HAYA MANENO ALITAKIWA AYASEME PALE TU AMRANI ALIPO TOA FATUA YA KUA HAKUNA KHILAFU ULIMWENGU MZIMA UME KUBALIANA!!! AMA KUYASEMA LEO NI DALILI YA KUBEBANA NA HII NI DINI YA ALLAH YENYE MFUMO WAKE HIVYO UKIENDA KINYUME NA MFUMO HUO HATU ANGALII UTU UZIMA WAKO WALA UKALI WAKO WA MANENO!!! WASSALAAM. 🙏
A.alaykum......ALLAH AKUHIFADH SHEKH WETU. UJUMBE HUU NI MZURI SHANA NA NI WAKATI MUAFAKA MANA MASHEKH ZETU WENGI WANAFANYA KAZI KUBWA NA NZURI YA DAAWA ILA KATIKA MAS ALA YENYE KHILAFU HUWA WATUAMBII MISIMAMO YA WENGINE BALI WANA SIMAMIA MISIMAMO YAO PEEKEE NA WANAKASHIFU (BORA WANGENYAMAZA) MISIMAMO YA WENGINE NA KUSHUSHIANA HEAHIMA.HALI HII INATUCHANGANYA SANA MAAMUMA WENU.NA BAHATI NJEMA WENGI WATU WAISLAMU TANZANIA TWAWAPENDA SANA MASHEKH ZETU WOTE HATA KAMA WAO WAKO KATIKA MANHAJI TOFAUTI (MFANO TWAMPENDA Sh.Nudin Kishk pia Twampenda Shekh Othman. Maalum) W TUNAOMBA MASHEKH ZETU KWA UJUMLA WASHIKE NASAHA HII YA SHEKH ABDALLAH BAWAZIR KUWA W ANAPOZUGUMZIA MAS ALA KHILAFIA WAZUNGUMZE NA MISIMAMO YA PANDE ZOTE KWA NIDHAMU NA UASILIFU . SISI TWAWAOMBE MASHEKH WOTE KWA UJUMLA WENU ALLAH AWAHIFADHI NA AKULIPENI ZIADA KWA KAZI NJEMA YA DAAWA MBAYOIFANYA.AAMIN Sisi MAAMUMA tuwe na hekima katika kujifunza toka Kwa MASHEKH ZETU na tuwache ushabiki kwani Kwa Ilmu zetu ndogo tukitia ushabiki tutaangamia. Allah atukinge na Shari ya uchache wa Ilmu na badali twamuomba Allah atupe Ilmu na atuidishie fahamu, Aamin
Maashallah Nimekuelewa na Ninakuheshimu Mno Ila Tukumbuke Kuwa Heshima ni Lazima Mdogo Kidaraja La Elimu Amuhishimu Mkubwa Kidaraja. Muhammad Eid kwa Level yake Lazima Amuheshimu Al Habibi Sheikh Amraan Kilemile Mtume S.A.w Amesema Si Katika Sisi Asiyewahurumia Wadogo wao Na Kuwahishimu Wakubwa Wao na Akawapa Haki Zao.
