Daah mzee anashukrani sana kwa waliomshika MKONO mbali na Madigrii yote hasahau mtu na kama amefariki anamuombea alale mahalapema Peponi hivyo NDIVYO watu hubarikiwa Mungu aendelee kuntunza huyu mzee MWENYE moyo safi
Hongera sana Prof hujasahau lugha yetu!! Maana Hapa Tz Watu waliobahatika kusoma mpka degree moja tu wakiongea Kiswahili huwa wanajifanyaga wanesahau lugha yao ya Taifa iliyowakuza.
Hongera sana Prof. Ingawa mara nyingi wasomi hutengeneza gape kubwa sana ya mahusiano na ndugu zake. Vinginevyo huyu Mgonile ni mfano wa kuigwa. Ombi: Serikali imutumie kama wenzetu kule Ulaya. Mungu akubariki babu Mafwenga.
Daaa, mzee hakua mtu wa kukata tamaa katika malengo yake. Ana uwezo mkubwa sana wa kumbukumbu kuhusu hatua zote alizozipitia. CV yake yote iko kichwani RIP Prof.
Vizuri Sana Prof tunapashwa kukutumia kuzalisha wasomi wengine, uzee nchi unaiachia nini? Basi type ushauri jinsi biashara kariakoo iweje, inaumiza viongozi wetu wapendwa
Mafwenga nilikuwa fundi wake kwa mda mrefu hasa hapo nyumbani kwake namfahamu mno na ni kweli alihamia hapo nyumba haina mlango hata mmoja lakini wahuni kwake hawasogei da
Hawa watu walikua sio Wala rushwa mpaka unamsikia mtu aliefanya kazi adi TRA anasema mshahara ulikua hautoshi akaamua kufanya kazi za ziada huyu mtu hakua mla rushwa. Hawa wazee wanakumbukumbu sana yaan Kila alichokutana nacho anakumbuka. Hii inamaanisha watu wa zaman kidogo hawakua na mambo mengi tofauti na Sasa kwenye utandawazi vichwa vinajaa mambo yasiyo na msingi.
RIP Prof. Mwafwenga tutkumiss sana. Huyu jamaa tulikuwa naye IFM miaka hiyo ya 1992-95 akisoma kozi ya Taxation nasi tukiwa Accountancy. Alikuwa hapendi dhuruma kiasi Viongozi wasiyo wajibika walimuona ni mkorofi. Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amin
Profesa nakupongeza sanaa lakini nakushauri usome Quran tukufu sanaa pamoja siyo muislamu utapata digrii kubwa sanaa mimi kama mwalimu ntaanza kukufunza kiarabu
😂😂 ni mtazamo mzuri. Wanasema money power & respect! Hao uliowataja kua wana pesa ni kwa sababu walikuta wasomi kama huyu mzee wanaumiza vichwa kutengeneza sera, na kuboresha mazingira ya biashara ili hao uliowataja waweze kushiriki shughuli za uchumi ili serikali ipate kodi nayo iboreshe shughuli za kijamii na miundombinu. Kwa pamoja ndio Taifa linajengwa ikiwa kunakuwapo na specialisations. Wote hatuwezi kua traders na merchants, wote hatuwezi kua wasomi kama huyu mzee. Bustani haiwezi kua na ua moja, haitovutia!
Wewe ni msomi gani mkuu unaejenga kaburi na matofali kaburi Bora linajengwa na matendo mema ,lisha mayatima,WAJANE,MASKINI nk,vinginevyo unachezea pesa mzee wetu.
Ila huyu katumia elimu yake na jitihada zake katika kushauri, kuandaa sera mbali mbali za uchumi n.k. vingi alivyofanya ni vitu visivyoonekana au kushikika " non tangible " . Binafsi naweza sema hakuwa bilionea, ila mchangonwake kama ungekua na copyright angekula pesa yeye na kikazi chake chote. Huyu alikua mtumishi wa serikali.
Hongera zake kwa degree na masters... ingawa amesoma sana na maelezo yake lkn sijajifunza chochote na sijaelewa maana ya hizo degree zote ...nimepoteza mb zangu tuu,afadhali ningeangalia mashamsham..😅nina mashaka nyingine amenunua ili aonekane kuwa ni msomi...hahahaaaaa
Ni content adimu sana. Ndio maana unastruggle ku connect. Nikusaidie tu kwamba katika maisha usibweteke na kile ulichokishika sasa, pambaka kupata changamoto kubwa zaidi katika kujijengea kitu unachokitamani. Sasa ifanye katika kutafuta chochote kile, iwe pesa, elimu, umaarufu, uongozi kisiasa etc