Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Doto Biteko amewaagiza viongozi wa Mkoa huo pamoja na Nchi nzima watu wote ambao hawataki kupeleka watoto shule watafutwe mahali walipo na ikibainika serikali iwachulie hatua
ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ilyamchele, Mkoani Geita
“Nimemwambia Mkuu wa wilaya na Mkuu wa Mkoa watu wote kwenye mkoa wetu na nchi hii ambao hawataki kupeleka watoto shule watafutwe mahali walipo ili watoto wale waende shule na kama mzazi hataki serikali chukua hatua” amesema Biteko
15 окт 2024