. Bwana YESU asifiwe! Karibu tujifunze pamoja ujumbe huu ambao watu wengi wamechanganyikiwa hata wapo (BAADHI YA WATUMISHI) wamepoteza dira na mwelekeo kufikia kupotosha KANISA LA MUNGU kwa kusema YESU SI MUNGU WALA SI MWANA WA MUNGU. Na zamani walikiri hivyo, ila sasa wamepotea; hii inaonyesha hizi ni siku za mwisho. 1. KWANZA YESU NI NANI, NA KABLA HAJAITWA YESU ALIITWA NANI NA ALIKUWA WAPI? Kabla ya ULIMWENGU kuumbwa na hakukuwepo chochote MUNGU ndiye alikuwepo. Na Musa ndiye aliyepewa "UFUNUO NA MUNGU AU KUFUNULIWA NA MUNGU" kumjua Yeye, maana huwezi kumjua MUNGU mpaka amekufunulia yeye. "UFUNUO" wa Mungu una mipaka. Kile ambacho Mungu ufunua kwetu ni kweli, lakini hajafunua kila kitu. "Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 1Wakorintho 13:9. Kitabu cha MWANZO kimeandikwa na Musa. Na aliandika kupita UFUNUO kutoka kwa Mungu maana wakati Mungu anaumba mbingu na Nchi Musa hakuwepo. Kama Musa hakuwepo na katuandikia haya basi hapo tunakiri kwamba "MUNGU UFUNUA SIRI ZAKE KWA WATU WAKE" "Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake. Zaburi 25:14 Hivyo Basi waandishi wote walioandika BIBLIA waliandika wakiongozwa na Roho Mtakatifu. "Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. 2Petro 1:21 Kwahiyo MAANDIKO AU NENO LA MUNGU NI UNABII ULILETWA KWETU KUPITIA WATU ALIOWACHAGUA MUNGU NA KUWAONGOZA KUANDIKA AU KUSEMA KWA MSAADA WA ROHO MTAKATIFU. HAPO MWANZO KABLA YA KUWEPO KUWEPO CHOCHOTE. "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Yohana 1:1, 3. Huu ni "UFUNUO" wa Yohana mwanfunzi wa Yesu aliopewa na Roho Mtakatifu. Musa naye alipewa UFUNUO akaadika haya, "Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1 Kwa mantiki hiyo, unaposoma KITABU CHA MWANZO ujue unasoma "MAFUNUO YA MUNGU" ambayo aliyaachilia kwa Musa ili ayaanadike na watu tumjue Mungu. Sasa tunaanzia hapa. "MUNGU AKASEMA" "Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetuNa tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mwanzo 1:26 Hapo ujue Mungu ameshamaliza UUMBAJI, Sasa angalia anavyoachilia UFUNUO kwa Musa kumuonyesha kwamba hakuwa peke yake, bali alikuwa na ZAIDI YA WANAYE FANANA NAYE. twende Pole pole utaelewa. MUNGU AKASEMA, "Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu" Angalia hilo neno "KWA MFANO WETU NA SURA YETU" SWALI..... MUNGU ALIKUWA NA NANI AMBAYE ANATAKA WAMUUMBE MTU ANAYEFANANA NA WAO? Ebu na wewe jiulize, Si mimi nimesema huo ni "UFUNUO WA MUNGU KWA MUSA" na Musa akaandika ili sisi tujue. MUNGU ALIKUWA NA NANI? Mwingine anaweza kusema alikiwa na malaika, Je, Mungu anafanana na malaika aliowaumba? Jibu ni HAPANA. "Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto. Waebrania 1:7. Referring to the angels He says, [God] Who makes His angels winds and His ministering servants flames of fire; [Ps.104:4.] Hebrews 1:7. JE HAO WANAOFANANA NA