Baada ya Elisha kukutana na mwanamke mshunami na kukaa kwake, akampa Neno kutoka kwa Bwana kuwa mwakani majira kama yale atapakata mwana, ndivyo ilivyokuwa.Baada ya miaka kadha yule mtoto aliumwa kichwa na akafa.Yule mwanamke alimfuata Elisha moja kwa moja baada ya kifo cha mwanae. Ndio maana ni muhimu sana kutunza mahusiano yako na Mungu hata baada ya Yeye kukupa unachokihitaji, kupewa unachohitaji kusikutoe kwake bali ndio kuzidi kukuweka karibu naye.
Hapa baada ya Elisha kwenda na kumfufua yule mtoto alikuwa ameishinda mauti.
Kuna jambo moja kuhusu roho ya mauti,unapoishinda itatafuta tu namna ya kurudi na kulipa..ndio maana ukiishinda isikufanye ukatulia bali uzidi kujiimarisha zaidi kwa Mungu. Ukisoma mistari michache mbele utaona kuwa ile mauti haikumuacha bali walipopika chakula ilikuwemo sufuriani tayari kwa ajili ya kuwamaliza wote.
Elisha akatoa maelekezo kuwa uletwe unga na akaurusha kwenye sufuria na ile mauti ikaondoka kabisa. Ukivuka hatua moja usimuache Mungu maana ni Yeye atakayekuvusha na hatua inayofuata.
#PastorSunbella#Roho#YaMauti
11 апр 2022