Kwa kweli mheshimiwa waziri mkuu umetumia busara kubwa Sana, Mungu akujalie, Mimi siyo mfanya biashara Ila kwa kinachofanyika na watu wa TRA siyo sahihi.
Kama ni kweli Waziri mkuu tutakushukuru sana kama hayo unayoyasema yafanikiwe katika ukweli dhulma zimekuwanyingi mnadhulumu sana. Tunakushukuru sana kwa nguvu zako na huruma juu ya wananchi wako Asante sana sana.
Dahaa hiii Tanzania yangu wafanyabiashara wakugoma haraka selekali yangu inawakimbili ila ila mdereva wakisubutu kusitisha huduma tutaambulia vilugu tenaa na kuitwa wahuni hongela mheshimiwa waziri pamoja jopolako 🙏
Asante Baba waziri wetu umetusaidia Sana Mungu azidi kukupa hekima zaidi umeweka sawa wafanyabiashara .Tumekuelewa Sana Mungu ibariki Tanzania bariki viongozi wetu wote wape hekima na maarifa zaidi Amina.
Wtz wenzangu, hii ni siasa ya funika kombe mwanaharamu apite, hakuna jipya. Amkeni amkeni kwa pamoja tuondoe kero hizi kwa kudai katiba, katiba, katiba mpya. Acha kupumbazwa na majibu ya papo kwa hapo, ili mridhike.
Ahsante sana Mhe. Waziri Mkuu. Ombi langu moja, naomba uweke namba za simu ambapo utapata taarifa za moja kwa moja. Kuna uonevu na maumivu mnayoweza kuyashughulikia kwa haraka tu.
Waziri Ubarikiwe kutumiwa kuwatia moyo na Abarikiwe Zaidi Raisi kuwasaidia waone mwelekeo Tunaombea Nchi yetu MUNGU Afanye njia pasipo na Njia ktk Jina la Yesu Kristo Aliyehai MUNGU Tusaidie turehemuu tusamehe Watanzania.
Serikali mnauwezo wa kulisimamia suala hili likakaa sawa Imani yetu ni kubwa sana kwenu lakini kwa hawa mnaowaajiri kutufanyia makadirio wallahi bado mnatuumiza kwa kias kikubwa inafikia muda mpaka tunazichukia biashara zetu kwann laikin
Hongera sana Mh Waziri Mkuu. Pamoja na kwamba ni muhimu sana kulipa kodi na kwamba maelekezo hayo yanaweza yakawaponza wafanyabiashara kufikiri hawatakiwi kufuatiliwa kuhusu kulipa kodi. Elimu kwa walipa kodi ni muhimu ila ni muhimu zaidi kwa wanaokusanya kodi. Wanakua Miungu watu. Yaani akishakua ofisini anaamua kukuambia chochote ila mradi amepata kisingizio chochote cha kumbana mlipa kodi atakoma. Wafanyabiashara wanateseka sana nchi hii. Hata wale waliofanya kazi na Serikali pamoja na shida ya watu wa TRA serikali nayo hailipi madeni hasa yale ya zamani.
Mheshimiwa waziri pole na majukumu kila mafanikio ktk nchi yahitaji uongozi bora umakini na kumwogopa Mungu. Kuna uwezekano wa kukusanya Kodi bila kuleta maumivu kwa wfanyabiashara na wageni wetu kutoka nchi za nje. Binafsi waziri mkuu nakuamini sana Mungu akupe hekima nyingi nchi yetu isimame imara. Na watu wa nchi za nje waje kujifunza hapa kwetu.
Yaani hata huku mabarabarani sisi Madereva wa Malori ni kukaguli njia nzima na hao TRA iwe mchana au usiku, Hata Polisi na wamekuwa TRa hii ni kelo Maheshiwa Waziri mkuuul.
Asante Sana Waziri Mkuu, Umekuwa ukitatua matatizo ya Watoto wa MUNGU wetu, TRA ni Mbwa Mwitu, wa Mjini, Hawa Mbwa Wameuwa Kampuni, yangu ya Ulinzi, Kiponda Security Company Limited, kwa Kunfungia EFD Mashine, Nawalaani wafe Kama walivyoniuwa Kimapato, Mama Samia Hassan Suluhu Hoyee
Jamani kweli imekua sio ile Tanzania tulie itazamia yani 1.mzigo unapoingia bandalini Kodi kibao 2.kodi ya mapato 3.leseni 4.sevice levi 5.fire extinguisher 6.usafi wa taka kajenjere na usafi wa jengo 7.kodi ya flem 8.choo 9.ulinzi 10.umeme 11.wafanyakazi 12.ulinzi st 13.kodi ya pango la st 14. Kuna died stck 15.kodi ya egesho la gari 16. kibari cha TBS 17 Hapo Unasomesha shule watoto ambazo sio za selikari Hebu TRA nao wafungue duka kariakoo walipe hizi zote tuone kama wataweza!!!! Bila kuwa na umoja hii itakula kwetu Bado Tozo ya simu. MUNGU AWABARIKI watumishi wawe na hekima
Yaani Mimi naona hopo selikali ilihifazi yai Zima Ili lialibike, lifike muda muafaka walipasue makusudi halafu wapige deki. Dawa ya yote katiba mpya Tena ileeeee ya warioba.
safi sana.majaliwa kuna.vijamaa vikitoka kitambaa cheupe vinasumbua sana hv vidogo.vya tra na.wale jamaa wa tigo ffu asee wanasumbua.sana watu kutoka.nje ya tanzania wanakufukuzia.mpk vichochoroni
@@blasimassawe4379 ndguu siyo kero tuu zaidi yakero mtu anakukadiri mapato halafu unamuaambia mbona imekuwaa kubwa hivyoo anakuambia eti mbona mkipata faida hamtuambiaa halafu anakujibu hivyo hata biashara ilipo haijui ilipo.