MUNGU NI NANI MPAKA WANAPANGA KUSHUKA? "Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. Mwanzo 11:7 Hii ni habari ya kuhusu watu walipoamua kukaa sehemu moja bila kutawanyika na kuamua kujenga mnara wa Babeli ndipo kikao kikakalika tena mbingu. Wakasema "NA TUSHUKE TUKAWACHAFULIE USEMI" kama alikuwa mmoja kwanini asiseme "NISHUKE NIKWACHAFULIE LUGHA" Musa bado anapewa UFUNUO WA KUMJUA MUNGU. Kwahiyo tuelewe kwamba Mungu hakuwa peke yake. Tunataka tuwajue hao alikuwa nao ni nani na nani? Si ndo maana yake. (Maaana ukipinga bila neno ujue wewe ni mpotoshaji, na unatumiwa na adui maana Neno la Mungu liko wazi kabisa linajitosheleza) Sasa twendelee!! BAADA YA DHAMBI KUINGIA ULIMWENGUNI. Mungu alikuwa anatafuta suluhisho la kumuokoa mwanadamu kwa kumuondoa katika MAUTI iliyoingia kwake kuputia ADAMU NA HAWA. "Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; Warumi 5:12. NINI KILITUMIKA KUONDOA DHAMBI? Walitumia damu za wanyama, lakini damu hizo HAZIKUFUTA WALA KUONDOA DHAMBI zilipotolewa bado dhambi zilionekana kwa Mungu.. "Kisha kuhani atatwaa katika damu ya hiyo sadaka ya dhambi kwa kidole chake, na kuitia katika pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, nayo damu yake ataimwaga hapo chini ya madhabahu ya kuteketeza. Walawi 4:25. "Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili; Waebrania 9:13 "Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka. Waebrania 10:3. KAMA KULIKUWA NA KUMBUKUMBU YA DHAMBI BASI DAMU HIYO HIKUFAA, MUNGU AKATUFUTA NJIA MPYA. Je katika njia hiyo Mpya ya kutaka kumkomboa MWANDAMU Mungu alipanga nini? ALIPANGA KUJA YEYE MWENYEWE. Sasa yeye mwenyewe anakujaje KUMKOMBOA MWANADAMU? Nijurudishe tulipotoka, "TUMFANYE MTU KWA SURA YETU" Hao ambao walizungumza katika kikao hicho ambao WANAFANANA. (Kumbuka jambo hili "MUNGU HAFANANI NA KITU CHOCHOTE" Kwahiyo Aliposema kwa mfano wetu, KAMA ANA NURU, basi na alionao pia wana NURU, kama ni "ROHO" basi na alionao ni "ROHO" kumbuka huu ni "UFUNUO" Musa aliuandika kutokankwa Mungu. Hivyo kumbuka katika AGANO LA KALE MUNGU HAKUJIFUNUA ZAIDI, KAJA KATIKA AGANO JIPYA. Sasa MUNGU anakujaje duniani kumkomboa Mwanadamu? Mungu anaanza kuachilia UNABII "UFUNUO" kwa watu wake anasema, ANAMPA UFUNUO YEREMIA. "Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili; Waebrania 9:13 Agano hili linahusu "DAMU" ambayo siyo ya wanyama, wala siyo kama yule aipelekaye patakatifu pa patakatifu alivyo mwenye dhambi. Hii "DAMU" inatakiwa isiyo na UCHAFU WOWOTE. na anaye ipeleka asiwe mchafu pia. Sasa wale WANAOFANANA WALIO PAMOJA anatoka mmoja wapo ili aje ULIMWENGUNI. Kikao kikaklika ili sasa kutafuta "MWILI" aingie humo ili awe MWANADAMU aje kukabiliana na dhambi kupitia MWILI WAKE. Wakamuona MARIAMU ambaye hajawahi kukutana na mwanaume yeyote. Hapo ndipo mpango unaanza wa kuja kwa "HUYO ALIYEKUWA NA MUNGU KABLA YA