Mama wa bilionea Erasto Msuya amegoma kuondoa kesi aliyoifungua mahakama kuu kanda ya Arusha ya kupinga mjane wa mwanaye Miriam Mrita kusimamia mirathi
@@janetsemahimbo8083 adai nn wakati watoto wapo labda wachaga ndo wapo hvyo lakin mm naona vioja kwenye hii familia sijawahi kuona mtu alieacha watoto harafu anakuja kusema Eti Mali zigawanywe Kama jinsi kitabu cha ukoo kinavyosema...kwani wanagawana ukoo au watoto?
Huyo maza syo bure hapo. Tuna anza kupata picha. Huenda huyu maza ana fahamu ukweli kuhusu kifo cha marehemu . Kuna haja Serikali kutoa tamko kunusuru haki za hawa watoto.
We bibi sikupendi wewe unakomaa kwan ujapewa urithi wew na mmewako nae pia ana watoto na mke waachie vya kwao unang'ang'ana hiyo roho mbaya we bibi mishavu bwaju ndy maana mnauwana hovyo wewe mwenyewe utaziacha hizo mali unazozitaka
Huu ni ubinafsi wa hali ya juu! Nakumbuka binamu yangu alizaa na mchaga but mchaga hakulea mtoto lakini alivyofariki familia ile ilimtafuta mtoto wa binamu yangu akarithi mali za baba yake majumba, mashamba, viwanja, miradi na magari walikua hata hawana habari nazo na si kwamba wao walikua matajiri kiivo, yaani kawaida tu lakini wana upendo sana sijui hawa wabakwama wapi aisee dah! Aibu kubwa, natamani washindwe tena kesi mxiuuu
Haiwezekani kufuta kesi katika mahakama yenye mamlaka kamili, ili kesi ikamaliziwe kangaroo court kwa mkuu wa wilaya, ni uhuni tu wa kupora mamlaka kamili ya mahakama. Kesi iendelee tu mahakamani kama hukumu itatoka kuwa mama han chake ni sawa tu lkn uhuru wa mahakama Uheshimiwe
Kusema kweli nashangaa sana watu wanaomlaumu huyu bibi, kikawaida huyu ni mama aliefiwa na watoto 2,wote kwa kuuwawa kikatili, bahati mbaya muuaji wa mtoto wake mmoja ndio huyo aliemsimamizi wa mali za marehemu, na mama wa hawa wajukuu inaosemekana wanagombea Mali, hivi tuvae viatu vyake, je ingekuwa wewe mtoa comment za hasira juu ya huyu mama ndio umefiwa na watoto wako 2 kwa kuuwawa kikatili ungekuwa rahisi rahisi kuacha mali zako zisimamiwe na mtu ambae ndio inasemekana ni muuwaji wa mtoto wako? Kisa kuna wajukuu? Its normal, wacha kwanza na yeye ajaribu kufight black,so far sijaona mjukuu under 18 hapo,hivyo wanauwezo wa kujitafutia mali pia.
Ningekuwa ndio mimi huyo mtoto ningewachana naona ningetamka wazi wachukue kila kitu nikaanza maisha yangu upya halafu tuone iyo Mali hao wanaoigombania itawapeleka wapi mana mwenye Mali kaiwacha
Haya mambo ya mirathi ni tatizo kubwa kubwa kuliko vile watu wanavyofikiria, kila mtu ana penda Mali na kila mtu huvutia upande wake ili apate zaidi kuliko mwingine. Hivi ni nani si wa muhimu ? BABA? MAMA? MTOTO? MKE? Jawabu wote ni muhimu. Kujua ni nani apate nini toka kwenye Mali ya marehem na kwa vigezo gani, hili wanadamu hawataweza kuweka Sheria itakayo maliza matatizo ya mirathi na malalamiko. Kwa sababu hizo na zingine nyingi ndio maana kwenye Uislam Mwenyezimungu ambae anatujua vizuri sisi wanadamu na vile tulivyo akachukua dhamana ya kugawa mirathi yote bila mtu yoyote kuingiza lake. Hivyo mtu akifa Sheria ipo tayari kila mtu ana asilimia zake anagaiwa mambo yameisha hakuna malumbano, wanaopata matatizo ya mirathi kwenye Uislam ni wale wanaotaka, ima achukue kingi zaidi au anataka kumnyima mwingine au hayumo kwenye kundi la warithi ingawa ni ndugu hivyo anataka kulazimisha na yeye apate.
