Alhamdulillahi Rabbil'alamiyn. Kipekee nimelifurahia saaana tukio hili ambalo nilikuwa nalisubiria tangu siku nyingi. Mama yangu kipenzi changu Dr. Samia Suluhu Hassan, Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania 🇹🇿 ,Allah akuongoze vema ktk kuliobgoza taifa hili, Na Allah akuhifadhi
It's finally over well done wanaosema Shaun yao the deal is over karibu sana DP world we expect a lot from you people I personally think and believe that you will perform very well karibuni Sana
Dr. Mpango Asante Sana kutuelimisha kuhusu uwezekano wa kuweza kunusuru uchumi na hasa wanyonge WATANZANIA TWENDE PAMOJA KUINUA HALI NA MATIMIZI YA UCHUMI.
Mama wee ni bonge la rais kuwahi kutokea Tanzania kwanza tu nilicho kupendea ni upande wa Tra kwa wafanya biashara sasa ni amani kwenda mbele na watu wanalipa kodi bila shuruti kongole MAMA YETU🙏🙏🙏🙏🙏
Hakika hongera sana viongozi wetu. Tanzania ni yetu, tuilinde sana kwa manufaa ya Watanzania. Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais wetu Mh Dkt Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake ili waendelee kuiongoza nchi kwa manufaa ya Watanzania.
Kuna mtu alisikika akusema "Limkataba la hovyo na la kipumbavu kabisa"hivi bado anaona ni la kipumbavu? Siyo Kila Daktari anatibu na kuyafahamu magonjwa yote. Kadhalika Kila mwanasheria hawezi kujua Sheria zote na hupaswi kutukana Kwa usichokijua.Hongera Mama Kwa uvumilivu wa nafsi na kukaa kimya huku ukisonga mbele.
Imekwenda hiyo.!!!! Kwa heri bandari ya Dar. Manyang’au na mafisadi na mabinafsi yameishaichukuwa. Watanzania wamebaki wanalamba vidonda na kuvuna mabua.
Ni sawa tu kwani Zanzibar imekaliwa na Tanganyika kwa miaka mingapi? acheni mama apige kazi, hata tukiuzwa sawa tu, kwanza wanaume ni wezi, ndio walioufikisha nchi hapa tulipo na umasikini wetu, bora hata mama Samia❤
Mama tunampenda,ilakunawatu wanamwangusha ,nchi jirani Kenya cement ni tsh 11,000/=,hapa kwetu baadhi ya maeneo kama Arusha na kilimanjaro cement ni tsh 17,500/=
Hongera mama. Lkn ninajambo moja tu. Kwenye bandari najua tumefanikiwa, sasa Basi muangalie maslahi na mikataba ya wafanyakazi hususani madereva wa safari za nje. Tunataabika Sana. Kwani Ni tofauti kubwa mno na madereva wa nchi za wenzetu. Mliangalie Hilo. Mungu awabariki.
Kinacholeta wasiwasi ni kusema mikataba hii mi 3 iliyotiwa signs imesimamia mkataba mama ambao ndo ulikuwa mzozo wa shughuli yote ya uwekezaji! Huku inasemekana maoni yamezingatiwa! ATC wazalendo wanasema maoni yao 4 kati ya ma5 yamesimamiwa! Sasa hapo itakuweje Raisi aseme mkataba mama ndo unasimamia hii mikataba mi 3 iliyotiwa sign kati ya serikali ya TZ na DPW!! Sijuhi labda sijaelewa vizuri! Kama nimeelewa vizuri basi maoni hayakusaidia kitu tuombe Mungu wahusika wafanikishe tusizidi kulipa faini za kusitisha mikataba! MUNGU IBARIKI TZ 🇹🇿
Haha serikali ya Tz ikiamua jambo lake hakuna atakae izuia ,,,leo wanasema wamezingatia maoni ya wadau ,,,,sawa lakni sio leo msaini mikataba alafu kesho iwe na mapungufu maana hio kesho wengi wenu hapo hamtakua madarakani hivyo isije ikawa kikwazo kwa vizazi vinavyokuja
Makamo wa rais kasema ukweli tunaishia kimasikini mh rais tunaomba angalau utusaidiee kujenga mfereji daraja la mwinyi mburahati magomeni hakika mama msikivu
Yaani sijui kinachoendelea huo mkataba wanawekeza Kwa sh ngapi sijasikia.na wa mda wa miaka mingapi? Tufafanulieni tujue.siyo tushangilie bila kujua kinachoendelea.maoni yangu yalikuwa taifa kama taifa lingetafuta fedha kukarabati hiyo bandari ili tutapoingiza fedha zote zibakie kwetu siyo kugawana na warabu.alafu huu mkataba tumesaini na serikali ya Dubai au kampuni ya nnchini Dubai.tufafanulieni tuelewe.kwa hiyo bandari baadae kuanza kazi hiyo asilimia 26 ya masikini wa nchi mtatugawia Hela angalau tujifunze kulalia hata magodoro.kwa sababu tumelalia mifuko ya safufeti mpaka mbavu zimeota sugu.
K Yaaani ktk hili hatuwaungi mkono kabisa. Faida na hasara mtazipata m ele ya safari yenu. Na mtu mwenye kichwa kigumu mpaka akutane na rungu limpige kichwani ndipo mtakapo just kwamba swala lilikuwa halifai. Majibu mbele ya safari yatapatikana.