Hasante waziri wetu kututia moyo mama pia ni mama Kuna kitu anakiona na mama ajawahi kushindwa kutatua chochote kinapoingia nyumbani kwake mama ni msikivu tu mama Samia hongeraaa tunakuelewa
MIKODI USUMBUFU HUU UTARATIBU MUMEONA WAPI DUNIANI.... KUDAI RISITI MAJIANI..... MTIHANI MKUBWA NCHI ZA KIAFRIKA KWA NINI HATUTIZAMI WENGINE WALOENDELEA WANAFANYA VIPI KWENYE MIFUMO KAMA DUBAI.....😢😢
Nimekuwa unalalamika kila Siku, TRA wa Vingunguti, Wamenifungia EFD Mashine, na Kusababisha Wateja wangu Wote Kuacha Kampuni yangu, Kufa, Leo hii nateseka Mtaani, Watoto wangu Wanateseka, Mke wangu anatese, Wazazi wangu Wanateseka, Na TRA Mnatanua na Malaya Mabaa, na Kununua Magari ya Rushwa, MUNGU amewalaani na Mtakufa Kama Mbwa Koko.
Watanzania tumesha pumbazwa yaani siasa kidogo bila vitendo tayari anafaa kuwa raisi.... huyu bado sana hawezi kuwa raisi wa watanzania tunayemtaka maana hana alichokifanya hapo zaidi ya kuongea
Hotuba nzuri sana Mheshimiwa waziri mkuu.. Wanatuharibia nchi hii Tanzania is a hub to all landlocked countries lakini sisi wenyewe ndo tunaleta uharibifu.. This is bad.. Rushwa Rushwa Rushwa
Yaani ni RUSHWA tu, kila sehemu ni kukamua watu pesa....watumishi wengi wa serikali sio waadilifu, mpk siku zimwagike damu ndio mtaamka, ...mifumo ni mibovu sana , pesa za serikali watumishi wanatia mikono yao kirahisi sana, hii yote ni kwa sababu ya MIFUMO,...mbona nchi za wenzetu tunaona huku mifumo ipo stebo tu...hakuna huduma utaitaka halafu uombwe RUSHWA, hakuna...kila kitu kipo kwenye mifumo...! Kodi zinalipwa....parking zinalipwa , mtu akiwa mzembe mwenyewe atakutana na fine , bila bughudha wala purukushani mitaani..!..lkn kwetu ajabu , ni vurugu mitaani ....Kiukweli huu ni uzembe wa MIFUMO YA SERIKALI...! BANDARINI mtihani, huwezi kuleta mzigo ukafuta tu utaratibu ukachukua mzigo wako, yaani ni VIPENGELE kuzungushwa ili tu utoe RISHWA...!.. VIWANJA VYA NDEGE mtihani.....yaani unashuka Julius nyerere airport watumishi wanasimamisha watu wanapekua MABEGI bila sababu za msingi, MASHINE za ukaguzi zipo lkn ni RUSHWA tu, mbona viwanja vya ndege vya wenzetu havifanyi huo upekuzi bila sababu....yaani ni AIBU......Hebu rekebisheni MIFUMO YA KODI ...mtu alipe bila KUFUATILIWA MITAANI..!
Kamilishs TRA Kisha angalia tanesco maana sisi vijinini Bora wangebakiza ile 321000 za mjini kuliko ilivyo sasa kwani kama hujatoa zaidi ya million na kuendelea Hadi million 3 umeme utausikia kwa jirani hata wawakilishi wetu madiwani na wenyewe ni wa kwanza kuomba Rushwa
Yan I experienced this on my last landing..perfum 5 ananiambia haziruhusiwi natakiwa kulipia kodi..mtu unashuka pale umechoka hata uelewi..wanakusumbua yan unahesabiwa hadi viatu eti wanakagua kama ni vipya ..mambo ya ajabu mnoo
Mh waziri mkuu sio kwenye soko tu mpaka idara ya maji huku unakuta kwa mwezi bili ya maji inakuja kubwa tofauti na matumizi ukienda kuhoji wanasema kuwa walikosea Ile bili ilikuwa sio yenu ila mwezi ujao tutawapunguzieni Hali ndivyo ilivyo nchini mh wZiri mkuu
Mama alikosea mapema sana alivyoapishwa kua rais kitendo cha kusema yeye sio mkali kama aliepita alikosea kauli yake mbiu kazi iendelee ilikua nzuri. Bahati nzuri anaye waziri mkuu makini otherwise angepata wakati mgumu sana. Kuongoza nchi lazim uwe mkali ukicheka na nyani utavuna mabua
Jamani kama inafikia unafanyika mgomo manaake kuna madudu hapo kwanini musiwachukulie hatua? Waziri mkuu kama mkuu kwann usifukuze kazi mt hapo ili wengine wakae kwa haki fukuzaaaa
Badhi ya mafisa tra wako kwennye magari ya landcruser nyeupe wakiwa na police wanakamata kila gari kukagua na kulazimisha kosa na kudairushwa ukikataa wanakupeleka lumumbaa wameiba sanaaa na kunyanyasa wafanyabiashara tumechokaa rushwa wamekua miungu macho kariakoo imekua kero kuganya biasharaa