Bibi soma kitabu cha hagai 2 mstari wa nane unasema fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu asema bwana wa majeshi unaweza ukawadhurumu watoto hao lakin usizitumie
Bibi hii Mali si ya ukoo ni ya mwanao na pili je. Mtoto wenu angekua hakuwacha Mali Aina yeyote mngekua mnazozana? Mwogopeni Mungu, malizeni mzozo ili hata marehemu alipo atulie. msifikiri anaraha na nyinyi wakati akiwa hai hamkutaka na ugomvi sasa ameondoka ndio mnaanza
Kwani mbona hayo mbona yako wazi kabisa mrithi wa mali si watoto wamarehemu coz mtoto nimkubwa kabisa huyo. Yani bibi hana aibu huyu sasa mahakama inashindwa nn kuamua jamani, sheria na vikao vya ukoo wapinawapi. Bibi naona anamtaka baba mwenye inchi aingilie laiti angejua baba akiingilia anaweza asipate ata soksi tu ya mtoto wake angeacha tu huyo muro ayamalize.
Aysha Juma sema astaghafiru !! huyo mama ni mzazi wa marehemu na mkaza mwana kamuua binti yake, nduguze huyo mkaza mwana muuwaji ndio wanasimamia mali za mwanae marehemu ambazo kiinimchake ni mgodi wa mumewe yaani baba ya huyo marehemu, MWATAKA HUYO BIBI ASISIMAME KIDETE DHIDI YA JASHO LA MAREHEMU MWANAE QQCHIE UKOO WA WARITA WALE BATA NA JASHO LA MWANAE !?!?! CHUNGUZENI KWA MAKINI MUTAMBUE HAO WAJOMBA ZA WATOTO NDIO WANALETA UKOROFI ILI WAENDELEA KULA MALI 'ATI ZA DADA YAO' KUTAKAPO PATIKANA SULUHI BAINA NA NYANYA NA WAJUKUU ZAKE WAJOMBA WATAKUWA WAPI ???? NJEEEE OUT !!! HIYO NDIO SABABU KESI HAIISHI KILA KESI IKIENDELEA WAJOMBA WANAZIDI KULA BATA !!! MAMA WA MAREHEMU ENDELEA KUTETEA HAKI NA JASHO LA MWANAO, WASIOLEWA WATAKUPAKA TOPE ! SHETANI ANAWAFUMBA WATU MACHO WASIONE UKWELI WA UTETEZI WAKO !!
@@ayshajuma2034 Aysha hebu rudia !!! wewe ni muislamu kweli ?! kasome vitabu vya mirathi ujuwe kila haki ya mtu iko vipi. BUT hawa sio waislamu kwa hivyo tuchukue nafasi kueleza dini yetu waone uzuri na tafauti ilivyo kwenye mirathi. Kiislamu huyo mke wa marehemu angekua ashapata thumni yake na kisha na wengine wakapata zao BAADA YA KUTIMIZA WASIA WA MAREHEMU. Wazazi yaani baba na mama wa marehemu wana haki zao kwa mtoto wao alofariki nayo ni 6% baba na 6% mama then baada ya hapo watoto wanagawana waume mara 2 ya masichana. Bahati mbaya hawa ndugu zetu sio waislamu na sheria ya kikristo kwenye Bible HAKUUUNA MIRATHI ! ndio balaa zote hizi.
@@salmasoso9839 Millioni 200 alizopata bibi sio zawadi !!! bali NI WASIA WA MAREHEMU MWANAE, pili haya yoote niloandika ni kulingana na yale mimi na wewe tumeyasoma So uhakika ni vile kuko na kumesemwa. Wewe waunga mkono mama wa marehemu jasho la mwanaelisimamiwe na nduguze mkaza mwanae ?
