Rais Samia Suluhu Hassan amewaagiza wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa iliyopo mipakani kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa mazao unaofanywa na wafanyabiashara kwenda kuuzwa nje ya nchi pasipo kibali cha Serikali.
Agizo hilo la Rais Samia limetolewa mkoani Rukwa wakati akizindua maghala ya kuhifadhia mazao ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) yaliyojengwa eneo la Kanondo mjini Sumbawanga.
✍@official_jennifersumi
#azamnewsupdates
29 авг 2024