Mgeni rasmi ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Jennifer Omolo akitoa hotuba wakati akizindua rasmi Bodi ya Ushauri ya Wakala siku ya Ijumaa tarehe 17/06/2022.
Uzinduzi huu ulifanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huu, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala Profesa Geraldine Rasheli alipata nafasi ya kuelezea kuhusu majukumu ya Wakala, utekelezaji wake na mafanikio ikiwemo kuanza kutoa huduma zake kidijitali kupitia mfumo wa kielektroniki wa GIMIS unaowezesha kupata huduma popote ulipo na utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya awamu ya sita katika kutumia mifumo ili kuboresha utendaji. Pia Afisa Mtendaji Mkuu alieleza kuhusu mpango wa Wakala kusogeza vituo vya kutoa huduma katika maeneo ya kimkakati katika ngazi ya wilaya.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala Bi. Dorothy Mwanyika kwa niaba ya wajumbe wa Bodi, menejimenti na watumishi wa Wakala alimshukuru mgeni rasmi kwa uzinduzi huu, na kuahidi kutekeleza majukumu yao ili kuhakikisha Wakala unakuwa endelevu na kuisaidia Serikali na wananchi kwa ujumla.
#GPSATanzania #BohariKuuYaSerikali #UzinduziBodiYaUshauri #GPSAMAB
20 июн 2022