Kutana na Eva John (24) kutoka Kiwangwa Bagamoyo, mkoa wa Pwani ambaye changamoto za kutokuendelea na shule baada ya kumaliza kidato cha 4 hazikumfanya kukata tamaa. Hapo ndipo alipoamua kuanza kufanya kilimo katika shamba lake la ekari 1 mwaka 2018 akiwa na ujuzi mdogo wa uzalishaji na upatikanaji wa masoko kusababisha mazao kuharibika shambani.
Kwa sasa ana shamba la takribani ekari 6 la mananasi ambapo amejiunga na huduma za TAHA mwanzoni mwa mwaka 2020 na kupitia TAHA Eva amekuwa akipokea ushauri wa kitaalam juu ya mbinu bora za kilimo, upatikanaji wa masoko na usindikaji ili kuongeza thamani ya mazao anayolima, kisha kudhibiti upotevu wa mazao.
Eva anauza mazao yake kwenye masoko ya Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro na alikuwa akiuza Kenya kabla ya kuzuka kwa Covid - 19. Hivi sasa anatarajia kuvuna ekari 5 za mananasi na anatarajia faida ya zaidi zaidi ya tshs mil 10.
Kupitia kilimo cha horticulture ameweza kuipatia familia yake mahitaji ya msingi, kujenga nyumba yake na pia kuwajengea wazazi wake, pia amejenga fremu za maduka ya kukodisha na anasaidia wanafunzi 13 kwenye eneo analoishi na mahitaji ya shule ili waweze kutimiza ndoto zao na wasiishie njiani kama yeye.
#TAHA
#HorticultureForHealthAndWealth
16 сен 2024