M/Mungu akipeni afya njema na maisha marefu ndugu yangu Moh'd na ndugu Jussa ilimuendeleze vvipindi kama hivi vya kuelimisha Wazanzibari na wasio Wazanzibari kwa ujumla
Maa shaa Allahu Brother Muhammad tunafaidi sana kwa juhudi zenu zote Allahu subhanahu wataalah atulinde na atupe umri mrefu na WINGI WA Amali njema na mwisho mwema Shukran
John Okello ndio alikua sura ya maasi ya mapinduzi ya Zanzibar 1964,lakini behind yake walikua kina Karume na Babu,kwa upande wa haki wangemlipa pesa kwa kazi alioifamya alafu wangemwambia aondoke. Mr Jussa😁,my deepest admiration to you for emphasising the people of Zanzibar/Tanzania to live and work together to achive a common goal. God bless us all🙏🙏
Kuna haja ya mjadala wa kitaifa juu ya uhalali wa mapinduz ya Zanzibar Maana kila tunapotathmin mapinduz ya zanbar tunahis yameigawa zanzibar na kuacha makovu makubwa
Ni mjadala wa muhimu ila ni mjadala mgumu sana huu ,wengine wayaita Mapinduzi matukufu ... Wengine waoona ni uasi usio na uhalali ... Kuwaleta pamoja makundi hayo mawili ni kazi ngumu sana
Viongozi wetu wa zamani nao wamekua km hawana akili vizur km mazuzu mtu anakuandikia barua tuu ya mapinduzi unakubali John okelo Allah atakulipa kwa unayostahili kulipwa.
OKELO alijipa jina la Mungu wa Africa dhulma mbaya ametumika kutoa uhai watu hatimae amefukuzwa hata pesa hajapewa Allah hutoa hukumu hapa hapa duniani 👊👊👊
Ila mimi kwa hisia zangu nalaani mapinduzi ya Zanzibar japokuwa ninasema ni mapinduzi matukufu... Imesababisha Zanzibar ibaki visiwa wakati Zanzibar ilikuwa ni kubwa kuanzia pwani ya Somalia mpaka pwani ya Msumbiji ila imekatwa na maeneo yao waliyo kodisha yote yamedhulumiwa Zanzibar ilikuwa ni nchi kubwa sana sana Afika mashabiki na kati lakini sasa imebaki visiwa viwili.... Eti Mzanzibar akienda Mombasa aende na anadaiwa paspoti wakati ilikuwa ni nchi yake!!! Alafu mujue hayo mapinduzi ni mpango uliyo sababisha baadhi ya maeneo ya Zanzibar yaliyo kodishwa ya sahaulike yasidaiwe tena..
Waingereza ndio wasaliti wakubwa Walifanya njama askari wazalendo wasiwe na silaha funguo za armoury walizichukuwa Ndio maana kukawa hakuna counter attack Ikawa wenye silaha kuwahujumu wasio Nazo majumbani
Huyu John Okello mafunzo ya kijeshi aliyapata wapi mpaka awe kama tunavyosikia maana sikusikia sehemu yoyote kwenye mazungumzo haya kama alifunzwa masuala ya kijeshi. Hali hii inaniletea mashaka kuhusu yeye: na kuhusu 'yeye' ni nani bado kwangu halijatimilika. Kivipi mtu wa kawaida na amabye historia yake haimuoneshi yeye kama alikuwa na mafungamano ya kisiasa/vuguvugu la ukombozi tena ambaye ni mgeni tu wa takriban miaka mitano (5) Visiwani aweze kuiangusha serikali kimapinduzi?
Kwenye Utangulizi wake (Prologue), Ukurasa wa 20 wa kitabu, John Okello anaandika akiwa Gereza la Kamiti, Kenya mwezi June, 1966: "It has not been easy to complete this book especially with such problems facing me as financial insecurity and travel restrictions between Uganda and Kenya, to say nothing of my imprisonment. I have to thank Mr. Peter Bala, my secretary, for helping me translate my thoughts from Acholi and Swahili into English and for typing the manuscript. I must also thank Mr. Richard Wakohozi for his help with the English manuscript and the East African Publishing House for undertaking to publish my book, even though they may not agree with what I have to say." Kwa hivyo, yeye mwenyewe anakiri kusaidiwa kuandika kitabu hicho.