@@luqmanhamed9710 Ndugu zangu mas'ala ya kiilmu hayazingatiwi ujana wala utu uzima mazingatio ya mas'ala ya ilmu ni hojja na dalili na sio umri wala miaka
@@sheikhsharifmaduatz2871 Asili Ya jambo hili ni Mas'ala ya Dini na Kilichoongelewa ni Tufunge Siku ya tisa Au Siku ya Alafat Ukweli ni Kwamba Maulamaa wa Kishafi na Wengineo Wameikhtalifiana Kwa Kauli Za Kielimu Sasa Katika Mas'ala kama haya inapotokea Sheikh Mwenye Ujuzi Anaongea basi Kama Kujibiwa Lazima Ajibiwe na Msomi wa Level Yake maana Atamjibu Kisomi Zaidi Pasi na Kumkosoa yeye kama yeye bali Kukosoa Ule Msimamo Alioegemea, wakati Huyo Ulamaa wa Pili Akiukosoa Msimamo wa Ulamaa wa Pili atakosoa huku Akijua WanaChuoni Wetu Wa Awali Tunaowategemea Waliikhilafiana Katika Suala hilo hilo kwa Kauli. Atakosoa Huyu Ulamaa Hali akijua Kielimu kuwa Watu Hawatukanani Ktk Mas'ala ya Khilaafiyya Na no Sharti Ajue Unachokosoa Kipo ktk Fani Gani ktk fani za Masomo ya Dini Alafu lazima Kujua Ulamaa wa Fani hiyo Wa Madhehebu ya Shafi, Maliki , Hanbali na Abu Hanifa wanasemaje . Hivyo kuna Adabu kadhaa zinazozunguka Mas'ala haya, tena ningependa Ukumbuke haya ni ya Dini Lazima Yaendewe kwa Adabu
@@ramamtetu2327 Kauli za wanachuoni Wa karne hizi zinaonesha hayo uliyoyasema. Kauli ya shaikh Albany ametofautiana na wanachuoni Wa kale katika hili lakini ameweka wazi kuwa kufunga pamoja ndio kauli yenye nguvu lakini kwake yeye kama Shaikh Albany anaona kila eneo wafunge kwa mwandamo wao kwa hoja na dalili zake. Na wapo wengi katika vigogo vya ilmu kama Shaikh ibn bazz shk. fauzani na wengineo
@@safinabakari9140 Allah Akulipe Kheri , tunataka Waislamu wa Mfano wenu Sio wale Wanaoweza Kusema Misimamo yao kwa Njia ya Ngebe na Nyodo huku Wakionesha Kuwadharau Washeikh Zetu Tena Kwa Mambo Ambayo Wanachuoni wa Mwanzo wameonesha Khilaatlfu Tatizo Kina Muhammad Eid wanatafuta Umaarufu katika Jamii Kiasi Anaongea Bila Kuchunga Uadilifu Tangu lini Advanced Level akawa Sawa na Digrii ? Amuogope Allah Ambae Amewatukuza Wanazuoni
Vijana wengi wanao comment humu yaonyesha wana uchache mkubwa mno wa elimu maana hata adabu ya kusoma hawana ni kumkashifu sheikh na kuwatukana. Anachosema sheikh ni ukweli, kukhitalifiana katika masuala ya kielimu lazina kuzingatiwa kuheshimiana mno na hawakutukanana maimam shafi na Maliki wala hanbal n.k na huo ndio ukweli. Hoja yako hata uipambe vipi inaweza ikawa haipo sahihi kabisa na ile unayoidharau kutoka kwa mwenzio ikawa ndio sahihi. Na Siku hizi vijana hata Quran hawaijui ni masuala ya kipuuzi hushabikia na baadhi ya wasiojua dini wamesoma mada za kubishania wajulikane na wapate umaarufu tu. Lakini kiukweli ni kuwa wamekhitalifiana maulamaa wakubwa ambao hapa Tanzania hakuna hata anayewapata kwa moja ya ishirini ya elimu yao, lakini kila mmoja aliheshimu rai ya mwenzie. Ila hawa masheikh wanaojidai Wao wapo sahihi na webzao ndio wamekosea ni dalili ya upumbavu Wao mkubwa na ukosefu wa elimu. Msimamo kwa mwenye elimu na taqwa ni kuheshimu rai za wengine na kujua mjuzi ni Allah na kutojiona tupo sahihi. Huo ndio msimamo wa wenye elimu. Msimamo wa wapumbavu hujiona Wao wanajua zaidi na wapo sahihi kuliko wengine na huwa tayari kuchunguza na kuwatolea aibu masheikh wengine kabla ya kuwavunjia hoja zao mbele za watu huwatafutia aibu na kuwatangazia. Hao ni masheikh waovu na wajungu.
UMMAH HUU UMEINGIA KTK TAFRIT ZA FIT'NA NA CHUKI ZA KIMADHEHEBU,MPK TWAFIKIA HATUA MUISLAM KWA MUISLAM WANATUKANANA NA HUU NI UFASIKI USIO NA TIJA,,..TAASUB NA MATAMANIO VITATUMALOZA.. #MKAMILIFU NI ALLAH SUBHANA PEKEE#
Sheikh kasema kweli. Tabu tuliyo nayo waislamu hatutafuti mwezi tuna tegeme sikiliza wapi wame ona mwezi Zamani watu walikuwa wakitafuta mwezi kama ume andama hadi kwenye beseni zamaji wakikosa kukamilisha mwezi 30 . Lakini sasa sheikh wangu kasema basi, izo ndio akilizetu zipo Allah atuongoze umma wa kiislam tuache mizozo Amin
@@sakinamubaraka1246 Kwa hiyo kila mtu ana shekhe wake mpaka akisema shekhe wako ndio sa hihi akisema mwingine matusi hajui dharau hii ndio dini inavyotaka jamani
Mudi idi ana jambo nyuma ya pazia. Lkn Allah ndie mlipaji, ikiwa ulilingania dini kwa ikhlas utalipwa, na ukiwa unayatumikia mambo mengine ili maisha yaende basi pia utalipwa tu. Allah hatomdhulumu yyte.
