Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Constantine Kanyasu ameyaweka bayana Makampuni yanayotoa huduma kwa Watalii yanayoshutumiwa kufanya vitendo vya kuwatapeli wageni kwa kuchukua fedha zao na kushindwa kuwahudumia kwa mujibu wa makubaliano,
Kanyasu amebainisha jambo hilo Jijini Arusha wakati wa Kikao baina yake na wadau wa Sekta ya Utalii ambapo ameongeza kwamba Wizara ya Maliasili inaadaa mpango wa kuorodhesha kwenye mtandao (website) Kampuni za Utalii zilizosajiliwa Nchini ili kuondokana na vitendo vya kuwatapeli wageni na kuiletea Nchi sifa mbaya.
14 авг 2019