Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Msingi Igurwa, Adrian Tinchwa (36) kwa tuhuma za kumuua, Phares Buberwa mwanafunzi wa kidato cha tatu Shule ya Sekondari Igurwa.
Taarifa iliyotolewa jana Jumanne Septemba 24, 2024 na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Blasius Chatanda imesema mwalimu huyo ambaye ni mkazi wa Kata ya Kanoni wilayani Karagwe, inadaiwa alimshambulia marehemu kwa kumpiga ngumi kwenye paji la uso na kutumia nondo kumpiga nayo miguuni na mikononi baada ya kumtuhumu kuiba simu yake.
"Tukio hili lilitokea Septemba 18, 2024 saa 8:00 mchana katika kijiji cha Kanoni Wilaya ya Karagwe, ambapo mtuhumiwa awali mnamo tarehe hiyo saa 3 asubuhi, imedaiwa alifika nyumbani kwake na kukuta kufuli la mlango wa nyumba yake likiwa limevunjwa na alipotaka kuingia ndani alikutana na Phares Buberwa mlangoni akiwa anatoka ndani huku akijaribu kukimbia," amesema.
Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi
(Imeandikwa na Ananias Khalula)
24 сен 2024