Luka 10:19
[19]Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Huwezi kukanyaga kitu kilichopo juu yako,Yesu anaposema kuwa amekupa amri ya kukanyaga nyoka na nge kwa maana nyingine ni kuwa kuna nafasi katika ulimwengu wa roho ambayo hizi nguvu za giza zimewekwa,yaani chini ya miguu yako.Na kama adui anajua kwa miguu yako utamkanyaga yeye na kazi zake zote ndio maana katika vitu anaviwinda kuvikamata kwa binadamu ni miguu.Ulishawahi kujiuliza kwanini wachawi au washirikina huchukua mchanga wa unyayo wa mtu alipokanyaga?au kwanini umekuwa ukiota umefungwa na minyororo miguuni?
Ukisoma Ayubu 13:27-28
📝Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu; Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.📝
Imeelezea vizuri sana.Mkatale maana yake ni "mnyororo".Ukifungwa na mnyororo kuna hatua zako na njia zako zinakuwa zimezuiwa na huwezi kusogea zaidi ya urefu wa mnyororo huo.Ndio maana kuna vitu vikubwa unajua kabisa una uwezo wa kuvifanya lakini hata ukijaribu vipi unaishia kushindwa lakini vya chini yake unavifanya vizuri na kwa ustadi..kuna mnyororo uliofungwa na unaweza kuvifanya vilivyo ndani ya urefu wa huo mnyororo.Ndio maana kuna familia ambazo kwenye kuishi hawazidi umri fulani, kwenye kupata kipato hakizidi kiwango fulani,kwenye uzao hawazidi idadi fulani ya watoto n.k na hata wakijitahidi vipi kusogea wanashindwa.
Huyu mtu hawakuishia tu kumfunga kwa mnyororo bali wameua na mapito yake yote.Kuna maono makubwa ambayo alikuwa nayo lakini tangu amefungwa hata hayo maono hana tena maana amehamishwa na kwenye njia ya kusudi lake.Anasema amekuwa kama kitu kilichooza na kusinyaa.Hakuna mtu anayeweza kukaa karibu na kitu kilichooza,yaani kwa huyu mtu kibali chake pia kimeondolewa,watu wanamkwepa..kwa ufupi amekuwa na roho ya kukataliwa.Lakini ukiangalia haya yote yanayomtokea yameanzia kwenye miguu yake kufungwa.
15 фев 2022