Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amebainisha hatua za utekelezaji wa miradi ya Sekta ya Ujenzi inayoendelea kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Kagera hususan ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja.
Bashungwa ameeleza hayo Wilayani Muleba Mkoani Kagera katika Ibada ya Shukrani ya Miaka 12 ya Uchungaji wa Askofu Grayson Mutegeki Katunzi pamoja na Harambee ya Ujenzi wa Kanisa Anglikana Mt. Yohana Kimbugu, iliyoambatana na Ibada maalum ya kuwaombea Viongozi wa Kitaifa na Serikali.
#wizarayaujenzi
14 окт 2024