Huyu Dogo ni Genius sana !!! Una feel kabisa kuwa ana knowdge zaidi!! Nasikia kutoa machozi hawa ni Almasi kwa Africa..anaitaji back up kali sana. Nimeshuudia uvumbuzi kibao lakini system zina let down sana,...TUKIACHA ROHO MBAYA, WIVU, CHUKI, NA UKANDAMIZAJI, KULOGANA....Hawa ma genius wanaweza kabisa.
Jamaa ameifanya sayansi ionekane ni kitu rahisi especially kwa sayansi kama hizo ambazo huonekana kuwa ni ngumu sana kama sayansi ya satellite na rocket. Asante sana kaka kwa kutufungulia njia maana umetupa picha kuwa ata bongo kuna mabrain mijitu yenye akili kubwa ila hawapati Njia au where to start. Serikali kupitia research center au science department sijui but we need to invest Big kwenye izi talent. Kumbe Mungu Tanzania hakutupa tu utajiri wa rasilimali pia Vipaji vipo. Again.. kaka tunakushukuru sana, u just made it look so easy ata mimi nimetamani kusomea yani tofauti kabisa na walimu wetu wanavyotufundisha science SnS asante pia this Content is the Real DeaL
Mimi mkenya lakini nimependa Sana anachokifanya huyu kijana daah,hawa ndio watu tunahitaji kwenye jambi zetu hapa AFRICA hongera Sana brother may God grant good health and long life we need you to inspire the current and coming generations aasante Sana I love this....hata sijui la kusema....
Msomi, genius, Kiswahili kimenyooka anatumia lugha kwa ufasaha wala halazimishi kingereza. Njoo kwa Std 7 failures, anataka kila neno aweke kingereza huku hajui na matamshi hawezi
Hasa ma slayqueens wetu hawa ni shida sana You Know, You Know zinakua nyingi sana kwenye maongezi kiingereza cha kuunga unga sana wanatishia watu... Ila wasomi wenye akili hawana hizi mbanga, kuna jamaa mmoja yule anafanya kazi Boeing ni m Tanzania nae ukicheck interview yake anaongea kiswahili fasaha tu na amekaa sana USA miaka mingi..
Amna kitu bora kama kuwa mzalendo ,umesoma lkn ukarudi Tanzania kuonyesha ulichokipata kazi nzuri zana tukipata vijana kama wewe kumi ambao wamesoma njee na kufika kiwango ambacho umefika na kurudi nyumbani kuendeleza ujuzi Tanzanian tutapiga hatua kubwa sana big up sana
Vijana wapo wengi sana wenye uwezo mkubwa sana wakifanya vitu kama hivi ukweli nikwamba serekali yetu haiko tayari kusaidia vijana wenye vipaji kuwaendeleza
Well done home Boy .. Kazania apo apo .. Nenda Kenya tu apo utapata nafasi na pesa nyingi kwa kazi yako hiyo ..!! Kibongo bongo bado tuko busy tunasifu na kuabudu kwanza ...!! Hawawezi kukuzingatia zaidi zaidi watakukwamisha na kukuvuruga tu ..
Watanzania hawawezi elewa coz hii field hawaijui wachache sana watakuelewa but hongera sana broo umeni inspire sana umetumia alot of money, time keep it up
@@ollymagicswabongo wapi hao wengi unaowazungumzia wewe, shida yetu sisi hatupendi kuona mtu akifanya jambo likafanikiwa tunaanza kwa kukatisha tamaa kwa kuonyesha kuwa yeye sio wa kwanza,
Dah,nimefarijika na kufurahi sana Asante sns Asante kaka yetu kwa Ubunifu huo sisi ambao tuko kwenye industry ya tech tunajua ugumu upi umeupitia mpaka leo hii wazo lako unalifanikisha.Big up brother usikate tamaa,tuko pamoja nawe
Hongera sana huyu ndio msomi wa vitendo hajaenda kukariri kama walio wengi wafanyavyo, wenye kujaaliwa wamsaporti aweze kulikomboa Taifa ktk masuala haya ya kisayansi ya juu
Tunasema tumshukuru Mungu na atuinulie bijana kama hawa,pia serikari inapaswa kuangalia vijana kama hawa na kuwapanguvu vijana wote wenye uwezo wa kutengeneza kitu chochote cha maendeleo ya kiuchumi watumiwe na serikari yao tuweze kujitegemea maana madini tunayo yanayo sapoti vitu vingi vinavyo husiana na sayansi tunaomba serikari itoe nguvu kwa wavumbuzi wote..Mungu ibariki Tanzania 🇹🇿 tuvbariki na vijana wa Afrika.
