WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amemtaka Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama kujisalimisha kwa Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dar es salaam akiwa na baadhi ya watu waliouziwa eneo la viwanja namba 1 kitalu 22 lililopo Kibada Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es salaam ili kurejesha kwa wananchi eneo hilo liweze kujengwa shule ya sekondari.
Silaa ametoa maagizo hayo alipofanya ziara katika eneo hilo Manispaa ya Kigamboni baada ya mgogoro huo kuwa wa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na baadhi ya watu walionunua eneo la shule akuwemo Allex Msama.
Aidha, Waziri Silaa amemtaja Alex Msama kuwa ni tapeli namba 3 wa viwanja jijini Dar es salaam na tayari ameishaagiza baadhi ya maeneo anayoyamiliki kinyemela kunyang'anywa ikiwemo eneo la wazi na eneo la fukwe lililopo Mbweni Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
Miongoni mwa watuhumiwa wa utapeli wa viwanja ambao tayari wameishatiwa nguvuni ni Johnson Mahururu na Paul Mushi ambao wote tayari wameishafikishwa Mahakamani, ikiwa ni katika orodha ya matapeli 7 aliyowataja Waziri silaa kama matapeli sugu wa Ardhi.
Operesheni hii imekuja tangu kufanyika kwa Kliniki ya Ardhi ya Jijini Dar es salaam iliyoanza mapema mwezi Novemba 2023 na kuhitimishwa mnamo tarehe 3 Machi 2024 kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi iliyokuwa inasumbua jiji la Dar es salaam kwa muda mrefu.
⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 713 750910), ( +255 783453136)
⚫️ Email: globaltvonlinenews@gmail.com
⚫️ OUR PLAYLISTS:
⚫️ MICHEZO na BURUDANI: • Habari zote za michezo...
⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: bit.ly/mikasa_y...
⚫️ GLOBAL RADIO TV: bit.ly/255globa...
⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: bit.ly/exclusiv...
⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: ndstream.net/gl...
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
⚫️ ANDROID:bit.ly/38Lluc8
⚫️ iOS:apple.co/38HjiCx
4 окт 2024