MKUU WA MKOA WA DODOMA ANTHONY MTAKA AWATAKA WATUMISHI CHEMBA KUJITAFAKARI NA KUACHA MALUMBANO.
Na.Faustine Gimu Galafoni,Chemba Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amewataka watumishi wa halmashauri ya Chemba kujitafakari katika utumishi wao kutokana na halmashuri hiyo kurudi nyuma kimaendeleo kwa kudorora ukusanyaji wa mapato,kiwango cha chini ufaulu na miradi mbalimbali kutotekelezwa kwa wakati, chanzo kikitajwa kuwa ni malumbano na mivutano isiyo na tija kwa watumishi wa halmashauri hiyo.
Mkuu wa Mkoa huyo amebainisha hayo Wilayani Chemba Mkoani Dodoma baada ya kufanya mkutano na Watumishi wa halmashauri hiyo ngazi ya vijiji hadi wilaya lengo ni kusikiliza kero pamoja na changamoto mbalimbali zinazosababisha halmashuri hiyo kusuasua katika nyanja mbalimbali zikiwemo nyanja za elimu,Kilimo ,na miradi mbalimbali ya maendeleo kukwama kutokana na malumbano kwa viongozi kama wanavyoeleza.
USISAHAU KU SUBSCRIBE CHANNEL YETU ILI UWE UNAPATA UPDATE MPYA KILA TUNAPO WEKA HABARI MPYA WAKATI WOWOTE
BONYEZA HAPA CHINI KWENYE MAANDISHI YA BLUU
www.youtube.co....
/ kahamatvonline
#KAHAMATVONLINE #HABARIZAHIVIPUNDE
14 окт 2024