Je? unakumbuka kile Kijiji cha Kutoka Shambani Cha Mrisho Mpoto ambacho alikuwa anakitangaza kwamba anatafuta vijana ambao watakubali kuacha kila kitu, simu, mitandao na vitu vingine ili waingie kwenye kijiji cha Kutoka Shambani kwaajili ya kilimo.
Weekend hii Bongo5TV ilitembelea shambani kwa Mrisho Mpoto, Mkuranga na kukutana na binti Anna Fanuel, ambaye ndiye msimamizi wa mashamba ya Mrisho Mpoto amefunguka jinsi alivyoweza kuendesha kilimo huku akiendelea kuwa mrembo.
Anna ambaye alikuwa Miss Arusha na mwanataaluma wa mahabara, amesema anapenda sama kilimo ndio maana kwake ilikuwa rahisi kuacha kila kitu na kufuata ndoto zake.
23 авг 2024