Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesimama na kuzungumza na wananchi wa Mji wa Tunduma wilayani Momba wakati akitoka Sumbawanga kuelekea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe uliopo mkoani Mbeya.
Katika mkutano wake wa hadhara na wananchi wa Tunduma, Rais Samia aliwasimamisha mawaziri alioambatana nao ikiwemo Waziri wa Maji, Waziri wa Ujenzi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI iliwaweze kusalimia na kujibu masuala mbalimbali yaliyoibuliwa na wananchi.
14 окт 2024