#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
NDUGU MHANDISI
Joachim Msafiri Kimaryo ni Kaka yangu na rafiki yangu wa kweli kabisa, mimi na yeye tukiwa pamoja vicheko huwa haviakauki maana tumekutana sote tunapenda sana kucheka na tunapenda utani. Humtania sana kuhusu karibia kila kitu, kampani yake ni moja ya kampani ambazo nazipenda sana. Tunaongelea kuhusu kila kitu mimi na yeye, iwe kuhusu binti yake Nuru kukua na kuwa na boyfriend, au kipaji na muonekano wa baadhi ya wana muziki wa hapa nyumbani, iwe kuhusu Zanzibar na jinsi anavyopata mafua akiwa kule au jokes za ndani kati yetu ambazo mara nyingi zinakua na lugha za kikubwa, yote hayo huongea nae na hucheka sana.
Si mtu ambaye tunakutana kila siku au tunaongea kila siku Ila pale tunapoongea huongea na tunapokutana basi ndo tumekutana. Nna heshima nyingi sana kwake, kwa jinsi ambavyo ameweza ku maintain status yake ila kubwa zaidi ni jinsi ambavyo aliweza kumzidi Marehemu Mzee wake maarifa ki aina na akaweza kufuata roho yake ilichokua inataka na akafanya mziki. Mziki ambao hapa wewe unavyosoma unajua umesaidia kutoa ajira na kubadilisha maisha ya watu wangapi. Na unajua kama Joachim Marunda Msafiri Kimaryo ni mmoja wa waasisi hao. Baba yake alilipia ada ya mwanaye kwenda kusoma nchini Uingereza ili aje apate kazi Tanesco ambapo yeye alikua akifanya kazi, ndo maana alimchagulia mpaka cha kusoma, ila Jay alipifika Uingereza gea ilibadilikia hewani INGAWA alimaliza kwa uzuri tu ile elimu ambayo Mzee wake alikua anataka aipate.
Baada ya kurudi nyumbani sasa, instead ya kwenda kuanza kazi Tanesco ambako nafasi yake ilikua tayari, Jay alitaka kuwa producer na aliweza kufanya hivyo ingawa Marehemu Mzee wake hakupenda, hili ni moja ya maswali nilimuuliza Kaka yangu, kama Mzee wake alishawahi kuyaona hata kidogo mafanikio yake au alishawahi kuskiliza kazi ambazo ni nzuri kijana wake alishawahi kufanya na ambazo zinaishi mpaka leo hii.
Master ametoka kwenye familia za kishua tu, Mama yake Scholastica Sylvan Kimaryo ni mmoja kati ya Ma Coach wazuri tu wa masuala ya kibinadamu na jamii, ashawahi kufanya kazi kwenye mashirika makubwa tu ya Kimataifa na mpaka leo mchango wake bado unatumika kwenye taasisi mbalimbali ili kuweza kuwaendeleza vijana katika nyanja mbalimbali za uongozi na maadili bora. Na Dadake yake Catherine naye pia yuko vizuri tu kwenye masuala ya u coach kama ambavyo Mama yake naye anafanya. So familia iko vyema na mambo yanaenda vizuri tu.
Master ni shule inayotembea, anajua vitu vingi kuhusu karibia kila kitu, ni rafiki mzuri na mtu ambaye mziki huu wa kwetu ameupigania tu sana na pengine wakati wa kujilipa au kulipwa ndo huu umefika. Kwenye maongezi yetu haya tuliongelea kuhusu maisha yake binafsi kama ilivyo ada, kuhusu familia yake na watoto wake lakini pia kuhusu Marehemu Mzee wake na Mama yake na studio yake, miaka ya nyuma wakati wanaanza na mahusiano yake na maproducer wa zamani haswa P-Funk ambaye pia alikua BEST MAN kwenye harusi yake.
Master pia nimeongea naye kuhusu mustakabali wa Bongo Flava, hapa tulipo na huko tuendako, na majibu yake ni kitu ambacho ungependa kuskiliza sana.
Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
RU-vid Link bit.ly/RU-vidSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
5 июн 2022