Kila mtu kuna kitu ambacho Mungu amekiweka ndani yake.Kuna nafasi ya wewe kukaa na kupitia hiyo ndipo baraka zako zilipo.Watu wengi wanateseka na kuhangaika kwa sababu hawajui nafasi Mungu alizowapa,na kwa sababu hawajui na kukaa katika nafasi zao,nafasi zao zimekaliwa na watu wengine.Ndio maana kuna vitu ambavyo sio vya haki vinavyotendwa na watu waliokaa katika nafasi fulani.Swali la kujiuliza,ni nani kawaketisha hao katika hizo nafasi?na ni nani ambaye kwa haki alitakiwa akae hapo?nini kimemzuia kukaa?
Je, mahali ulipo ndipo unapotakiwa kuwepo?
Unaposikiliza neno hili kutoka kwa Mtumishi wa Mungu Pastor Sunbella Kyando Mungu akafungue ufahamu wako ili ujue ni nafasi gani iliyo haki yako na akuwezeshe kukaa hapo.
#PastorSunbellaKyando#Ukuta#Yeriko
2 сен 2021