Hakuna ujanja ujanja kwenye Mali za watu. Baba anawatoto sawa kimetokea nn mpk kufikia hapo.woote hawaaminian n chuki za hali ya juu.cha msingi mahakama ipo na humpa MTU haki yake kwa alichokifanya.
Uyo mama anapigania urithi uende kwa mabinti zake akidhani kuwa familia ya mrita inachukua mali so zitahama ukoo wakati ni vilevile hata mashangazi wakirithi hizo mali watawapa watoto zao na zitahama ukooo tu
Tatizo hawa ndugu hawawezi kuelewana kwani kuna KIFO kati kati. Mama ana uchungu na kufiwa na mwanae. Sasa bibi atumie busara amemkosa mtoto anaenda mkosa na mahusiano kutoka kwa mjukuu mjukuu
Hivi jamani mbona mimi kama sielewi, erasto si ameacha mke na watoto? Sasa urithi alioacha una uhusiano upi na huyo mama na ndugu? Mahakama impe mali zote za erasto kwa watoto na mke wa erasto full stop
Hao kina msuya hawana lolote ispokuwa wanataka kudhurumu tu hao watt tamaa zimewajaa si kingineo hapo hamuon hata haya mnataka mali za marehemu wakat watt na mke wa marehemu wapo🙄🙄🙄🙄 angelikuwa marehemu kaoa mke lkn hawajazaa harafu anataka mali za mume wake halikuwa hana mtt hapo sawa familia ya marehemu mngezigawanya lkn watt wapo na wanasoma bado mke pia yupo sasa mwavitakia nn kama sio roho mbaya na tamaaa? Mna sahau na kuna watt na mke pia? Hebu serkali iliingilie kat hili jamoon mbona uonevu wa macho macho huu? Magufuli lione hili baba najua ww tamko lako ni la mwisho hakukua na haja ya kusumbua majaji.
BiBi unantafuta laana ya MUNGU ukiwa Mzee,mumeo alikuwa horobo na ukijumlisha uchoyo wako ndo maana hamkutoboa maisha,mwanao akakaza sharubu akatengeneza dira kwa watoto wake,Leo unakuwa bugdha kwa wajukuu zako,badala utubie dhamb za ujana wako unatengeneza na kutunga usaa wa maumiv yako kaburin watu km niny JAMAICA wamesha'wabombo clAtts
Sheikh uktaka kujua huYu bibi SIO itafute hili sakata mwanzo mpaka lilipofkia,hak gan anayoitafuta kashachezea M200 na VTU vague mbaya zaid ahad ya makubaliano alyoyatoa kwa mh mkuu wa wilaya juu ya utenguz wa file ya usimamiz wa mirath na kuuendeleZa kukaza nwaz bib yupo na maslah yake na si kuona wajukuu wake wakisonga mbele, pia kwann bib umeshawah KUJIULIZA?.
