Wataalamu wanaonya kuwa hata afya ya mwili mzima inakua inaathiriwa na afya ya kinywa na meno.
Daktari wa kinywa na meno kutoka Hospitali ya Aga Khan, Masaki, Winfred Mgaya anasema mtu ambaye hana meno mazuri, hushindwa kula vizuri na afya yake inadorora hivyo kuna umuhimu mkubwa wa afya ya kinywa na meno.
Anasema upande wa kutunza afya ya kinywa na meno kuna suala kubwa la usafi wa kinywa na meno wa kila siku angalau mara mbili kwa siku ingawaje hushauriwa kila baada ya kula lakini angalau mara mbili kwa siku.
6 сен 2024