🔘JE, NA WEWE UNA HABARI? 🔘WASILIANA NA MwanaHALISI TV (+255 767 400402), 🔘WhatsApp (+255 692 318213) 🔘Email: mwanahalisitvnews@gmail.com 🔘KWA HABARI ZA KILA SIKU: mwanahalisionli...
Sema sanaaaa Kijana Mzalendo ni kweli usemayo Familia ya Mwalimu Nyerere haiko vizuri njaa tupu hawajaliwi hata tunaona nyumba zake haziko vizuri hazitengenezwe zimechakaa tunaziona kwenye mtandao
Unahaki ya kuitwa kijana Mzalendo umesema kweli kabisa nakuunga mkono kwa asilimia zote Mungu akulinde na kukupigania Mzalendo natamani kama viongozi wangeyafanyia kazi ayo maneno.
Maombi na kuomba Toba kwa ajili Tz Ili nchi ipone tulipomkosea mungu tunafanya yasiyompendeza kila mtu kwa imani yake kuhusu Nyerere hata ukiamshwa usingizini anakumbukwa kuunganisha makabila ndo Amani hiii Nyerere hoyeeee
Mwalimu Nyerere amepigania dunia(South-South Commission),Africa(mwanzilishi wa Umoja wa Africa),Tanzania(Tanganyika na Zanzibar) na Tanganyika.Sera za ujamaa na kujitegemea.Azimio la Arusha na vijiji vya ujamaa.
Kama naanza kukuelewa vile! Kwamba siku hiyo ya tarehe 14 ilitakiwa kuwa maalum kwa kuonyesha vitu/kazi, sanaa nk alivyovifanya na hata kuvisimamia Mwl Nyerere kote nchini na siyo suala la kupokea Mwenge ambao kwa hali halisi zoezi lilitekwa. Mavazi na kila kitu kilitakiwa viwe na sura ya Nyerere na siyo Samia!! Nafananisha siku ya Pasaka ambapo dunia nzima hukumbuka ushujaa wa Kristo Yesu, namna alivyoteswa, kudhalilika, kutemewa mate, kuuawa, kufa kuzikwa na hatimaye kufufuka siku ya tatu!! Hakuna katika siku hiyo ambayo mambo ya kawaida ya kidini makanisani kote duniani huonyeshwa tofauti na kumbukizi hiyo!! Tujifunze tulipokosea
Isisahaulike kuwa GM,akiwa mzungumzishaji wa bunge la afrika,wkt anastaafu,alikchukuwa na samani za taasisi Hadi kidiplomasia akatakiwa kizirejesha! Uadilifu wake ☆
Kwanza hakuna kiongozi yeyote na hata wanachama wa CCM wanao muenzi Mwalimu Nyerere, wanacho Fanya NI unafiki tupu. Nyerere alikuwa mwadilifu, mtii, mpendwa HAKI, mcha Mungu. Hawa tulip nao NI MAJIZI,Wazalendo feki Mabepari uchwara. Wauzia NCHI na Manyang'au.
Ni kweli kabisa usemayo kama Kabudi ni mzuri sana tokea tuko naye kwenye gazeti la Uhuru wakiwa Vija wadogo na wenzao Salvatory Rweyemamu Saidi Nguba Bardiwin Mziray Sengondo Mvungi Kwey Ruseme Agrey Mlimuka na wengineo ambao nimewasahau kwa ajili ya umri wangu
Ni ukweli ulio wazi, akina mama lishe na mahali pengine wanadanganywa na kamtungi ka kilo 25 eti tumewaondoa kwenye matumizi ya mkaa kuondokana na magonjwa. Mmmmmh, mtungi wa kilo 25 baada ya kuisha ?
@@ray9738 Mambo yanayofanyika Botswana ya kumuenzi Mwalimu.1.Matumizi mazuri ya mapato ya kodi kwa kuwalipa watumishi wa umma mishahara ya kadri,bila kuwabagua wabunge na watumishi wa serkali.Hapa kwetu kabla Mwalimu hajang'atuka mishahara ya wabunge na gratuity zao zilikuwa za kadri tu.Sasa,gratuity ni karibia ya Tshs.300millioni kwa miaka 5.Magari ya serkali ni machache sana.Kila mtumishi wa umma hata mawaziri wanaenda kazini na magari yao,kama unavyoona India na Uingereza. Hapa magari ya watumishi wa umma yana bajeti ya serkali kubwa.2.Masomo yanalipiwa yote bila mikopo.3.Vijana ajira ni hivi ukitoka shule unapangiwa mahali pa kufanya kazi.Kama ni kilimo lipo trekita na huduma zote za serkali bila malipo mpaka uvune.Haya ndiyo tulikuwa nayo wakati wa Mwalimu.Yapo,mengine.Tuwasiliane kama unayahitaji au pendant ubalozi wa Botswana Nairobi Kenya utayaelezewa.Mimi nilikuwa SADC Gaborone na hizi zilikuwa nchi zangu za ufuatiliaji wa sera zao maendeleo hasa za usimamizi wa mztumizi ya raslimali za maji.
Lakinii Nyerere alienda vikaoni na maamuzi, haswa pale yalipolengwa maazimio. Maazimio karibu yote yalikuwa fikira za Mwalimu. Sijui alifikiri yeye tu ndiye ajuaye. Alikuwa mkiritimba.
Kwa sababu kabla ya vikao alikuwa anakutana na wazee na vijana wenzie aliowaamini na kushauriana kuhusu mambo muhimu ya nchi… wakishakubaliana ndipo Nyerere akiwa kiongozi alikuwa anatoa maamuzi yaliyokubaliwa na washauri wenzie mbele ya UMMA.