#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
MASTER
Kwa wengi wenu hii sura ni ngeni kabisa, ila pengine jina pale la zamani na kama wewe ni mtu wa zamani linaweza lika kukumbusha kitu, ila kama hukuwepo enzi hizi za Samia X basi ugeni wake pengine uwe ndo chachu ya wewe kutaka kumfahamu vizuri, na nikuambie tu kwamba hutajuta hata sekunde moja kumskiliza yeye.
Jina ni Henry Kulaya aka Coach Carter kama ambavyo Mjukuu wa Malkia wa Uingereza Prince Harry humuita, ni Mtanzania mwenzetu na asili yake na wazazi wake ni Moshi, yes ni Mchaga ambaye baada ya kumaliza masomo yake Mama yake alimpa nafasi ya kwenda kusoma nchini Uingereza, mambo gani alisomea utayaskia mwenyewe akiyaelezea na jinsi ambayo alibadili winga na kuingia kwenye masuala ya Elimu pia utamskia mwenyewe akielezea safari yake hiyo, ila mimi nataka nikuambie vile nilikutana naye na jinsi ambayo napeeenda na na enjoy sana kumskiliza.
Safari yake ya career yake aliyoichagua au niseme aliyo chaguliwa maana kwake si kitu aliwahi kufikiria, kuwa MWALIMU? Kabisa? Ila ng’amua hili… Ilikua ni moja ya maamuzi bora zaidi ambayo amewahi kuyafanya kwenye maisha maisha, safari haikua ya lele Mama au rahisi, kumbuka alikua nchi ya watu, mweusi na si mzaliwa wa pale, Henry anakumbuka vizuri vikwazo ambavyo alipitia na utamu wa mafanikio yake haswa pale alipokua akiwekwa kwenye list ambayo yeye pekee ndo alikua sio mzawa na umri wake pia ulikua mdogo.
Baba na mume Henry anatuhadithia jinsi ambayo alitafutwa na watu wa Prince Harry na kutaka kwenda kutembelea shule yake ambayo yeye ndo alikua Principal, humu anatupa hadithi hii kwa kina (na Prince hakuenda kumtembelea mara moja kwa taarifa yako) na jinsi ambayo urafiki wao ulivyojengeka.
Sasa Henry amerudi nyumbani Tanzania na hii ndo sababu ya Mimi na wenzangu kutaka kuongea nae, imagine kutoka kwenye maisha hayo ambayo na mshahara wake bila ya shaka tunaweza kuukadiria na kuamua kurudi nyumbani, si kwa ubaya… Ila katika nchi ambazo mfumo wa elimu umezeeka nasi ni wa moja wao, mageuzi na mapinduzi mazito yanatakiwa kufanyika pengine haraka iwezekanavyo, je unadhani kwa ugumu wa kazi na vikwazo vilivyopo pengine ndo kilichomvutia yeye? Au kuna jengine ambalo mimi na wewe hatulijui?
Haya yote atatuelezea yeye, maana kati ya vitu ambavyo mimi hu enjoy nikiwa na Kaka yangu huyu ni KUMSKILIZA. Basi tufanye hivyo pamoja na yangu matumaini UTAPENDA.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
10 апр 2022