Mashallla sh bawazir kazungumza sahihi hapo zamani hatukhitilafiani sasa tu kila.mmoja kwa sh kuliko mwenziwe Ama iddi ya hajj kila nchi mpka leo wanatafautiana hata mwaka huu pia hiyo ndio sahihi kila.mmoja na muandamo wa nchi yake
Usiseme hoja haieleweki, sema ww hujaelewa. Solution ni ww kusoma. Soma utapata maamuzi ya wapi ni sahihi. Ndio anachotaka shekhe. Na ukali wake ni kwa sbb hataki mashekhe wafarakane ktk mambo ya dini bali wafundishe tu ili mwny kuamini afuate anachokiamini na dini itaendelea
@@mohamedothman9769 nisome nini??. Unataka kuleta miyayusho kwenye dini?. Huwezi kujua Arafah kuliko MASWAHABA. Kina IMAM ALI walifungaje?. Watu walioishi nyakati bora walifungaje Arafah?. Msilete ukisasa kwenye dini. Dini inafuata asili ya maumbile, haifuati maendeleo. Maendeleo yawepo yasiwepo DINI ipo pale pale. Ni lazima tufuate vile vile tulivyoachiwa na MTUME. Kama wao hawakufunga pamoja basi hiyo ndiyo sawa, hakuna cha maendeleo wala mavi yake maendeleo!
Usitumie nguvu nyingi ukatokwa na maneno yasiyofaa, suala la msingi ni kujua unachofanya na kuepuka migogoro ktk dini. Mifarakano haina msaada popote pale duniani
Sheikh yupo sawa na ameeleza vizuri ila Kwa habari ya uhakika MAURITANIA mwaka huu hawakula na Saudi walikula kama tz...mimi nimetoka huko..na wana maulamaa kupindukia...Sasa sheikh inakuwaje hapo...
Mzee wetu anaonekana anatetea upande wake.ikiwa kishiki alisimama mimbali tena siku ya ijuma nakusema kwamba watakaye swali siku yapili niwajinga ao wanatafuta umarfu.mbona hajamkemea kama hataki malumbano?
Hapa hamja gunduwa kuwa huyu sheikh wetu hajaaa tajaa mtu yoyote wala sheikh yoyote bali anaaeleza shida tunazo pataa inapo fika msimu kama huyu wa Ramadhan na arafaa na hiyi anwani inaonyesha vingine hivi ma youtube channel zingine hazina adabu na ma sheikhe zetu chungene sana kwa kushangilia fitnaa
Sheikh umesema kweli hii channel ni ya uchonganishi inamfata sheikh mmoja mmoja inamuuliza unasemaje kuhusu sheikh huyu na inaenda kwa mwingina inamuuliza unasemaje kuhusu sheikh no 1
Sheikh Abdallah Bin Bawaziri Allah akuhifadhi ujumbe umefika lkn naona utachoka tu bure coz hao jamaa akina iddi kazi waliopewa ni kuwagawa waislamu wakiacha kuwavuruga waislamu mshahara hakuna
Wazazi wanapokua kitu kimoja ktk kuwalea watoto kuna 90% za kuongoka kwa watoto hao na kinyume chake ni kuharibikiwa kwa hivyo nyinyi mashekh munatakiwa muwe kitu1 ili dini yetu isonge mbele,ispokua mashehe mpunga ambao itikidi zao sio sahihi hao ndio wa kupambana nao kwa mfano kuna shehe mmoja mpumbavu anakwambia ukimwamini nabii iliyaas hakuna kufa kwa kweli waislmu tunamajukumu mengi kuna watu wangap hawajasimu,kuna watu wangap hawasimamishi swala we must to be careful
aliy maulid: kuhusu yule anajita nabii ilysa, kifupi yule sio sheikh ameisoma dini lkn kwa ajili ya kupotoa. kw7bb yeye kwa mujibu wa maelezo yake anapigana na quran. allaha s.w anasema kila nafsi itaonja mauti yy anasema haamini kufa. kwahiy kapigana na quran.
