Madeleka Mwenyenzi Mungu akupe maisha marefu na yenye Baraka uendelee kuwasaidia watanzania. Ninapinga mbinu zote ovu zinazopangwa kumdhuru mtu huyu. Wenye kutengeneza mbinu hizi namwomba Mungu apite nao, wasiendelee kuishi!!!
Kwa kweli sasa tunaona juhudi za chama cha mawakili wasomi TLS,tunafarijika sana tunapofuatilia mabaraza yenu haya katika midahalo ya kukosoana wenyewe,na kuifunua mfumo wa utawala unaopindisha sheria kwa kukanyaga katiba katika maamuzi yao ya kudhulumu wananchi kwa faida yao binafsi.
Wakili msomi Madeleka usikate tamaa wakati mapambazuko yamekaribia pambania haki Mungu hataacha kukulipa juhudi zako,na atakulinda popote kwa mkono wake wenye nguvu kuliko hawa wanaovuta pumzi yake ya bure kutumia nguvu kuwaumiza wengi wala hawajui ni lini BWANA atatwaa uhai wao na kuacha vyote wanavyojikusanyia!
Watanzania kwa ujumla wao kwenye sanduku la kura mwakani ndio watakao ondoa mfumo huu mbovu wa katiba ya 1977 Mungu yupo pamoja na wapenda haki, watanzania lazima watafanikiwa kupata haki zao.
Kweli hiyo Mahakama ipo nimeshawahi kwenda kumlipia mtu faini ya uzembe na uzururaji .Kitu ambacho alikutwa barabarani akienda Bilcanas usiku saa nne .Dar kuna mambo ambayo huwezi kuamini yanafanywa kwa uonevu tu .
Tatizo ni ulevi tu , ukiwa madarakani unajizima data kwamba hautakuwa madarakani milele, lakini pia siyo ukoo wenu nyoote mpo madarakani Mnachokipanda mtavuna tu hata kupitia wajukuu zenu , WATAUMIZWA NA WAKANDAMIZAJI WENZENU NA MTAPIGA KELELE
Hongereni sana Mawakili na mawakala wa sheria, Kwa sisi wapenda haki na mifumo tunafurahia sana mijadala hii. Tunamuunga mkono Wakili Mwabuksi, Haki haiombwi, haki inapiganiwa🫡
Hata nyie mawakili mnayomatatizo.mbona maamuzi ya kesi yanatolewa kwa lugha ya kizungu? Hamuwatendei haki watanzania.hamtaki kuandika sheria kwa Kiswahili, Kweli mnaruhusu mahakama iwahukumu watanzania kwa lugha wasioielewa,mna jambo lenu ninyi mawakili ambayo sitaji. Hamjali watanzania dhambi inawarudia.Hivyo tesekeni mpaka mwisho.
Tatizo la Shangazi huwa anapenda sana kuogea kizungu, sasa si watu wote wanaojua kizungu. Hebu naomba uwasaidie watu hawa manake ni wengi wanaofuatilia midahalo kama hii.