Baraza kuu la Mila ya kimasai Tanzania (Maa) wamekemea vikali kitendo Cha baadhi ya Wazee wanaochangisha kiasicha sh.milioni 2 Kila wilaya kwa jamii hiyo nchini kwa lengo la kufanya sherehe ya kumsimakia kiongozi mkuu wa kimasai (laigwanani) ambapo nikinyume na taratibu za mila na desturi ya kimasai.
Akizingumza kwenye mkutano Mwenyekiti wa malaigwanani Tanzania Aisack Lekisongo amesema kuna baadhi ya Koo ya jamii ya kimasai ziliokiuka kanuni na taratibu za Baraza na kufukuzwa Kisha wakaanzisha kundi lao ambalo lengo ni kua Baraza jipya na kumsimika kiongozi wao ambayo ni kinyume Cha Mila na desturi za kimasai.
7 окт 2024