Ni ya kutoka moyoni hii enyi CCM...au unafiki fulani na kumdhalilisha mtu...pamoja na changamoto zake alizonazo za afya yake? Kwani utaratibu wa Mbowe Mbowe kutumia chopa hauna maelezo na sababu zake? Kwani usafiri anaotumia mwenyekiti wenu CCM ndo unaotumiwa na kila mtu huko? Maridhiano makubwa na upendano wa kweli ingekuwa ni kuacha kutekana, kufunguliana kesi za uongo, kutesana kwa vipigo vya polisi visivyo na sababu, kushirikiana kwa pamoja kujenga mustakabali mwema wa kuendesha nchi kwa kuwa na katiba mpya, tume huru ya uchaguzi na mihimili imara ya kitaasisi ya kuhakikisha kuna utawala bora...kujenga nchi yenye kufuata HAKI! Haya ya kuchangiana, kusaidiana yataoneka mema zaidi katika mazingira ambapo kila mmoja hamtilii mashaka meingine. Yataonekana ni utani wa kweli na si utani wa kushushiana heshima au kumzodoa mtu. Simba a Yanga hutaniana sana na washabiki wa kweli hununuliana hata vinywaji huku wakitaniana. Lakini wapo katika ushindani wa mpira ambao husimamiwa vizuri na kwa haki na waamuzi...japo kasoro zaweza kuwepo za kibinadamu kwa marefa.
Aibu kwa ccm mnayofanya ila nimewapongeza kwa kuwa mmetabili raisi ajaye imekaa vizuri Sana mtaongeza kufanya hayo akiwa anaelekea Ikulu mtenda haki pamoja na kwamba wanaoendelea kumdhalilisha bila 7bu, Lakini ndivyo ukweli unavyokwenda kutumia maana hata Yesu akiwa amebeba hatima ya Dunia alidhalilishwa kiasi Cha kutemewa mate ndiyo maana tupo hapa leo.Tanzania MUNGU anakwenda kutupatia kiongozi wa kutoka kwake ikiwa mifumo ya kuwapata VIONGOZI haitaingiliwa
Nafikiri mmeona ndani ya ccm Lisu anashangiliwa. Msigwa kawaponza indirectly ndani ya ccm wafuasi kibao wamfuata Lisu, maana ilipo mali yako ndipo roho yako ipo.
Mimi na shangaa sana MTU kashiba kande zake huko anasema yafaa kuigwa kitendo cha CCM kuchangu pesa Kwa ajiri ya Kamanda Lissu wameshidwa kumpa HIKI zake za Ubunge Leo change hivyo visendi hivyo ni unafiki TU
nakuambia hivi washaanza kujitafuna wenyewe ccm ndani kwa ndani we unafikiri kinnana kujiudgulu ni mjinga nape kuwa kando ni mjinga yajayo yanafurahisha
Lissu hanunuliwi wananunuliwa wasio na akili timamu kama hao wakina Tomaso mnaowatumia Kijani Chadema ni chama makini sana nasio vyama vingine kama vyo Watanzania CHADEMA ni kweli tusifanye makosa Tena watu watuchangulie hapana
Lisu hiyo hera ikipokelewa atakuwa amekubali kashfa iliyotolewa na Makara pamoja na Msigwa. Huwezi kuzidiwa ujasiri na Hamisa Mabeto aliyekataa Range ya Harmonise kwa ajiri ya diginity yake. Mimi nafikiri hizo hera zirudishwe na wapewe onyo kali kuwa wakome kbs. The way forward, chama kingefanya top up haraka Lisu akanunuliwa Range mpya ili kukata ngebe. Kujikomboa ni pamoja na kukataa dharau.