"Mwingereza alisema hawa watu lazima wapige kura kama wanamtaka Mwarabu au mtu mwingine. Wapatikane watu watano na wapigiwe kura. Kulikuwa na Chama kinaitwa Arab Association wao walikuwa wanataka nafasi ya Sultan waizuie wawe nao na walikuwa wakichochewa bado kuwe na nguvu. Huku kwetu kulikuwa na African Association na Shiraz Association. Ilibidi watu wakawa wazungumze. Mzee Hayati Abeid Karume alikuwa mtu wa 'sports'. Alikuwa anacheza mpira. Alikuwa akienda Dar es Salaam kila Pasaka. Alikutana na akina Bibi Titi Mohammed na Hayati Mwalimu Jk Nyerere walikuwa wakitafuta uhuru. Akakwambia na wao Zanzibar wanaanza harakati za kutafuta Uhuru.
Nyerere alimwambia hao Shiraz ni Waafrika ila walitawanywa ili watawaliwe. Alimwambia waungane ili wawe kitu kimoja. Wakiwa kitu kimoja kama Waafrika watafika mahali fulani. Hakuwa mchoyo alikuwa akitaka maendeleo na kuinua watu" Mama Fatma Karume.
14 окт 2024