Walimu hebu waache viboko hata kwa mwezi mmoja tuone! Walimu wengi huwa hawachapi kwa hasira lengo ni kurekebisha! Wenye hasira Mungu awasaidie! Usimnyime mtoto mapigo😊😊😊
Mtu akifanya kosa, akipata adhabu inamsaidia kujitafakari yaani opportunity cost either aadhibiwe au aache makosa. Adhabu ni asili ya binaadamu, hata Allah anaadhibu duniani na akhera. Kila kitu kina wastani wake yaani kufanya kitu kwa kati na kati. Kumuadhibu ndiyo huzaa adabu. Ila ni vizuri kujua tatizo la mtu kabla ya kumuadhibu
Unaweza kutumia fimbo kuadabisha....na si adhabu Kadhalika Unaweza kumuadabisha Mtoto kwa fimbo bila ya hasira Ila hii njia anayoitoa Mwalim si sahihi moja kwa moja.kuna manufaa katika speech yake ila si kwamba kapatia asilimia Mia. Tuweni makini sana hasa sisi Walimu Kadhalika aina ya Watoto tulio nao Dunia ya sasa
Hii ni mateso siyo sahihi kabisa. Adhabu shuleni ni tofauti kabisa na ukatili huu. Chapa na fimbo nyembamba miguuni na siyo na fimbo kama gongo. Halafu kuchapa mikononi ni kosa kubwa sana tena sana
Huna akili wewe na Kama huna chakuchangia kaa kimya, nani kakwambia watoto wa kike ni kosa kuwachapa mikononi?? Mtoto wa kike hairuhusiwi kumchapa matakoni
Idea za kizungu una kitu unataka kukisema ila njia uliyotumia ni mbovu. Waislamu tumeamrishwa kutoa adhabu za makosa mbalimbali ni kuwa huujui uislamu ndio mana
Kila kosa Lina matokeo yanayo umiza hio ni law hata kwenye maisha ukukosea kufanya jambo litakuja na matokeo usiyo ya penda hata amri za Mungu ukishindwa kuzifuata utapata matokeo ya kuumiza so kumchapa mtoto si kitu kibaya ila kinatakiwa kutumika vizuri ili kujenga cuz hata maisha ya mtaani haya tubembelezi tukikosea
Ndo anajutia alichokua anakifanya huku Uingereza walimu hawachap ukimgusa tu mtt unafunguliwa mashitaka unafukuzwa kazi mimi mwanangu anadamu ya kiswahili mama ake nishachapwa huko ninakotoka basi kila week anarudishwa nyumbani 2 days asiende school ndo adhabu anayopewa anaekewa vikao kuonywa anarudi darasani lakini hasikii ingekuwa bongo washamtia ngeu hivi😂😂
Kuadabisha ndio inatakiwa na kuadabisha inawezekana pia kuwa unaweza kumtia adhabu lkn bila ya kupiga Kuna adabu za kulipa , kuandika , kufanya jambo lolote jema Au kumfahamisha na hii ndio nzuri zaidi
Fimbo ilituletea adabu shuleni saiz watoto wameachwa wamekuwa mashoga na wenye dhalau wasio na misingi mizuri acheni huo umaghalibi unahalibu mfumo wetu
Elimu ya africa haina faida. Walimu nao hamna kitu kama ingekuwa na faida mchina asingejenga madaraja wasomi wetu wangejenga ila tumebez kwenye ukatili wa fimbo na elimu haina faida
Ukija kwenye upande wa kusoma na kuhifadhi quran na kuhifadhi kutubi na vitabu vingine yaan kwenye upande wa dini nikisema dini na maanisha uisilamu kuchapwa kuwepo kwa sababu hata mtume ﷴ ﷺ alipewa adhabu na jibril kwa hiyo kuchapa watoto kuna faida pia na mm naona faida ni kubwa kuliko kumuacha nikuchunga t namna ya kumchapa kuchapa kusiko umiza
@@alibinjuma793 kipindi mtume (s.a.w) anafundishwa kusoma na jibril alayh ssalaam, alibanwa mbavu huku akiambiwa "iqraa" yaani SOMA.. huu undo ulikua mwanzo wa kutufikia quran tukufu. fuatilia kisa hiki, utajifunza mengi inshallah
Asiyefunzwa na maame hufunzwa na ulimwengu, haya ogopeni kuchapa watoto ulimwengu ukawachape! na kumbukeni kichapo cha ulimwengu ni kikubwa na hakina vipimo pia hakina lengo la kufunza bali kuadhibu. Wazungu wamefikia wapi katika hili? leo hii watoto wanatukana wazazi wao huko na kuwapeleka polisi kilakukicha kisa wamepewa haki zinazowatoa katika maadili sahihi ya ki-utu. Adhabu ya bakora ilikuwepo kabla ya ukoloni! ... jitieni hamnazo msubiri kuwa na jamii ya mashoga, majambazi, malaya nakadhalika
Mimi nimeona mara nyingi kwenye upapande wa secular walimu wanaochapa sana ni wale ambao walifeli wakahonga na kutoa rushwa na kununua majina mpaka wakawa walimu yaan kiufupi walimu wasiokua na akili
Na kwa mzazi kama mimi nikigundua umemchapa mwanangu kwa namna iliyomdhuru basi huyo mwalimu ajiandae kwa kudhuriwa pia katika muda,mahala nitakapopanga
Katika baadhi yetu Wafrika kuna watu wajinga sijawahi kuona. Hawaoni mzungu hufunza mbwa kujua kushika mwizi wa madawa ya kulevya. Je wanafunzwa kwa kuchapwa...?