Waafrika tuache upumbavu huu wa daima kuweka nguvu zetu zote kwenye kandanda ya Ulaya na kushindwa yetu. Tunajua kuchambua timu zao na kuzifurahia utadhani ni timu za Afrika. Ukiwauliza wazungu juu ya soka la Afrika hawana habari na wala hawana mpango wa kulifuatilia. Waafrika sijui nani alituroga? Tuko kama mazezeta. Tunaishi Afrika lakini daima macho yetu yako Ulaya na Marekani. Kazi ni kusifia vya wazungu. Nao wanatumia vyombo vyao vya BBC,DW, SAUTI YA AMERIKA kuhakikisha tunaendelea kuabudu ngozi yao na utamaduni wao. Sijui ni lini Waafrika tutazinduka usingizini?
Kujiuzulu kwa iyo general ni sehem ya uwajinikajo,uwazi na democrasia ambayo Tanzania na mataifa mengine Africa mashariki haipo wajifunze kuwa wasikivu kwa raia wao