ULIMWENGU KUWEPO AMBAYE ANA ASILI MOJA NA MUNGU" Unapozungmza ASILI maana yake chanzo chake ni kimoja, alikuwepo, yupo na atakuwepo. MFANO. Mwanadamu (mtu) ili akamilike lazima awe na ROHO, NAFSI NA MWILI. vinapoungana hivi vitatu ndipo anapatikana MTU. Kwahiyo kama alivyo MTU ni mmoja ana ROHO,NAFSI, NA MWILI ndivyo na MUNGU alivyo. TANGAZO LINATOLEWA. "Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Luka 1:30-31 TUKUMBUKE UFUNUO WA NABII ISAYA ALIOPEWA NA MUNGU KUUSEMA KUHUSU MTOTO ANAYEZALIWA. "Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Isaya 9:6. SASA TUANGALIE SIFA ZA HUYU MTOTO. 1.UWEZA WA KIFALME UTAKUWA MABEGANI MWAKE. 2.MSHAURI WA AJABU. 3.MUNGU MWENYE NGUVU. 4.BABA WA MILELE. Sasa Nabii isaya ANAFUNULIWA juu ya huyu mtoto jinsi alivyo. Ukiona sifa zote hizote ni sifa za MUNGU. Hapo ndipo tunarudi kule tuloktoka "KWA MFANO WETU NA SURA YETU" Kwahiyo huyo mtoto ana ASILI ya MFALME, MSHAURI, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE. Na asili hizo ndizo anazo Mungu. MUNGU huyu ana majina mengi na amejifunua kwa watu na kujitambulisha kwa majina yake. (Ukiyataka nionbe inbox nakutumia) YESU alipozaliwa na kupewa jina hilo "YESU" lenye maana yab"YEHOVA ANAOKOA" alikuwa anaitwa "NENO" NENO ANAVAA MWILI WA MWANADAMU. "Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli. Yohana 1:14 Kwahiyo jina la YESU ni jina la MUNGU maana ndiye anaitwa JEHOVA. "amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao. Waebrania 1:4 Angalia hilo neno "JINA ALILOLIRITHI" Kwa mantaki hiye NENO aliyekuwepo tangu mwanzo anapewa jina la YESU maana yake JEHOVA ANAOKOA. KWA NINI ANAITWA MWANA WA MUNGU Kwa sababu "Amezaliwa" alijushusha kama hana UTUKUFU WOWOTE akakubari kuwa kama mwanadamu, lakini wakati huo yeye ni NENO aliyekuwako pamoja na Mungu mwenye U-UNGU mmoja na Mungu. WALIOISHI NA YESU NA KUMSIKIA NA KUTEMBEA NAYE (WANAFUNZI) YESU ALIKUWA AKIJIFUNUA POLEPOLE. Yesu hakutaka kuwaambia kwa uwazi kwamba yeye ni "MUNGU" ambaye ni ASILI moja na MUNGU aliyejifunua kwa MUSA, ELIYA, ELISHA, IBRAHIMU, DANIELI, EZEKIELI, NK. Yesu alipokuwa akiwaambia MUNGU ni "BABA YANGU" maana yake alikuwa amejinyenyekeza sana kama mwanadamu kuonyesha utiifu. Mtume Paulo alipewa "UFUNUO" na kuandika. "ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; Wafilipi 2:6. Maana ya hili neno "naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho" Maana yake, KWA NAMNA YA ALIVYOKUWA KAMA MWANADAMU, NA AKAISHI DUNIANI NA KUUVAA MWILI HAKUTAKA KUNG'ANG'ANIA ASILI YAKE YA UUNGU KUWA NAYO DUNIANI ILI KUFANANA NA MUNGU ALIVYO HUKO MBINGUNI NA YEYE AWE HIVYO DUNIANI" NITAENDELE.. Endelea kufuatalia mpaka mwisho. Ubarkiwe.
I really agree with pastor ndacha. When you read bible in the book of John, the bible says that in the beginning was the word, (jesus), and the word was with God, and the word was God.