Watu bwana,mtu amekufa na ana watoto ambao ndio warithi wakubwa wa mali hizo huyu bibi ameshikilia yy kwenye kufungua kesi zisizo na msingi tuu,hebu mpeni zote izo mali muone kama atavuta miaka mia mbele uyu,kama ni mm ningekua nishatoa maamuzi mapema ujinga ujinga tu
We mama mali zina kuhusu nini mwanao kafa kaacha watoto unahangaika kutwa mahakaman kusimamia za kwako na mumeo unazeeka vibaya tapeli mkubwa wewe nyooo
hakuna utu bila pesa huyu marehemu asingekua tajiri family hii isingeteseka mahakamani kutwa jamani jaribuni kuwa na utu japo kidogo mmpumzishe marehemu kila siku anatajwa kwenye mambo ya mahakama tu hakuna hata siku moja mmetenga muda kumfanyia maombi marehemu duuh pesa wewe
SHIDA NI FAMILIA YA WARITA !!! WAMEKULA BATA KWA WASUYA MPAKA DADA YAO KASHIKWA KWA MAUWAJI, SASA BATA LAWATOKA MDOMONI WANAWATUMIA WATOTO ILI WAENDELEEE KULA BATA !!! MBONA JAMANI HAMUANGALII JANGA HILI KWA UNDANI !!!! KAMA MSUYA ALIKUFA TANGU 2013 KULIKUWA HAKUNA SHIDA MKEWE AKISIMAMIA MALI NA PIA WALIGAWA PESA ZA BANK KAMA ILIVYOANGIZWA NA WASIA WA MAREHEMU NA WATOTO (BADO WAKIWA HAWAJAKUWA WAKUBWA) WAKIISHI NA SHANGAZI ZAO AUSTRALIA NK BALAA ILIZUKA BAADA YA MKE KUKAMATWA KWA TUHUMA ZA MAUWAJI NA ALIPOKUWA NDANI NDIO JAMAA ZAKE WAKAWA WANASIMAMIA MALI, JE MIMI NA WEWE NA MUAFIRIKA YOYOTE MZAZI GANI ATAKUBALI MALI ZA MWANAE WA KIUME MAREHEMU ZISIMAMIWE NA JAMAA ZA MKEWE WAKATI BADO KUMALIZIKA WASIA WA KUGAWA VITU KULINGANA NA VIKAO VYA MILA ZAO ???????!!!! HAO WAJOMBA NDIO SHIDA KUBWA KUBWA KUBWA SANA NA WALLAHI SHETANI AMESIMAMA KIDETE IONEKANE MAMA WA MAREHEMU NDIE MKOROFI AMBAPO SIVYO KAAABISA !!!
Mama ni tamaa ama ? What's wrong with the daughter in law taking care of her husbands wealth of course in future watoto watariidhi incase mama yao hayuko dah some mothers 🙄
@@Bigboy-nx3nc asa kaka mfano mimi ndo mkeo n imekufa sindio alafu wewe ndowakusimamia mali upo gerezani nani atakae simamia na mda huo watoto awajafikia umli wakusimamia
Bibi Mchaga, Babu ndiyo Mpare Wachaga kwa Mali Mnatish!! Familia yote Bibi ndiyo mwenye sauti!! Babu hana sauti anafata Bibi anavyotaka!! Babu anapoteza wajukuu wake jaman!! Wapare tunavyopenda wajukuu ametutia HAIBU!! MFUMWA MRUNGU NI KINI HICHI!! MTUGERA SONI!! HOOO KIDIDI!!
Flora Ngido Mwenzio anapigania mali zisiendee kwa mashemeji na hamna kosa katika hilo. Wapi ulishaona mjomba anarithi mali?.. MALI ZA UKOO HAZIHAMISHWI KIRAHISI HIVYO....
@@Bigboy-nx3nc We sio muhelewa Mali ni za watoto Mjomba ni mama anasimamia tu kwakuwa Mm wa hao watoto yuko jela. Mali haijachukuliwa wao ndiyo wanataka kuzichukua!
Mimi nadhani wengi wanachangia pasina na kufanya utafiti wa kina, mimi kwa mtizamo wangu sioni kama bimkubwa ana makosa kwa harakati zake, kwa sababu kifo ni kifo cha utata ambacho kimetokana na mauaji bali jambo lingine kwa namna nilivofuatilia ni kwamba mke wa marehemu inathibitika kwamba amekiri kumuua wifi yake Aneth Msuya ambaye alikuwa anafanya kazi B. O. T kwa kuchinjwa kama kuku kwa maana ya kwamba huyu mama (bibi wa watoto wa marehemu) kapoteza mtoto wa kiume na wa kike kwa kuuliwa, kwahiyo huyu mama ana kitu tunaita "the wound in the heart" kidonda moyoni ambacho kimechangiwa pia na mkwe wake, hivyo basi mi nadhani ugomvi si Mali bali ugomvi ni kuridhika yule ambaye ameua mwanao aendelee kula maisha na starehe hali ya kuwa wanawe wawili "they have been killed innocently" wameuliwa bila hatia, hivyo basi wanaotoa maoni dhidi ya huyu mama wanatakiwa kuwa waadilifu bali wafanye "critical analysis", huo Ndio mtizamo wangu my brothers and sisters!
