Pia uwezo wa Kijana huyo musandile ni sawa na uwezo wa wabunge mia wa ccm ,inabidi kama taifa limchukue ajenge nchi ashirikiane na mama na sio kumpiga vita , kwenye masuala ya nchi lazima tuondoe siasa,ndo maaana wenzetu kwenye masuala ya kitaifa wanachukua watu wasomi toka tasisi mbalimbali na sio kuchukua machawa wenye njaa ndo wawe waongeaji hawana Cha maana zaidi ya kupongeza ili kulinda tumbo
Ndile Mungu awe nawe nimebarikiwa sana na hekima zako. Mimi niko na wewe tangu Mbozi mission secondary najua tulivyosaidia watu kutkuonewa tukiwa olevel usitishwe na upotoshwaji huyo jamaa kashindwa kwa jina la Yesu
@@musandile8142Mussa Ndile; maelezo yako ni mazuri na yanaeleweka vizuri,hebu endelea na msimamo wako wa kutetea haki Katika Taifa letu,waamshe na vijana wengine mtetee haki zenu pia mlikomboe Taifa letu kutoka mikono ya Hawa mafisadi, majizi, manyang'au majangiri, majambazi ya rasilimali zetu, usikubali kununuliwa na ccm ukawa chawa! Nchi inaangamia ndugu! Kutawala huu wa sasa wa ccm ni janga kwa Taifa letu! Wanauza kila kitu! Vijana amkeni tuikatae ccm uchaguzi huu 2024/2025 kuanzia wenyeviti wa vitongoji, mitaa, vijiji, madiwani, Wabunge na Rais msiwachague hawa wauza rasilimali zetu ccm! Tusipoikataa ccm sasa hivi huko mbele ni majuto makubwa kwa Wananchi maskini! Asante. Mungu azidi kukulinda daima.
Watu hawaelewi wamejawa na uchawa ,wanao mharibia mama ni wanaccm hawezi mtu toka mbali akaja akaiba ndani ya nyumba bila mwenyeji kuhusika walio soma Cuba wanajua
Hapana msipindishe ukweli hakuna anae mmharibia rais samia, ila yy mwenyewe Rais ndo tatizo. Yy ana Akili pia ana mamlakka, kama anwaacha akiwa anaona wanacho fanya wakat ana mamlaka ya kuwakemea, Inamanisha yy Rais ndo anawatuma That is the meaning. Hawezi kukwepa kuambiwa hilo wakati anawaona na anawaacha waendeleee nayo kama hajalidhika nayo
Na jeshi la akiba maana yake ni nini acheni kuzushia watu uongo huna lolote tukutane kwenye serikari xa mtaa chadema inaenda kushinda kwa upepo wa kisulisuli ushindi wa kivumbi myajua hamjui
Hii nchi Rais wetu inabidi awe makini na hawa anaowaita chawa wake,hawa vijana kutoka CCM ni watu wasiojitambua na ni hatari sana kwa usalama wa nchi yetu,wao wanadhani hii Tanzania ni Mali yao peke yao,wanafikiri Watanzania wengine hawana haki kwenye hii nchi,ebu fikirieni mtu wala sio Kiongozi,anaitisha mkutano na Waandishi wa Habari ili kumtengenezea mazingira mabaya mtu mwingine achukiwe na Rais na vyombo vya Dola vimwone kama adui mkuu wa hili Taifa,huu ni ujinga mtupu na ni upumbavu kutoka kwa hawa vijana wa CCM,lengo lao kuu ni kumshawishi Rais awateue ktk nafasi za uteuzi alizonazo Rais kwa kuwafanya baadhi ya Watanzania wengine wawe na maisha magumu na ikiwezekana wawe wamefungwa Gerezani na hata kuuwawa ili wao kama machawa wa CCM waishi maisha mazuri wayapendayo kwenye nchi hii ya mfumo wa Vyama vingi vya Siasa,ebu tumwangalie huyo kijana Mussa Ndile,kamaliza chuo Kikuu,hakuna Ajira,anajitafutia maisha yake,Kajiajiri,anatokea kijana mpumbavu wa Iringa anataka kumharibia tu shughuli zake ili akapate taabu huko mitaani,huu ni uchawa kama aliokuwa anaufanya Bwana Msiba kwa Watanzania wenzetu ambao sio maadui wa hili Taifa letu la Tanzania,machawa wa aina hii ni washenzi,hatari na ni wa kuupuzwa tu.