Je wale waliokuwa wanapita na magari yenye spika na kukufurisha watu mbona hamsemi mlikaa kimya kueni waadilifu ktk msiegee upande mmoja SHK MOHD IDDI yuko sahihi mawahabi acheni kuleta firqa sisi popote tulipo tutaheshimu MUFTI anavyosema
Soud alhatham. Hizi chuki zako yaonyesha wazi kuwa elimu yako ni mdogo mno kuliko chochote. Kwa hiyo maimam Wote wanaosema arafa ni moja ni mawahabi? Kwa hiyo kama mnavyodai mawahabi huvaa nguo fupi na kufuga ndevu na mtume s.a.w alikuwa wahabi? Haya niawazo ya wajinga na masheikh zao wajinga mno wanaowafundisha hayo maana mtume s.a.w kasema ما أسفل من الكعبين من الإزار فهو في النار، Kilicho zidi fundo mbili za miguu ni cha motoni." Hadithi sahihi. Na imethibiti mtume hakuvaa zaidi ya hill. Pia alifuga ndevu na yote hayo tumeshuhudia anayeyafanya huitwa wahabia. Nimelipenda hill jina la kuitoa wahabi maana wanaolitumia hilo kuitoa wengine ni wapumbavu wa kupima mambo mno.
Mimi ninaona east Africa pekeake ndio ina mzozo kuhusu hii arafa lakini karibu nchi nyingi duniani siku ya arafa ni moja ingawa wanatofautiana masaa lakini ikifika arafa wote wanafata saudia sasa sijui labda ndio tuseme hawana uelewa mkubwa huku kwetu ndio kone uelewa mkubwa?wallah huu ni mtihani kwakweli
Asriya Aljabri mashallah.. ndio maana mahujaj wakisimama sehem hyo ya arafa katika siku husika (yaumul arafa) kwa mujib wa hadith ndio sisi tunafunga hyo siku. Na huo ndio usahih wa mambo kwa mujibu wa qauli ya hadith ya mtume عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه أن النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((صِيَامُ يَوْمِ عَرَفَةَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ وَالسَّنَةَ الَّتِي بَعْدَهُ )) أخرجه مسلم
Mimi naomba nijulishwe kwa hiyo.mufti wa Tanzania amekosea kutangaza siku ya iddi na funga ya arafa? Na je ni nani mwenye mamlaka ya kutangaza mwezi .au kila MTU Ana hakki ya kutangaza mwezi?naomba nijibiwe
We BABDEO MILADU hapa kuna cha kujifunza sana acha kuwa double standard, mara umuweke MWAMBUNGU anafanya uzushi wake na unaweka vichwa vza habari vya kiushabiki. Huyu mzee anazungumza haki tupu kuliko lile dude lako linalotumiwa na bakwata kuwapotosha watu.
Ulivoanza bawazir nilidhani unasimama kati ya abuu idd na kilemile kumbe polepole unaangukia kwa kilemile wewe ungebaki kati sawa.Kumbe tunakoelekea tutaipata na hija ya maka na tuko vigwaza hoja ulimwengu wa leo shekhe tuache na muandamo wewe na kilemile bakini na teknolojia
Cha ajabu ni hawa hawa waliokua wakisema : القول ما قال الله وقال رسول الله. Hivi sasa wanatuambia : القول ما قالت وسائل الاعلام. Yaani anasema kua zamani kulikua hamna vyombo vya habari hali ilikua ni vyengine LAKINI SASA VYOMBO VYA HABARI VIPO INABIDI TUVIFUATE. SUALI LINAKUJA HIVI : JEE DINI YA MTUME ILIKUA NI YA MITANDAO AU VIPI !!?? IKIWA MTUME HAKUA NA DINI YA KUFUATA MITANDAO JEE NYINYI HII DINI YA KUFUATA MITANDAO MMEITOA WAPI.!!???. AU KUFATA MITANDAO NDIO : قال الله قال رسول الله. ؟؟؟؟؟؟ ؟؟؟؟؟؟؟؟.