Bibi yuko sahihi mnaomlaumu hamjui uchungu wa mtoto hivyo ni lazima Bibi huyu na Mme wake wapewe kiasi cha mali za marehemu mtoto wao yaani hapa ukiangalia ni mgogoro kati ya familia ya Marehemu Msua na Familia ya Mke wa Marehemu Msua japo Familia ya mke wa Marehemu imejificha kwa mgongo wa watoto hapa lazima busara zitumike ili kumaliza mgogoro huu
Hii kesi ni kubwa mno kwasababu inahusiana na mauaji ambayo familia ya Msuya wamepoteza watu wawili alafu upande unaotuhumiwa ndo unaosimamia Mali yaani kwa Akina Mrita , swala liko hapo .na siku zote msimamizi wa Mali ni mke , mke Yuko gerezani inabidi wajomba wasimamie kazi inakuja hapo
BAHATI MBAYA NDUGU ZETU WAKRISTU MUMEPOTEZA MILA MUKAIGA MILA ZA KIZUNGU !!! MALI ZA MWANAE ZINASIMAMIWA NA NANI SAA HII WAKATI MKAZA MWANA WAO YUKO JELA ? WEWE UTAKUBALI MALI ZA MWANAO ALIE FARIKI KAMA MKEWE HAYUPO MALI ZISIMAMIWE NA NDUGU ZAKE MKE ? MUNAJITIA AIBU NA MATAMSHI YENU !! HUYU MAMA ANA HAKI SANA SANA NA USIMAMIZI WA MALI ZA MAREHEMU MWANAE MALI AMBAZO ZILITOKAMANA NA MGODI WA MUME WAKE YAANI BABA YA HUYO MAREHEMU AMBAE ALIKUWA MTOTO WA KIUME PEKEE. MAREHEMU AKIFARIKI WANAE BADO HAWAJAKUWA NA UMRI MKUBWA MPAKA PALE MAMA YAO KUKAMATWA UKOO WA WAKE WARITA WAKAWA NDIO WANASIMAMIA MALI ZA MAREHEMU KISHA SASA WANAWATUMIA WATOTO WA MAREHEMU KUWAGOMBANISHA NA NYANYA NA BABU ILI WAO WAENDELEE KUSIMAMLIA NA KULA BATA BILA AIBU !!!
@@mwanamutemi Lakini bibi na babu walipewa mgao wao na hata Kama jamaa alikuwa anachimba na mgodi Wa Mzee wake basi Mzee achukue mgodi wake mbona msuya alishaanzisha migodi yake??issue Kama watoto Wa msuya wakubwa Sana Bibi na babu walipaswa kuwasimamia wajukuu wapewe Mali zao kisha wawaache...sasa Mara Dada Wa marehemu kachukua mil75 zanini?