Viruri sana. Tungekuwa na wasomi wa aina hii angalau wangefanya jambo. Ona wasomi wetu wengine wanavyovuruga taaluma zao, wanadharau utanzania wao, lugha yetu kiswahili, wamejifanya nusu wazungu kiasi kwamba fikra zao na mitazamo yao ni huko walikopatia elimu si tanzania.
Jamaa anafanya Broadcast(Radio&Tv), Telecom, yumo Electronics kwenye components level, Robotics yeye, Aerospace yeye, Astronomy yeye, physicist yeye, Electricity yeye nk..nk. Kweli kijana ana muda wa kufwatilia mambo haya na anajua aisee! Katushangaza wengi😊.
Moja ya mapinduzi makubwa ya kiteknolojia,changamoto ni kwamba hakuna anayeshikwa mkono kuendeleza na kueneza taalaum yake kwa vizazi vijavyo na mwisho wa siku wanapotelea hewani. Fursa hizi zikitumika vizuri pengine siku moja tutakuwa hub ya kiteknolojia badala ya kuendelea kudumazwa na wenzetu waliopiga hatua.
If you are tollerant of constructive critics I can join you to provide with some important info towards your success. Tuanze na challenges to encounter: 1. Sattelite material to protect it from intense temperature variation of +100 to -100 degr centigrade. 2. Satelite productivity is based on scanning surface if the earth which requires continous adjustment of instruments to face the intended surface sector of the earth. This needs automatic change of instruments to face the intended target area of the surface. 3. Proper frequency for long visual line communication which is usually above vhf band (L,S, C ,X Band in GhZ) using effiently solar power provided otherwise there will be not enough power for all instruments onboard. 4. Space is full of storms..radio/solids and hence protection of onboard instruments is important.Otherwise they will be rendered useless within minutes after delivery into space. These are few challenges to be addressed before we come up with practical sattelite. Otherwise lets call the step you are in as a mini weather station. A scientist has to call a spade a spade . Big up for the stage you are towards a long way of satelite making. My salute.
Build your own, he doesnt have to answer none of your questions. Visit him at Olspace if you have anything tangible else you are here to prove what kind of salty hater you are.
Tunaomba muendelezo wa ufafanuzi zaidi juu ya satalite. Pia nikupongeze Mtanzania mwenzetu kwa hatua hii. Niombe serikali yetu kutumia ubunifuu huu kwa Masirahi ya Taifa🇹🇿
Hongera, ila sijui utafanyaje ku-raise fund ukizingatia tanzania hakuna space rocket na serikali tz mara nyingi haiwekezi kwa wabunufi wa ndani tofauti na USA au china, usa taasisi kama darpa na NSF zinawekeza kwa startup zinazotengeneza vitu vinavyo-push teknolojia
if you understand something enough, you can explain it a 7yo kid, what you see is a master at work....Anajua what to talk about and what not to, he is not just a great engineer his communication skill are great, he is down to earth no ego kabisa....keep the work brother, ila hapo kwenye code tupe exp zaidi kidogo next time microsoft code ndo zipi which language exactly? tupia hizo we curious 😅😅
Vijana kama hawa wanatakiwa kupewa sapoti na tuzo .. namfikiria anayafanya haya yote kwa pesa zake mwenyewe , .. yaani natamani zile pesa wanazopewa wachezaji wa mpira kila wakifunga goli wangefanya vivyo hivyo kwa vijana kama hawa safi sana shayo
Hiki ninachokiona hapa ni kikubwa sana! Hii ilipashwa kuwa moja wa mfano wa bunifu za kufadhiliwa moja kwa moja na serikali au hata watu binafsi na mashirika! Ila kwa vile nchi zetu za kiafrika hasa kusini mwa jangwa la sahara hazina muda na wanasayansi wake, sintashangaa kuona bunifu kama hizi zinapotea tu pasipojulikana! Kongole kwake bwana huyu, nimemfwatilia muda mrefu hakika ana kitu kikubwa sana. MUNGU aendelee kumuwema kwa faida ya kizazi chetu sasa na hata baadae.