Mtumishi hakika wewe umenikuna moyo wangu mno maana unaipiga roho ya mpinga kristo kwa neno ,Asie mjua Yesu kristo yupo chini ya rana, Jina lake Mungu ni Yesu kristo,
Tangu Yesu alisema mimi niko alikuwa amejitambulisha yeye ni MUNGU Rudi kwa Musa alipomuuliza MUNGU wakiniuliza huyo aliyekutuma ututoe misri ni nani? MUNGU akasema waambie mimi NIKO ambaye NIKO amenituma na alipowaambia hivo hawakubisha Na sasa Yesu mwenyewe anasema kabla ya Ibrahimu mimi NIKO Hapo mwenye akili na ajue
This Tv Channel I recommend it 100%.. It's take high quality Videos.. and very Clean Voice.... Naomba muwe mna Tuma mada live... Congratulations 👏👏👏👏👏👏
Uko sawa mtumishi ata mmi nimefunguka leo kama Yesu ni mwana wa Mungu yye ataitwa Nani na uyu mwana akuagi hadi leo na kwann hilo jina limanguvu linaweza kubadilisha kila kitu....kwa maan hiyo YESU ni MUNGU
Tena kama hukumu kubwa.mwanadamu.atahukumiwa.kukataa kuwa yesu sio.Mungu nabii isaya anasema jina.lake.imanueli Mungu pamoja.na wanadamu yesu kwa wanadamu ni Mungu .tusimkosee Mungu wanadamu tusome sana vitabu
Wewe mwalimu kama sio roho wa mungu amekujiabia hao waslamu ni wanafiki sana lakini ashukuriwe mungu amekupa hekima ya kuwakomesha yesu ni mungu real si wakubahatishsa mhukumu wa ulimwengu
Mungu ni mmoja hana nafsi tatu ana nafsi moja kwa kuwa ni mmoja tu. Mitume wote waliamini na kufundisha kuwa Mungu ni Baba wa Yesu Kristo. Mathayo 16:13-17 Yesu alimwambia Petro kuwa nini lake ulikuwa ufunuo wa Mungu kwake! Yohana alipoandika 1:1-1 Hapo mwanzo, ni mwanzo upi? Marko 1:1 Marko anaandika pia Mwanzo, Mwanzo upi ni mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo! Wasiofahamu maandiko hufikiri ni mwanzo wa uumbaji lakini ni Mwanzo wa Injili. Yesu alipofufuka alimwambia Mariamu Magdalena aende awaambie wanafunzi wake kuwa anakwenda kwa Mungu ambaye ni Mungu wao na anakwenda kwa Baba ambaye ni Baba yao. Yohana 20:15-17 Yohana anaanza kwa kuandika hapo mwanzo 1:1 Hatimaye anahitimisha kazi yake ya uandishi akimtaja Yesu kuwa ndiye Kristo Mwana wa Mungu na ukiamini utapata uzima kwa Jina lake 20:30-31 Kama hauamini kuwa Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu hauna uzima!
Yesu siyo Mungu , kwa kuwa kuzaliwa kwake kulitabiriwa hivi: Malaika Gabrieli alitumwa na Mungu. Malaika alimwambia Mariamu kuwa Atalanta mimba kwa uweza wa Mungu, na Jina la mtoto atamwita Yesu , naye atakuwa ni Mwana wa aliye juu! Luka 1:26-27,30-32 Kama Yesu ni Mungu ni dhahiri kuwa huyo Yesu wenu ambaye ni Mungu hakuzaliwa na Mariamu ! Kama Yesu ni Mungu basi malaika Gabrieli ni mwongo na alimdanganya Mariamu?
JAMANI NAOMBA NIWAHABARISHE kidogo kuwa NDACHA ALIMALIZA DARASALA SABA TU WAKTI SULE NI PHD HOLDER .Kwahiyo NDACHA ANAONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU wakati DR.Sule anaongozwa na akili zake tu.Mubarikiwe kwa kunielewa
Msimamo wa ndacha ni kuwa yesu ni Mungu kwa asili yake kwakuwa mwana wa mwanadam ni mwanadam na mwana wa Mungu ni Mungu kwa asili , kwahiyo yesu kristo ni mwana wa Mungu
Siku zote nasemaga utofauti wa mkristo na muislam ni huu hapa, WAKRISTO WAMEPEWA MAMLAKA NA MUNGU YA KUMTIMUA SHETANI, lakini WAISLAM MAMLAKA HII HAWANA
Bibilia inasema mungu nimmoja na pale yesu anasema mungu wangu mungu wangu mbona umeniacha wamekua mungu wanganui mbona ua changanya wakiristo yesu yeye amesema katika bibila ametumwa je kama yeye ni mungu ametumwa na nani? Na maandiko yanayo sema yesyu ni mungu ni watu wamesema, yesu hajakubali hata andiko moja kua yeye ni mungu
Ndiyo maana sisi wasomi na watafiti wa Maandiko Tunasema Yesu ni Mungu %100 ni Mwanadamu,,Sababu za kuwa Mungu ni Katika Roho ni baba wa Milele, na Katika mwili ni mwanadamu,Ndo Kule kuchukuliana na sisi Ebrania415
Mzee wa upako kakurupuka kusema yesu sio Mungu...sjui anasoma biblia gan yn...hajui kama mwana wa Mbuz ni mbuz? Hvyo mwana wa Mungu ni Mungu....Yesu anaitw Mungu mwenye nguvu ..soma Isaya 9.6