Wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili ya DW mjini Bonn wamuaga mfanyakazi mwenzao Oummilkheir sauti ya dhahabu ambaye amestaafu baada ya kuhudumu kwa miaka takribani 42. #kwaherioummilkheir
Jina lake ni ishara tosha ya kua mtu mzuri. Ummi= mama Kheir = kheri/mwema Nakupnda sana sana, wengi wanasifu sauti yako ila mimi nasifu lafdhi yako na namna ya unvyokichambwaga kiswahili.
Nafurai kuwaona waandishi wengi tu wa DW,nilikuwa nafikiria Rasid Chilumba na Bruce Amani kuwa ni waxed kumbe hapana,Ma OMil hongera sana kwa yote ulio tufanyizia sisi wasikilizaji wa DW Asanteni kabisa kila la Hero kwa ku stahafu
africa mashariki na ya kati wengi watoto wakike waliitwa kwa jina umul khair ndio sauti nzito kweli weka sign up ile sauti yakufungua radio dw we will miss you mungu akuchunge from kuwait
Hakika nilikupend sana uommi na sitochok kukupend kwa saut yko. Na ekesha wakati ulipokua ukitangaz nilikua nafikiria ni mzungu ambae amejifundish kiswahil. Samaha unatokea wp Mama oummi
Very unique and wonderful voice . All the best Oummi. Kulikuwa na mtangazaji mwingine wa Idhaa ya Kiswahili ya Deutsche Welle ambaye alikuwa anaitwa Osman Mirachi(ji). Alikuwa na kipindi kiitwacho 'Darubini' kila Jumanne baada ya habari ya saa saba mchana ambaye nalikuwa nakienzi sana. Alienda wapi?
Mama yangu hongera sana, nitakumbuka sauti yako daima ila nitakuwa napitia maktaba mbalimbali mtandaoni nisikilize tena na tena. Mungu akujaalie afya njema
Machoz yannitoka tu ila nakuombea kheyr nmemmis mno Mohammed Abdul-rahman na sasa ht sijazoea kumkosa ntakukumbka nawe saaana nkipenda mno ukitaja majina ya Kansela wa ujeruman na Rais wa Uturuki daaah allah akuzidishie kheyr.....
Na Sasa huko ujerumani ,Chancellor Angela marcel ameiba ujerumani kutuma katika ufanisi kidiplomasiiiia,,Na Sasa tuangaaziie huko mashariki ya mbaaaali
Yani nakupenda bure mama yani natamani kukusikiliza kila wakati Kwa kweli kwa hii sauti yako ya kipekee mimi natamani kuendeleea kuisikiliza sauti yako mama Hivi kuna mtu umemwachia hiyo sauti?? Hakika nitaimisi DW kwa ajili yako
Huyu mama kwakweli amekua akinipasha habari na binafsi nimewahi kua najaribu kuongea kama yy. Nimeanza kumsikia hasa taarifa za habari za saa saba mchana tangu nasoma shule ya msingi mpaka nahitimu chuo kikuu. Ni miongoni mwa watangazaji ambao sitaweza kuwasahau kamwe. Mungu aendelee kua pamoja nae daima kama alivyokua nae DW. Kutoka Boooooooo.......nnn
Nahisi natokwa na machozi ya huzuni kuwa sitaisikia sauti ya aina yake ya utangazaji ya huyu mama Oommi ambae amestaafu. Ninamwombea maisha mema uko aendako. Naamini pengo lake haitazibwa.
Mara ya kwanza namsiliza ilikuwa 1998.Ndo nilianza kupata akili yankusikiliza taarifa ya habari.Ubishi ulokuwepo ni mwanaume au mwanamke?Binafsi yeye na Adulhaman Baramia nilikuwa nawapenda sana.Halafu wote wa Comoro
@@abilahirufai8269 ndiyo lkn kwa mujibu wa Maelezo yake Oumilkheir baada ya kustaafu Commoro ni nyumbani lkn pia Zanzibar ni nyumbani kwa hiyo ni Kama ana uraia wa nchi mbili na anapapenda Sana Zanzibar kwani amekulia huko.