#ikuluzanzibar #ccm #samiasuluhuhassan #habarimaelezo #ktnnews #wizarayahabari #wizarayakilimo #wizarayaafya #wizarayaulinzi#Tanzania
Na Zaituni Mkwama,
NAIBU Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya amemuonya Mkandarasi anayejenga Barabara ya Maragarasi-Ilunde -Uvinza kwa kiwango cha lami kufuata mkataba wake ili mradi huo ukamilike kwa wakati.
Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 51.1, inajengwa kwa thamani ya shilingi Bilioni 62.7 mkandarasi wake anaelezwa kusuasua na kukiuka matakwa ya mkataba ambao unaelekeza akabidhi barabara hiyo mwezi oktober mwaka huu.
Naibu waziri Kasekenya ametoa agizo hilo mkoani Kigoma mara baada ya kukagua Barabara ya Maragarasi-Uvinza na kusisitiza kuwa hatua ya asilimia arobaini na tano iliyofikiwa kwa sasa haiendani na matakwa ya mkataba.
Awali akitoa Taarifa ya mradi huo Mhandisi mshauri kutoka kampuni ya NORPLAN LIMITED Henry Ngogoloni amesema mkandarasi huyo anafanya kazi kwa kusuasua huku Meneja TANROADS mkoa wa Kigoma Mhandisi Narsi Choma akisisitiza kusimamia zaidi kazi hiyo .
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: / spotileo-176. .
HabariLeo: / habarileo
DailyNews: / dailynewstz
INSTAGRAM;
HabariLeo: habarileo_tz?ig...
SpotiLeo: spotileo?igshid...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: HabariLeo?s=09
28 сен 2023