CCM chama Cha ovyo sana wanasiasa za kizamani sana.Sijui kwanini wanapenda kudeal na Chadema wakati vyama vya upinzani ni vingi? Kyela Chadema wametoa msaada wa chakula kiongozi wa CCM aliyekipokea katiwa ndani kaambiwa anadhalilisha chama. CCM acheni kunyanyasa watu kama mnaona mnataki kubaki peke yenu,futeni mfumo wa vyama vingi mbaki peke yenu watanzania tujue moja, kwamba hamtaki upinzani.
uyu wa iringa ..akamatwe atoe ushahdi aliyajuwaje hayo na kuthibitisha anayoongea..kwajli anawachafuwa watu..nafki na muongo na uyu ndie anayeandaa..tuache unafiki watanzania
Kaka uko vizuri tatizo la wanaccm wengi ni vizabinazabina,bendera fuata upepo,kazi Yao ni uongo kuchonganisha viongozi ,subiri mtaona wakati wa uchaguzi,2025 ccm itakavyogawanyika vibaya baada ya kura za maoni,Sasa hivi Kuna wabunge waliopita wakati wa jpm wengi Hawana amani ,nakuna kundi linasema ni kundi la mama ! Sasa kama halijawekwa sawa hili heeeeee
Huyu mwanahabari sidhani kama ana nia nzuri ktk kumhoji huyu kijana. Amejibu maswali yote vizuri sana. Musa ni kiongozi mziri sana anayelipenda kazi yake.. Ni watu wabaya wanataka kumchafua tena hawana hoja
Jukumu la mwandishi wa habari ni kuhakikisha anauliza kitu ambacho anayeulizwa atatoa majibu ya kina na kumfanya mtazamaji au msikilizaji kupata uelewa kamili juu ya kilchoulizwa. Mwanahabari/mwandishi hana jukumu la kupaka mafuta kazi yake ni kumfanya muulizwaji kujipaka mafuta
Waliotia hasara nchi katika ripoti ya CAG mnashindwa kudeal nao.Mnadili na watu wa chini.Mnaogopa maandamano wakati hamtekelezi wajibu wenu kutatua kero za wananchi.Maandamano ya wananchi ni ishara kwamba viongozi mmeshindwa kutatua matatizo ya wananchi.
Ndugu zangu watanzania niwaombe kwa moyo wa dhati kabisa tuache kuwalebo watu vibaya. Naieleweke kwamba hapa simu 2000 hatuitaji siasa. Pia taarifa zinazozagaa mitandaoni kuwa hili jambo Nila siasa naomba nimuombe ndugu patrik ajitathimini kwani haya nimaisha ya watu. Pia ingelikuwa ni siasa basi hata wananchi wanaoishi na kupata huduma ndani ya soko hili wasinge tuunga mkono juu ya upazaji sauti.niiombe serekali itutatulie kero zetu pia wapo watu wachache wanao muaribia Rais.
Nawasikitikia sana kwani mnakumbuka shuka wakati kumekucha. Mfumo wowote ukishachoka anguko lake huwa halizuiliki. Jipangeni acheni kutapatapa angalieni kilichotokea kwa ANC. Hata Ile Soviet Union ilisambaratika siyo kwa kupenda Bali ule mfumo wa kikomunist uli - expire na ukasambaratika. Pia kuweni makini na machwawa wenu wanatia madoa kwenye kazi nzuri iliyofanywa na awamu ya sita.