@@MtuSafi Sivyo ulivyoandika. Wasia wa marehemu ulisema PESA zilizoko BANK Wazazi wake wapewe 40% STOP ! huo ni wasia. ndipo ikawa 200M kwa baba na 200M kwa mama, Kisha ndipo wazazi katika hizo zao wakatoa 75M wakawapa mabinti zao ambao HAWAMO KWENYE WASIA WA KAKA YAO. NANI ALIHAKIKISHA 40 % YA PESA NDANI YA BANK ILIKUA 400M ? HAKUNA LAKINI WAZAZI WALIPOKEA NA KUANDIKIWA NA KUTILISHWA SIGN KWAMBA WAMEPOKEA PESA KUTOKA ACCOUNT ZOTE ZA MSUYA ZA BANK. Nikikupa ukweli WAZAZI WAMECHEZEWA SHERE HAPA ! Kukeuka wasia ni laana kwa anae kosa kutekeleza haki hiyo, SASA NIKUULIZE WEWE, MKE KAMA UMEKUFA WANAO BADO KUTIMIZA UMRI WA MAJUKUMU KISHA MKE WAKO AWE HAYUKO JE UNGEPENDEZWA NA MASHEMEJI ZAKO NDIO WASIMAME MALI ZAKO ILIHALI WAZAZI WAKO WEKO HAI NA WANA NGUVU ? WASIA WA ERASTO MSUYA HAUKUWA PESA ZA BANK PEKE YAKE, KUNA HISA ZA MAKAMPUNI NA HOTELI AMBAZO AMETOA KWA ASILIMIA KILA AMTAKAE KAMUANDIKIA, HIVYO BASI NI KUSEMA WAZAZI WANA ASILIMIA FULANI ZAO AMBAZO WAKUZIPATA WAKATI MKE WA MSUYA AKIWEKO, LEO YUKO MAGEREZA NA WAZAZI WATEGEMEE HISA YAO WALETEWE NA NDUGU ZA MKAZA MWANA WAO ???! TULIZENI BONGO MUMUELEWE MAMAKE MSUYA NA MACHUNGU ALOYABEBA
@@mwanamutemi nimekuelewa kiasi tuu,Ila yule mama hana machungu yoyote kwanza ni mtu mzima hakutakiwa kuongea kwenye camera kitu ambacho tunaona kwamba wazee Wa Leo ni wazee vijana bibi anapenda Mali Kama msichana...mjukuu yule sio kupangiwa apewe chake kwani tatizo nn asipewe chake?...Yani yule bibi sio mtazamo Wangu Bali watanzania wote wanashangaa Hii familia mana hata mm binafsi sijawahi kuona tukio Kama hili...wanamwambia mshkaji et akasome ndo aje kusimamia Mali hvi kuna somo la kusmamia Mali kweli?...AnyaWay wacha wazulumiane mana wengine hata huyo Erasto hatumjui Ila tunachangia mada sababu yameletwa mtandaoni.
@@MtuSafi kweli sana lakini mambo haya huwa ni funzo kwetu tulo baki hai. Mimi namuunga mama mkono kabisa. wewe wasema hana machungu ! kumbuka huyu mama amepoteza mwana wa pekee wa kiume Msuya, Baada ya hapo mkewe msuya kahusika kumuua binti ya mama huyu huyu, Baada ya hapo IWAPOTEZA WAJUKUU SABABU YA WAJOMBA WA HAO WAJUKUU KUPAPIA MALI ! MACHUNGU SI MACHUNGU !! Narudia tena nukta muhimu ambayo watu hawaioni, Msuya alifariki 2013 na mambo haya yameanza 2017 tena yameanzia kuuwawa kwa dadake Msuya ? huyu kijana saa hii ana miaka 20 babake akifariki alikuwa miaka 14 na akisoma nje chini ya mashangazi zake. 2017 mamake aliposhikwa wajomba zake wakawa wanasimamia mali, mashangazi walipotaka kujua mambo yanaenda vipi wakagundua hao wajomba wanafuja mali na ndipo wakaingilia kuuliza pamoja na wazazi WAJOMBA kugundua itakua ngumu kwao wakamuingiza kijana kwenye sakata ili kijana awe ndie mlalamishi. WAJOMBA AMBAO NI WA UKOO MWENGINE WANGEONDOKA KWENYE SHUGHULI ZA MALI YA UKOO MWENGINE SABABU HUYO KIJANA NI UKOO WA MSUYA WALA SI MRITA UKOO WA MAMAKE, HAWA WAJOMBA WANAMTAFUTIA HUYU MTOTO WA MSUYA LAANA KUTOKA KWA WAZAZI WA MAREHEMU BABA YAKE !! NAAMINI WAJOMBA MHAO WAKIKAA KANDO, WAZAZI WA MSUYA NA WANAWE WOTE WATAPATANA NA MALI ZA MSUYA HAZITAKUA NA MGOMGORO WOWOTE !!!