#JAMBOTV
Mkuu wa wilaya ya kisarawe Ndugu petro magoti amewaagiza watendaji wa vijiji na kata kuacha mara moja tabia ya kumaliza shauri zinahusu matukio ya vitendo vya ukatili dhidi ya Watoto badala yake washiriki kikamilifu kufichua na kuripoti uhalifu na wahalifu wa ukatili kwenye vyombo vya sheria.
Mhe. Magoti ametoa agizo hilo Akizungumza na watumishi katika hafla ya makabidhiano rasmi ya ofisi kati yake na Mhe. Fatma nyagasa aliyeamishiwa Wilaya ya kondoa mkoani Dodoma.. Mhe Magoti amesema hawatamvumilia mtendaji yeyote atakayechelewa kutoa taarifa juu ya matukio ya ukatili katika eneo lake.
Katika hatua nyingine Mhe. Magoti amewaagiza wakuu wote wa Idara kuandaa taarifa ya fedha za miradi walizopokea na matumizi ya fedha hizo katika utekelezaji wa miradi husika.
...........
Tufuatilie kwenye mitandao ya kijamii
►RU-vid: / @jambotv908
►INSTAGRAM: / jambotv
►TWITTER: / jambotv_
►FACEBOOK: / jambotv
►WEBSITE: jambo.tz/
12 сен 2024