Hilo swala liko wazi maana chadema wameacha kuongea hoja wanazungumzia maswala ya uzanzibari Kwa mama Samia na tuwaambie hayo maandamano tunajua ajenda zenu Hadi issue za kariakoo Sasa hatutakubali mbuzi wawili waharibu amani ya nchi hii lissu anatoa matusi Kila Leo lakini vyombo vya usalama vinaangalia
Kazi ya kuchunguza mambo ya jinai vyombo vya usalama ndiyo vina wajibu,Kama raia ukiona Kuna hali ya hatari mahali Fulani huna budi kuripoti sehemu husika,na vyombo vya usalama tunaviamini Sana sababu wao wanautaalamu huo.Asa huyo jamaa yeye anakitengo gani kwenye vyombo vya usalama.Tusivishushe hadhi vyombo vyetu vya usalama kwa fitina za masilahi binafasi
Vijana kama hawa wanatakiwa kuwa viongozi wa watu wasikilizwe badala yake wanasikilizwa machawa tena ukiwafuatilia hata shule hawana ila uchawa unawafanya kuteuliwa na kuwa ma-RC/DC😮
Wa Tanzania chonde chonde tusianze kuitana majina ya kutisha kwa kufanya hivyo tunapandikiza dhambi kubwa sana Maneno kama gaidi jasusi ni maneno magumu sana Tukianza kuitana au kutuhumu kwa staili hii madhara yake ni mabaya na ile misemo ya Wa Tanzania ni wa moja itaondowa dhana hiyo hapo serikali na vyombo vya ulinzi viwe macho na matamko ya mtu mmoja mmoja kwani yanaweza kuleta taharuki katika nchi yetu pendwa Tanzania
Hao ma-ccm ni waoga pamoja nakuwa na silaha zote za kivita..Maana ni wakati wa WATANZANIA kuikomboa nchi yao mikononi mwao! Wakitambua hilo woga umewameza!
Uchawa tuu jamani huyu naye anatengeneza mtafaruku kwa maelezo yake na pia huyu mtu Nina wasiwasi anaweza akatengeneza kikundi cha vijana cha aina hiyo na kujifanya ni vijana wa cdm serikali iangalie watu kama huyu ni chanzo cha mtafaruku nchini
Wewe kama uliyoyasema kuwa mtu/watu hasa wanasiasa wanayo haki ya kuandamana na kutoa maoni yao sijui Shida iko wapi?halafu unatumia neno taharuki katika maeneo ambayo hayakuhusu unaogopa kupoteza hiyo nafasi uliyonayo ya viti maalum?maoni ya wapinzani wa chama chako yatapelekea kubadilisha sheria zilizopo ukose hata hako kadogo ulikopewa acha makasriko DC
Huyu naye anayesema taharuki maana yake nini, kama ni haki kwanini unasema taharuki!? nawewe umetumia intellensia gani kujua hayo!? Hivi ninyi kwanini mna kudharau kazi ya jeshi la Police!? Tunavyo vyombo makini sana vya kugundua hilo.
Mpango wa siri mipango gani, hayo masilahi mapana ya nchi upana wake nini wakati watoto wanalipishwa hadi mitihani ya moko. Hospitali dawa hakuna, wazee wanateseka hawatibiwi,wamama wanajifungua kwa gharama kubwa.upana huo wa maslahi ya nchi ni upi?
Niuongo niuongo hakuna kitu kama hicho? Watanzania NI waoga sana hawawezi kufanya hayo unayoongea wewe unasumbuliwana njaa fanya kazi kaka maneno hayata kusaidia
Mnaojitokeza tukutugombania wtz kwa sababu gani. Yapo matatizo ya msingi nchi hii ya kumjadili. Tuna tatizo la ajira nchii. Tatizo la msingi sio vyama vyetu. Uchama au mtu mmoja sio tatizo letu. Mikakati ya fursa mbadala badala ya uchuuzi tangia ngazi ya familia Zetu taifa zima.
jamani uyu musa mkweli ..na anaongea ukweli mtupu kuliko huyo mchochezi wa iringa n muongo..wanasaikolojia naomba msaidie hapa..uyo mnene njaa na mnafki na hana elimu na muongo sanaa ..Police nqomba mumuhoji yule mtoa tarifa za uongo ili kupotosha umma