Ili uwatawale watu ni lazima uwafarakanishe. Kinyume chake ni kweli, waislam tunapaswa kuwa kitu kimoja pamoja ma tofauti ndogo sn tulizo nazo ili tuweze kusimamisha kalima Tawheed
@@mohamedothman9769 Umoja wa waislam haupatikani kwa kuswali iddi siku moja. Nawengi wanaosema tunataka tuswali iddi kwa pamoja kwa kufuata muandamo wa saudia basi hao hao ndio wanao farakanisha waislam na ndio walio shikilia mrengo wa takfeer
@@abdulgadiradnan5028 ndio maana ukaambiwa fuata kile unachokijua inatosha. Sasa mifarakano ya nn, muache anayefata muandamo wa Saudia naye aendelee. Au kuna tatizo na hapo?
@@mohamedothman9769 Mashaallah ndugu yangu nakushukuru kwa nasaha yako na kwa hakika usia wa kufuata kile ninacho kijua nimeichukua tangu mwanzo na nitaendelea kufanya hivyo. Lakini tatizo lipo kwa huyu shekhe wetu alipo taka kutilia mkazo kwa lile analo liona ni sawa kwa kueleza kitu bacho sio sahihi pale aliposema kwamba ulimwengu mzima wa arabuni wanatoa iddi na saudia katika mwezi wa dhulhijja na hapo ilibidi tulisahihishe hilo. Na jambo jengine ni pale alipo sema tuache kufuata ya kale tufuate mitandao kwani wale wa kale akiwemo mtume walikua hawakua na mitandao ndio wakawa wanatafautiana katika kutoa iddi ya dhulhijja. Jee pana makosa kusahihisha ambacho hakipo sahihi !!???.
Hadithi gani inasema Tufunge Arafa Mwezi 8? Asokujuwa nani kwamba Wafata Saudia Tarehe Zako Towa Hoja Za Vitabu Siyo Kutowa Kichwani mwako Abuu Idi katowa nawe vipinge majambo tote ya Uislam Yamepatikana kutokana na Mwezi Muandamo Tu iWe Hujja Mwezi 9 iwe Ashuraa Mwezi 11 weramdhani ni kuangalia Mwezi Shekh mnapoteza watu
Na jambo lingine Masheikh wasome zama...Kwani kujua tunaishi kwenye zama zipi itatupa uwepesi kufahamu mengi na kuepukan na MITEGO ya watu wanaotumia UISLAM kama sehemu yakufanikisha mambo yao...Wataalamu wa Anga wa Uingereza huwa wanaeleza mara nyingi mwezi unaotangazwa na saudia kiutaalamu na kivipimo hauendani kiuhalisia...Huku tubaambiwa Saudia wao wanatumia Vifaa vya kisasa kuangalia mwezi...Vifaa gani vinapishana na wengine?mwenye macho na mzima wa akili haambiwi tizama...Kusoma zama punguzo la matatizo yawakabili mwiislam yeyote...والله اعلم
Watu hawana adabu ni viongozi wao. Mufti yupo na qauli ni khilafiyah ukianza kupingana na mufti hadharani na kuunda vya kwako hata kama viko sahihi kwa upande mwingine lkn tambua kwamba huna hiari ya kumpinga kiongozi ukalimega kundi la waislam. Kama humkubali mufti hilo ni jambo lako binafsi ulijengee ukaleta faraka kwa watu
Shekhe ni jambo gani hilo muttafaqun aleih. Wewe ni muongo sheikh au ni mjinga ndugu zipo nchi ambazo iddi yao ya dhulhijja sio ya saudia. Kwa hivyo wewe imma ni muongo au ni mjinga na katika hali zote hizo mbili wewe hufai kufuatwa
@@issarajabu5696 Ndugu mimi sikukata kua huyu ni muongo ungelisoma maandishi yangu vyema ungejua nimesema nini. Sasa kwa mfano wa haraka haraka tu nchi ya oman hawakuwafuata saudia na iddi yao ilikua sawa na iddi ya huku kwetu. Lakini huyu shekhe amesema arabuni yote ilifuata saudia jee huoni kua huyu shekhe hatoki katika hali mbili imma : 1: muongo. Au : Mjinga. Sasa hebu niambie wewe huyu bwana atakua katika hali gani isiyo kua hizo hali mbili.!!????.
