Asante sana Prof. Kabudi. Unaielewa historia ya taifa letu vizuri sana. Kiswahili chako ni cha kuigwa na kila Mtanzania hasa wale wenye ulemavu wa kuchanganya Kiswahili na Kiingereza wakidhani ndo wataonekana wasomi. Unakipa heshima Kiswahili chetu.
Prof. Well done siku nitakutafuta niombe historia hii bora kabisa Mungu akihifadhi na kila lililo ovu na akupe maisha marefu ili tusome mengi toka kwako binafsi saluti kubwa kwako
Asante Profesa na salamu kwa wanasingida. Mheshimiwa kabudi bado nakuomba uongee na Mheshimiwa Raisi kuhusu Mkataba wa Bandari Kwani Mheshimiwa Rasi alituambia wewe ni Mtu wa Mikataba. pamoja na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao kwa kweli unahitaji marekebisho makubwa kwani wazanzibar kwa asilimia kubwa wanasema tanganyika inawanyonya nami sielewi. kabisa Tangyika inawanyojnyaje zanzibar. Mimi Naona tuwe na Nchi Moja tu. na serikali tatu hiyo inahitaji kura ya maoni pande zote Mambo haya naona ni vyema yaongelewe na ninyi wazee sasa hivi. na sio kesho.
Kama huoni Zanzibar inadhulumiwa vipi na Tanganyika basi acha Muungano ubakie hivi hivi lakini sasa mamlaka yote iliyonayo Tanganyika kwa Tanzania sasa ipewe Zanzibar na Tanganyika iwe na Serikali yake kama ilivyo leo Zanzibar. Wazanzibar HATUKUBALI hata siku moja iwe nchi moja, kimsingi hatuutaki tena Muungano kwa sababu Watanganyika wengi hamuujuwi Muungano kwa sababu hauwaumizi, Wazanzibar wote wanatafautiana kusiasa lakini kwenye kudhulumiwa na Muungano wote wanaelewa. Nakutajia mambo machache Wazanzibar hawahawahi kuwa na hata Naibu Spika, Naibu Gavana, kuna taasisi kadhaa za Muungano kama vile NECTA, TCRA, ATCL nk Wazanzibar hawapati hata ujumbe wa bodi achilia mbali management. Kwenye Katiba ibara ya 133 - 144 imezungumzia masuala ya fedha ikiwemo kuanzishwa akaunti ya pamoja, mikopo na misaada, CAG nk mbona ibara hiyo hadi inadaiwa Katiba Mpya HAZIJATEKELEZWA. Fedha ndio uchumi mkiizuwia hapo Zanzibar ndio mumeiua kabisa. Ndio tunasema Katiba mpya tuangalie na tuujadili upya Muungano kwanza tuone uendelee au uvunjwe. Wazanzibar HATUTAKUBALI Katiba Mpya ambayo ni Mkataba mpya bila kuelewana vizuri kwenye hii. Yanayoidhulumu Zanzibar hayatokani na Katiba iliyopo ni kutokutekelezwa tu, kuna assurance gani kwamba Katiba Mpya ITATEKELEZWA 100%?
Singidani NI jina la kimangati ua barbagi pia hujakosea Sana watindiga NI WA barbagi WA mbugani na wanyaturu hawakutokea ethopia wametokea Somalia wao na Watusi waliondoa wakati moja
Amesha ramba asali uzalendo umemshinda sasa anafukuzia vyeo. Tuliambiwa yeye ndio mzee wa mikataba na matumda yake tumeyaona bandari wanakabidhiwa Dubai na watanzania wanafukuzwa kwenye ardhi ya nchi yao wapewe wageni hongera Prof.
Nabii hanaga heshima kwao,,,,,watu kama hawa ingepaswa kuonekana wamekalia ngazi za juu za uongozi wa nchi ili tuyafaidi madini yaliyomo vichwani mwao,,,,ila ndivyo hivyo
Prof. Well done siku nitakutafuta niombe historia hii bora kabisa Mungu akihifadhi na kila lililo ovu na akupe maisha marefu ili tusome mengi toka kwako binafsi saluti kubwa kwako