Sh Mohamed mimi nathamini sana sana vipindi hivi unavyoandaa na kwa kweli nafarajika sana sana na uchambuzi wa Mheshimiwa Jussa na sioni sababu ya kumnanga Professor Abdulrahman Babu japokua napingana nae kwa asilimia 60-70 lakini heshima yangu kwake kama mwanamabadiliko na mpambanaji itabaki pale pale … na kwa kweli nimepata moyo sana kuona mpaka dakika za mwisho alitetea alichokiamini japokua si muungi mkono.. OMBI KWA VIPINDI VIJAVYO Tunaomba uchambuzi wa kitabu cha Dr Harith Ghassani “kwaheri ukoloni “ Shukran
Asante sana kwa maelezo yenu. Babu kusema kweli ametoka na ukoo wa Maulamaa wa kubwa na alistahili ashike ukanda wa wazee wake upande wa kwa baba yake kwakuwa yeye ndo alikua mwana mume pekee na ndugu zake wote walikua wanawake. Ukoo wake ni mfupi ulikua unamuhitaji sana kuendeleza mengi na makubwa waliyo yaacha wazee wake. Lakini hakufanya hivyo ndio maana hayo mnayo yasema hakuna na msimamo kamili
Nafrah na najisikia hamu ya kutaka kujua mengi kutokana na kipindi chenu hiki ningependa muendelee zaidi na zaidi Sema kidogo katika kitabu cha leo ckupata nafasi ya kusikia kuhusu kesi iliyomkabiri babu na wenzake ya uhaini na je? aliachiwa vipi. Asanteni tunatarajia mengi kutoka kwenu mwenyezimungu akupeni afya.
Babu anastahiki kuenziwa na kukumbukwa katika histora ya ZNZ. Apewe japo mtaa watu wamkumbuke. Tujifunze kuwaenzi watu kama hawa pamoja na el comandante Ali Mahfoudh na wengine. Kuna mitaa ina majina ya watu wasiotuhusu, wetu wenyewe tunawasahau kwa makusudi. What a shame!
mi nilikuwa naomba jamani hiki kitabu cha Babu nitakipata wapi maana nimetafuta miaka yote nimekikosa nimeonana hadi na mchapishaji mwenyewe pia hana,sasa mwenye nacho jamani naomba anielekeze nitakipata vipi? mana nakitafuta sana.
Babu was the biggest loser katika Zenj Revolution. He was nullified by Nyerere by appointing him in the Union cabinet thereby giving Karume breathing space and freedom to rule without fear of internal challenge.