@@abuushaukan9828 Hakuna ikhtikafu ktk swaumu ya arafa kwn ilianza kufungwa kabla faradhi ya hija na ilikuwa ikifungwa trh9 dhulhijja kw muandamo sio kutazama watu viwanjani
@@mahfoudhmabrouk809 Mitandao ni bid'a haikuwepo wakati wa mtume wala maswahaba wala karne tatu bora kwa hivyo turudini vile mwezi ulivyo kua ukizingatiwa wakati huo na tusi khalifu eti sasa ipo mitandao kama anavyo dai sheikh bawazir huko ni kukhalifu na hilo ni bid'a.
@@abdulgadiradnan5028 Si kweli kua mitandao ni bid'ah. Hakuna mahala popote ktk uislam kunakokataza mitandao abadan! Halafu kama binafsi yako unaamini hivyo basi huna budi kuacha kutumia hata hiyo simu yako. Pia usipande gari tena wala boda boda wala ndege. Wende hija kwa punda au kwa ngamia . katoe na vile vipaza sauti vyote hapo masjid kwenu na yale mazulia pia yaondoeni maana hayakuwepo wakati wa Rasuulillah wala wakat wa maswahaba wote wanne/wote.
@@mahfoudhmabrouk809 Ndugu si kila siku mnasema kua haifai kufanya ila kile alicho fanya mtume !!??? Mbona mnabadili kauli zenu.!!???. Jee mtume alitumia mtandao katika suala la mwezi !!???. Alaaaa kumbe silazima mtume afanye ndio nasi tufanye !!???. Alaaa kumbe sio kila ambalo mtume hakufanya ni haramu kufanya !!!!. Basi kanuni hiyo mnayonitaka katika mwezi muitumie kwa mengine pia. Nimesoma kwako kua haifai kuharamisha kitu bila ya kua na dalili ya kuharamisha. Basi namaulid ni hivyo hivyo na mengi pia ni hivyo .
@@abdulgadiradnan5028 Hakuna taabu akhy. Jambo la msingi ni kwa sisi wote kuitafuta elimu kwa jitihada zetu zote tena kwa kutaka msaada kwa Allah azza wa jallah. Mifano unayoleta hapa hata haiendani na kitu kilichokuwa kikizungumziwa. Ila kikubwa ilikuwa ni kujaribu kufumbuana macho na si vinginevyo. Namuomba Allah atujaalie kuifahamu haqi na atujaalie wepesi kuifuata na atudhihirishie baatwil na atupe wepesi wa kuiepuka. Allahumma aamiyn! Allahumma aamiyn!
Mzeee hanah hoja huyo uwahabi unamsumbua kisha namshauti aende kwa sheikh mohmad idd ataelekezwa...pia elim za mitandao Kuna sehem hakuna tv wala cm watafanya vipi ibada zao....dini haiendi kwa rai ya mtu....imam ally anasema laiti dini ingelikuwa yaenda kwa rai basi khofu ingelifuutwa chini yaani pa kukanyagia na sii kufutwa juu
Bila shaka umekosa adabu kabbisa kabisa, bila shaka huyu mzee km si umri wa babaako basi anaweza pia akawa babu yako. Km kweli una imani ya dini basi ifute hii kauli yako, lau ukiwa kinyume na hapo basi iache hii kauli ili iwe ushahidi siku ya Qiyama.
Naam kabisa suala halijajibiwa bado tunababaishwa sihoja kusoma hoja ni uelewa na uelewa kila mtu kaelewa vyake sasa kama kuna mitandao ndi inavyosema fiqhi sheria kama tufate Saudi basi kuna na haja ya kuwa mwanamke asikae eda akapimwe na ultra sound akionekana na mimba jawabu Sheikh bado hujaleta hoja kwa mujibu wa sheria ya kiislam mze wetu Mashaa Allah Allahumma Barik lakini bado suala la Arafa lina utata kaeni nyote masheikh wa pande zote mbili muelewane mlichokifahumu na mkosowane mlokuwa bado hamjajuwa kusudio lake khasa watu wanfunga kwa pahala au wanfunga mwezi tisa
Wote hamja muelewa ila mna taassub,amesema kuna wanazuoni kutokana na kukosa teknolojia enzi hizo wakashauri kufunga mwezi nane au tisa ili tu tuwe pamoja na mahujjaaj,lkn bado hujalazimishwa kufata mahujjaj yawezekana ukabaki na msimamo wako huo huo wa kujifanya hujui kama watu wapo arafah
Kadhalika utaulizwa nn hukumu ya ultra sound,wallahy huwez kutoa hojja ktk qur an wala sunnah,ispokua utatoa qaanuuni,hilo sasa laashiria kwamba kanuni hua zunaambatana na zama na hali
IVI BAADA YA KUSHIKA KITABU NA SUNNA KUNA NINI CHA ZIADA KAMA AIO IJMAA MA QIYASI !! TEKNOLOJIA INA NAFASI GANI KATIKA DINI? sawa twende kiteknolojia: je mtu haruhusiwi kupunguza swala akiwa safarini eti kwa sababu anasafiri kiteknolojia ?
