John Martine ni kijana wa miaka 30, mkazi wa kijiji cha Managa Wilaya ya Babati. John ni moja ya vijana waliopata mafanikio katika sekta ya Horticulture kupitia zao la nyanya baada ya kujiunga na kupata elimu kutoka TAHA. Mafanikio hayo ni pamoja na elimu juu ya zao hili na kilimo kwa ujumla, kuweza kujenga nyumba, kumiliki vyombo vya usafiri na kukidhi mahitaji ya familia yake.
27 фев 2022