Тёмный
No video :(

Salama Na DITTO SE6 EP55 | TUNER PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460 

YahStoneTown
Подписаться 396 тыс.
Просмотров 13 тыс.
50% 1

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Lameck Ditto Sr ni Baba, Mwalimu, mwanamuziki, muandishi, mentor, mume na zaidi ya yote ni mwana tu ambaye maisha alopitoa kipindi anakua hayajawahi na wala hayatawahi kumsahaulisha yeye ni nani na wapi ambapo ametokea na wapi anataka sana kuelekea maana huko ndo kwenye kesho yake, na kwa kumsikiliza ambavyo nimemsikiliza, kesho yake anaithamini sana na amekua akiiandaa vizuri ili hata siku moja asije akakwama na kuanza kuishi maisha ya jana ambayo yalikua si mazuri hata kidogo.
Yeye na Baba yake mzazi walikutana kwa ‘bahati mbaya’ tunaweza tukasema hivyo maana wakati yuko zake Morogoro akiendelea na maisha ya kuishi yeye na Kulwa huku wakijilea wenyewe, Ditto au Dotto ananihadithia vile ambavyo Rafiki yake aliweza kumkutanisha na Mzee wake bila ya yeye kutegemea.
Alikua ananiambia vile ambayo ilikua inabidi apambane kupata ya kula na pa kulala baada ya kuja jijini Dar es Salaam na haya yote ni baada ya yeye tayari kuwa umeshatoka na WATU PORI enzi hizo na hapo pia ni baada ya kupata nafasi ya kurekodi album moja na producer PFunk enzi hizo, PFunk huyo huyo ambaye alikua akilitikisa TAIFA kwa kazi nzuuri alizokua akifanya na wasanii kadha wa kadha ikiwa pamoja na Juma Nature.
Lameck anakumbuka jinsi alivyokua analala ndani ya kiduka kidogo cha mwanawe mmoja ambaye alishamsomesha ili amstiri ki hivyo, alivyokuja Dar alikua anakaa kwa mwanae mmoja ivi na mkewe ila baada ya ahadi za album kutoka na kwamba mambo yatabadilika kugonga mwamba, Lameck ilibidi atafute ustaraabu mwengine.
Nilitaka kujua kama hiyo ndo ilikua lowest moment ya maisha yake? Au kifo cha Mama yake? Au Mamu kukataa album yake kwa kusema haikua na kiwango kile?
Sasa ni Baba na mchumba wa muda mrefu wa Binti mmoja ambaye nae alikutana nae ki ajabu ajabu tu na ambaye pia alimzungusha sana kabla hajanasa kwenye ndoana. Baba wa mtoto ambaye Mimi baada ya kukufanya nae mazungumzo nilikutana nae uwanjani akiwa ameenda kumuangalia Lameck Jr akifanya yake kwenye moja ya mechi za soka za shule ambayo anasoma. Kwenye meza aliniambia moja ya ahadi ambazo amejiwekea ni kuhakikisha yuko pale kwaajili ya mtoto wake, jambo ambalo yeye hakuwahi kulipata mapema.
Mwanzo nilikuambia yeye pia ni muandishi, muandishi wa mashairi ya muziki na pia ni muandishi wa matangazo, kazi ambayo anasema Marehemu Ruge Mutahaba ndiye ambaye kwa kiasi kikubwa alimuelekezea huko. Na mentor wake mwengine ni Ndugu Ruben Ncha Kalih ambaye kwa asilimia KUBWA amempika na akapikika.
Tulizungumzia pia umuhimu wa mmoja kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kupata pesa, kuweza kukabiliana na MSIMU ambao unakua huna wimbo (au kazi) lakini bado ukaweza kuishi, kuhusu maamuzi ya yeye kwenda THT wakati tayari alikua ARTIST ambaye ameshajijenga. Tuliongea pia kuhusu Ruge, Barnaba, Amini na mambo mengine tele. Binafsi nilikua na wakati mzuri sana wakati tunaongea haya na yangu matumaini itakua hivyo kwako pia.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
‪RU-vid Link bit.ly/RU-vidS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Опубликовано:

 

5 сен 2024

Поделиться:

Ссылка:

Скачать:

Готовим ссылку...

Добавить в:

Мой плейлист
Посмотреть позже
Комментарии : 25   
@johansenbashange2628
@johansenbashange2628 Год назад
Leo ndio nimejua kumbe ni Ditto alipiga zile sound kwenye Dar stand up!
@nawwalpascal5627
@nawwalpascal5627 Год назад
Huyu ndo msanii wng nmb 1
@Zuulito
@Zuulito Год назад
Nampenda sana jamani
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
Salama na Joel nanauka please please please
@simonballu1124
@simonballu1124 Год назад
salama ndo mtu pekee video zake hazinaga ads safi kabisa salama.
@Joliegal834
@Joliegal834 Год назад
Mmh😂 sip kwel
@Joliegal834
@Joliegal834 Год назад
Imenikuta
@donnietommie8444
@donnietommie8444 Год назад
#SalamaNaDrLeaky #SalamaNaDrLeaky
@rizikiones5687
@rizikiones5687 Год назад
Msanii sana
@mmn7480
@mmn7480 Год назад
jamni napenda salama akicheka
@maicgado58
@maicgado58 Год назад
Dito mtu mbadi
@kalibarikiedson5885
@kalibarikiedson5885 Год назад
Niliisubiri sana kwa hamu hii
@mchinjanyau9055
@mchinjanyau9055 Год назад
Salama Na #MASANJA MKANDAMIZAJI
@abdulrajabu8252
@abdulrajabu8252 Год назад
mtafute nuru the light itakua bonge moja la interview 🔧
@nahyialetomia9284
@nahyialetomia9284 Год назад
Mtu handsome
@heppypankras4578
@heppypankras4578 Год назад
Here we go
@broza_Tv353
@broza_Tv353 Год назад
🤣 eti nikiskiliza mwenyewe nazima
@godfreymiho4927
@godfreymiho4927 Год назад
🤗🤗
@gataramaabdul9761
@gataramaabdul9761 Год назад
1
@faudhiasalum7279
@faudhiasalum7279 Год назад
Salama na juma lokole please please please
@ashaidd2912
@ashaidd2912 Год назад
Joel nanauka mlete jaman
@lilianmnyanyi1854
@lilianmnyanyi1854 Год назад
Amina
@alexkissinga.5883
@alexkissinga.5883 Год назад
Aya athumani tajiri inapanda lin???😢
@tanzaniamycountry9308
@tanzaniamycountry9308 Год назад
Athumaniiiiiiiiiiiiiiii Maneno kidogo pesa ming
Далее
MPOKI NA WAZAZI WAKE
10:59
Просмотров 13 тыс.
Linkin Park: FROM ZERO (Livestream)
1:21:01
Просмотров 4,5 млн
INTERVIEW SHOW  BABA LEVO  at COCONUT fm ..ZMOTION
7:05
Salama Na Lord Eyes Ep 20 | HAWATUWEZI Part 1
32:10
Просмотров 96 тыс.
Linkin Park: FROM ZERO (Livestream)
1:21:01
Просмотров 4,5 млн