Waziri wa ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amesisitiza kuwa serikali itakamilisha ujenzi wa mradi wa barabra ya kutoka Kabingo mpaka manyovu na kuondoa changamoto iliyokuwapo kwa muda mrefu.
Hivi angezipeleka sehem nyingine mngeshitaki wapi na kumtoa Uraisi hamuwezi, acheni chuki , kwani hela zilizojenga uwanja chato zilitokana na bajeti ipi? Si zilimegwa kwenye bajeti zingine?
Kigoma ilitelekezwa kwa muda mrefu sana! Asante Mama kuikumbuka Kigoma... Endelea na sehemu nyingine za Magharibi na Kusini, hamna maendeleo, barabara za lami hamna, benki hamna, wakati ndio mikoa tajiri kwenye Nchi hii... Inawalisha Wananchi Tz nzima, ila Wakazi wa Mikoa hiyo hawana maendeleo... Sio haki...
Pesa za hii barabara ni za mkopo toka wakati wa Hayati JPM. Barabara hii inaanzia Kibondo, Kasulu hadi Manyovu. Sasa haya maelezo mengine yanatoka wapi?
@@ibrahimallyweunaijuahiyoco8608 penye ukweli uongo hujitenga! Nyota ya marehemu ipo pale pale ndiyo sababu shuleni tunafundishwa kwa mawazo ya watu wengi waliotangulia na hatuendi kuwauliza fomula zao au mawazo yao!
@@MrIsale mama anafanya kitu gani zaidi ya kuendeleza Ilani ya CCM ya 2020-25! Wanaposema yeye ametoa pesa ana utajiri gani wa kulipia hii miradi kama siyo kodi zetu ambazo zinalipa pia na madeni yetu!
Kuna mradi wa barabara inayo Unganisha Mkoa wa Kigoma na Tabora kati ya Nguruka (Uvinza) na Kaliua nyenye kilomita 36 ndio imesimama kwasababu Fedha zinatolewa na Serikali ya Sasa. Hapo alipo waziri, barabara inafadhiriwa na Bank ya Africa hivyo basi haiwezi kusimama hata kidogo. Na JPM kabla ya kuondoka alisema na aliahidi lazima aijenge kabla ya 2025 na sasa kazi inaendelea.