Marekani wamepishana sana na saudia lakini arafa ramadan wanafata saudia korea China Australia na nchi karibu zote zinazopishana masaa wanafata saudia huko huko Africa ndio kone mashindano ya kutoelewana mungu atuhifadh
Sheikh wetu punguza jazba.Sheih Iddi allah amhifadh alitowa dalili zavitabu na wew hatujasikia kutoka kwako dalili yeyote .sasa kwaushauri wangu Mze wetu bola ungewashauli masheih yote kuliko kuonekana utatetea upande 1
Shekhe sisi hatukatai kuwafata ktk masuala ya mwezi ila bado hamujatoa hoja tulihitaji mutupe hadithi ya kuwafata mahujaji?!!!!,na pia tulitaka kujua mwaka wa pill hijria zilifaradhishwa iddi fitri,pamoja na iddi Adh-ha sasa mtume alikua anafunga funga gani na alikua anachinja na alikua anasoma takbira miaka 6,wakati miaka yote sita nguzo ya tano haijafaradhishwa(hajji haijafaradhishwa),au ilikuja hadithi ikabatilisha?tupeni ushahidi
Zaid evaris: haya mambo ya dini ni masuala ya kielimu usichukulie kwa ushabiki na kumuita sheikh ambaye ana elimu na hadhi kuliko wewe unasema anabwabwaja kwa kuwa wewe unafuata ushabiki na sio dini. Yeye sheikh ametumia vitabu na wewe unatumia ushabiki tu ukiulizwa huyo abuu idi kayapata wapi hujui ila wewe simba na yanga unayaingiza katika dini. Haya masuala ya arafa hayamtoi mtu katika uislam kwenye kukhitalifiana ila wewe yanakutoa na yanakuweka mbali kabisa na uislam maana unajenga chuki pamoja na washabiki wenzako na unamtukana muumini. Mtume S.A.W anasema " Kumtusi muumini ni ufasiki ( uovu na dhambi) na kumuua ni ukafiri"
@@nahidjhalafamily5987 labda haujamsikia Abu Idi amezungumza akiwa na vitabu 3, cha Uthaimin,cha Alkhalil na Qarar al ulamaa na akasoma hoja na dalili zilizomo humo,sheikh Bawazir anaongea tu na hata akitaja kitabu hasemi hicho kitabu kinazungumza nini
@@canoksancomprehensivelearn7182 nakubali Shekh Bawaziri kanizidi vyote umri,elimu na kutembea ulimwenguni kama ambavyo nakubali shekh Abu Idi kanizidi hayo hayo,mm navyofahamu kubwabwaja ni kuongea maneno mengi bila ushahidi au dalili, nakuuliza ww ambae unajipa mamlaka ya kuwatoa watu ktk dini au kuwaingiza,kwa mujibu wa shekh Bawaziri suala la arafa halina tofauti sababu ya maendeleo ya teknolojia,leo watu wakisimama arafa tunawaona kwahiyo tufunge,nakuuliza ww ukishindwa utamuuliza shk,leo kwa maendeleo ya teknolojia mwanamke anaweza kupimwa na akajulikana ana mimba ya miezi kadhaa na hata jinsia ya mtoto inajulikana swali je kinamama wasikae eda ikiwa vyombo vitaonesha ana mimba ya miezi kadhaa?na je maendeleo ya teknolojia yanaathiri sheria tukufu ya dini yetu ya kiislam?sheria ambayo sifa yake ni kufaa kwa kila zama na kila eneo?